Budget ya mwaka 2011/2012-tanzania

Mkombozi

JF-Expert Member
Feb 19, 2008
805
425
Wakuu, kama tunavyojua budget ya 2011/2012 inasomwa kesho na waziri wa Fedha wa Tanzania Mr. Mustafa Mkulo. Je kwa wale walioko jikoni kuna haueni yeyote kwa wafanyakazi? Kodi kwa wafanyakazi yaani PAYE ni kubwa mno, 30% ya mshahara ni kodi sawa na Makampuni makubwa. Serikali wangeishusha angalau kufikia 20% ingekua nafuu zaidi kwa mfanyakazi.

Mfano kama Mshahara ni TShs 1,000,000 kodi itakayokatwa ni TShs 300,000 ambapo mfanyakazi anabakiwa na TShs 700,000. Mfanyabiashara wa kiwango hiki ulipa kodi ndogo sana, tena anaruhusiwa kupunguza garama za biashara. Mfanyakazi haruhusiwi kupunguza garama za kumwezesha kufika kazini kama mafuta, nauli, mavazi maalumu ya kazi, chakula cha mchana, n.k Hivi vyote asingekua anaenda kazini asinge ingia garama hizi.

Pia mwenye Budget atuwekee humu tuisome, sio siri
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom