mayenga
JF-Expert Member
- Sep 6, 2009
- 4,118
- 1,966
Nilikuwa nazungumza na mzee mmoja, ambaye ni mtu mwenye heshima yake katika jamii na anao umarufu wa haja. Mada yetu ilikuwa ni kuhusu maendeleo ya taifa hili na fikra za watanzania hasa viongozi wa wakati huo.
Mzee huyo ambaye katika kipindi hicho cha uhuru alikuwa shuleni anaeleza mwamko na uelewa mkubwa wa watanzania waliokuwa nao. Matokeo ya fikra pevu za Viongozi wetu zilimfanya Rais wa Marekani kipindi hicho Reagan kuitembelea Tanzania.
Baada ya Rais huyo kutoa sifa lukuki kwa nchi hii,alitoa misaada mingi ikiwemo chakula mashuleni jeshini na taasisi nyinginezo ukiwamo unga maarufu ujulikanao kama Bulgur Wheat. Inasemekana unga huo ilikuja kujulikana kuwa unga ulikuwa na sumu iliyokuwa ikiharibu polepole akili za watanzania hasa uwezo wa kukumbuka na uwezo wa kutoa maamuzi.
Mzee huyu anahitimisha kwa kusema kuwa,vijana wengi waliokula unga huo ndo kwa sasa ndio wanashikilia madaraka, wakiwemo mawaziri, marais, wabunge, majaji, nk na kwa jinsi hiyo ndo maana viongozi wetu wa sasa wamekuwa ni watu wasiokuwa wapembuzi. Wamebaki watu wa kutii kila waambiacho na pengine ubunifu kimekuwa ni kikwazo.
Jamani mimi ni kijana wa 1980 je, mliokuwepo kipindi hicho haya yana ukweli?
Mzee huyo ambaye katika kipindi hicho cha uhuru alikuwa shuleni anaeleza mwamko na uelewa mkubwa wa watanzania waliokuwa nao. Matokeo ya fikra pevu za Viongozi wetu zilimfanya Rais wa Marekani kipindi hicho Reagan kuitembelea Tanzania.
Baada ya Rais huyo kutoa sifa lukuki kwa nchi hii,alitoa misaada mingi ikiwemo chakula mashuleni jeshini na taasisi nyinginezo ukiwamo unga maarufu ujulikanao kama Bulgur Wheat. Inasemekana unga huo ilikuja kujulikana kuwa unga ulikuwa na sumu iliyokuwa ikiharibu polepole akili za watanzania hasa uwezo wa kukumbuka na uwezo wa kutoa maamuzi.
Mzee huyu anahitimisha kwa kusema kuwa,vijana wengi waliokula unga huo ndo kwa sasa ndio wanashikilia madaraka, wakiwemo mawaziri, marais, wabunge, majaji, nk na kwa jinsi hiyo ndo maana viongozi wetu wa sasa wamekuwa ni watu wasiokuwa wapembuzi. Wamebaki watu wa kutii kila waambiacho na pengine ubunifu kimekuwa ni kikwazo.
Jamani mimi ni kijana wa 1980 je, mliokuwepo kipindi hicho haya yana ukweli?