Bunge letu la Tanzania limekuwa na vitu vikubwa viwili (1) Sehemu ya malalamiko (2) Sehemu ya kusemana vyama vya upinzani na serikali. Hivyo ni vitu vizuri lakini je nani Tanzania anaongelea mbinu mpya za mandeleo kuanzia kwenye elimu, Afya, Biashara, Viwanja na Barabara je mbinu mpya ziko wapi na ni nani anaongea. Pamoja na Maendeleo ya hapa Marekani kila siku kuna mbinu mpya watu wanakuja nazo za kutatua matatizo tofauti kuanzia kuboresha elimu, Afya na biashara. Mimi natafuta kwenye magazeti, bunge na hapa JF watu wenye mawazo mapya ili tukosoane lakini sipati napata malalamiko tu kuanzia bungeni mpaka hapa!. Umasikini wetu unatokana na vitu vingi na ni lazima kila siku tufikirie mbinu mpya za kujiendeleza. Ukifikiria vizuri hata sisi vijana tulioko nje tulikuja kama mbinu ya kujiendeleza hata kama tusikofanikiwa lakini mafanikio hayatatoka kama hubadilishi mbinu kutokana na hali yako.