EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Niliposoma heading hii kwenye gazeti moja nilifurahi sana nikajua rais wangu umeanza kuziona kero za wananchi wako, cha ajabu niliposoma habari yake nikagundua ulikuwa huwaambii watanzania ulikuwa unawaambia watu wa Sudani na Sudan kusini kuwa risasi huwa hazitatui matatizo njia pekee ya kupata majawabu sahihi ya mvutano kati ya pande hizo ni kwa njia ya majadiliano, hata hivyo nikafikiri rais una akili sana kwa kuliona hilo.
Ziko wapi hekima ulizotumia kuwaambia watu wa Sudani, ina maana watu wa Sudani ni bora kuliko watu wa Tarime, Rais wangu kweli nasikitika sana ningekuwa na uwezo ningekuja ikulu kukuuliza hili swali kwanini uhurumie watu wa jirani kuliko watu wa damu yako?
HabariLeo | Kikwete- Bunduki hazitamaliza matatizo yetu
Ajabu rais wangu unaporudi nyumbani akili kama hizo sijui huwa unazipeleka likizo maana watu wanapigwa risasi wala sijasikia ukitoa maneno ya busara kama hayo, asikari wanazidi kuua watu bila huruma tumeshuhudia mauaji ya Arusha baadae Mbeya baadae Tarime jana tumesikia huko Mwanza na Dar es salaam asikari wakiwapiga watu risasi za kichwa sielewi kesho itakuwa zamu ya nani, rais wangu uko kimya kama hakijatokea kitu, hivi tumekukosea nini kiasi kwamba watoto wako huwajali unajali watoto wa jirani? Tuhurumie basi kama tumekukosea.RAIS Jakaya Kikwete ameziambia Sudan na Sudan Kusini kuwa bunduki haiwezi kutoa majawabu ya mvutano kati ya pande hizo ambazo zitatengana na kuwa nchi mbili tofauti Julai 9, mwaka huu, 2011, wakati Sudan Kusini itakapokuwa Taifa Huru.
Ziko wapi hekima ulizotumia kuwaambia watu wa Sudani, ina maana watu wa Sudani ni bora kuliko watu wa Tarime, Rais wangu kweli nasikitika sana ningekuwa na uwezo ningekuja ikulu kukuuliza hili swali kwanini uhurumie watu wa jirani kuliko watu wa damu yako?
HabariLeo | Kikwete- Bunduki hazitamaliza matatizo yetu