Mallaba
JF-Expert Member
- Jan 30, 2008
- 2,554
- 47
Habari ambazo zimetufikia muda si mrefu uliopita zinapasha kwamba mtanzania wa kwanza kucheza katika ligi ya NBA,Hasheem Thabeet (pichani) aliyekuwa akichezea timu ya Memphis Grizzlies, ameuzwa kwenda timu ya Houston Rockets ya jijini Houston,Texas katika mabadilishano maalumu baina ya timu hizo mbili.
Katika mabadilishano hayo,mchezaji Shane Battier aliyekuwa akichezea timu anayokwenda Hasheem(Houston Rockets) anajiunga na Memphis Grizzlies.
Hasheem ambaye maendeleo yake katika ligi hiyo ya NBA yamekuwa hayaridhishi,anakwenda Houston mji ambao unaaminika kuwa na watanzania wengi zaidi nchini Marekani kuliko mahali pengine.
Katika mabadilishano hayo,mchezaji Shane Battier aliyekuwa akichezea timu anayokwenda Hasheem(Houston Rockets) anajiunga na Memphis Grizzlies.
Hasheem ambaye maendeleo yake katika ligi hiyo ya NBA yamekuwa hayaridhishi,anakwenda Houston mji ambao unaaminika kuwa na watanzania wengi zaidi nchini Marekani kuliko mahali pengine.