Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
Kuna baadhi ya mikoa hapa nchini hususan Kagera hasahasa Bukoba hapa mjini, Kyaka Bunazi, Karagwe hawajui kabisaaa kama kuna tatizo la umeme nchini. Wanapoona magazeti yanaandika kuhusu mgao wao wanashangaa akusema eti ni Tanzania wanayoijua wao au nyingine. Nawaomba wawapigie simu ndugu zao walioko mikoani kwingine wawaeleze mziki ulivyo. Bukoba hapo na maeneo wanayoyataja wanapata umeme kutoka Uganda ambao kukatika ni mara chache sana. Waganda wako kibiashara zaidi kiasi kwamba kwao hutokea ukakatika lakini wanaouuza Tanzania haukatiki. Nisaidieni kuwaelezea jinsi ambavyo watu wanaoishi kwa kuuza ice cream hawana kazi sasa hivi, wale wauza maji hawana kazi, na mambo mengine kibao. Wanaofanya kazi viwanda vya samaki hapa wao kila siku wako job, mashine za kusaga wao wako job kila siku, waulizeni wa Shinyanga huko wawaeleze. Waandishi wa habari na sisi vijana wanaharakati hatuzushi. Nchi ina hali mbaya msidanganywe na Geografia iliyowabeba. Mwingine anadiliki kusema eti "kweli wapinzani hamna dogo, mbona umeme hapa una miezi karibia 8 haujakatika hata kufikia muda nusu saa?" ni kweli lakini Tanzania sio Bukoba tu, wananchi kwingine wanatabu bana! CCM wengine watatumia kutoelewa kwa wananchi waseme wapinzani wazushi, kisa kelele za umeme wakati hawajaona umekatika. Wasiofikiri wataamini. Mwenye kuamisha kiwanda akilete huku azalishe na sio siasa za kuwadanganya watu kuwa nchi nzima ina umeme.