nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Bunda
Bw. Kambarage Wassira ambaye ni mtoto wa Mbunge wa Jimbo la Bunda Bw. Stephen Wassira, ameibuka mshindi katika nafasi ya ujumbe wa Mkutano Mkuu Taifa.
Nafasi ya Mwenyekiti wa CCM wilayani humo ilichukuliwa na Bw. Chacha Kimanwa baada ya kumbwaga Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Bw. Erasto Majura na Bw. Mramba Simba.
Msimamizi wa uchaguzi huo Bw. Maximilian Ngesi ambaye ni katibu Mwenezi CCM mkoani Mara, alimtangaza Bw. Bonfas Mwita kuwa mshindi wa ujumbe wa NEC.
Bw. Mwita aliwashinda Bw. Cyprian Msiba ambaye ni Mtangazaji wa Kituo cha Channel Ten na Bw. Daudi Iramba.