mchemsho
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 3,212
- 867
Habari za kuaminika ni Kwamba hospitali ya Taifa muhimbili Imetoa Mpya nyingine kwa kuwakabidhi wafiwa maiti ya Muhindi badala ya Mswahili mwenzao. Maiti hiyo iligundulika kuwa siyo yenyewe baada ya kufikishwa Tanga eneo la Mkanyageni ambapo mazishi yalikuwa yafanyike leo saa 7 mchana, baada ya kugundua hilo imebidi maiti huyo muhindi asafirishwe kurudishwa dar, pia ile familia ya kihindi ambayo maiti wao alichukuliwa inasemekana wako njiani kwenda tanga kumrudisha maiti asiyekuwa wao ili wapewe maiti wao. Chanzo kikubwa cha mkanganyiko huo inasemekana ni majina ambapo maiti wa kihindi anaitwa "luke" na mwingine aitwa "lukeman" sina hakika kama majina yanaandikwa hivyo. Nawasilisha.