Breaking News: Kapt. Komba atafutwa na Polisi

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,461
39,928
Habari zinazoingia taratibu zinasema kuwa yule mpiga debe maarufu wa CCM Kapt. John Komba anatafutwa na Polisi kutokana na kufanya vurugu kwenye mkutano wa Upinzani. Kesi ya jinai imefunguliwa mjini Kibaya huko Kiteto na baadhi ya viongozi wa upinzani. Kapt. Komba alivamia mkutano wa Chadema ambapo alilazimishwa kushushwa jukwaani na FFU. Kwa mujibu wa sheria ya Uchaguzi ya 1985 (as ammended) ni marufuku kwa mtu kuingilia kampeni za uchaguzi wa chama kingine.
 
Mwanakijiji,

Pamoja na hayo yote mimi naiiita danganya toto tu. Hakuna kitu atafanywa huyu bwana zaidi ya kuchukuliwa maelezo then imetoka. Let us wait and see and Bravo for the info
 
umesikia mzee mwanakiji we achana nao hizo za komba kukamatwa ni za kweli ata mm nilisikia pia ila kuna shaka kama kweli wanaweza kumchukulia atua yeyote ya kisheria,si unajua ccm wanavyombeba yule jamaa.tusubiri tuone lkn
 
Habari zinazoingia taratibu zinasema kuwa yule mpiga debe maarufu wa CCM Kapt. John Komba anatafutwa na Polisi kutokana na kufanya vurugu kwenye mkutano wa Upinzani. Kesi ya jinai imefunguliwa mjini Kibaya huko Kiteto na baadhi ya viongozi wa upinzani. Kapt. Komba alivamia mkutano wa Chadema ambapo alilazimishwa kushushwa jukwaani na FFU. Kwa mujibu wa sheria ya Uchaguzi ya 1985 (as ammended) ni marufuku kwa mtu kuingilia kampeni za uchaguzi wa chama kingine.

Jamani Komba na tumbo lake sijui kama ataweza penya mlangoni mwa polisi post ndogo labda apelekwe wilayani. Yule mwimba kwaya naye kazidi na TOT ujinga.
 
Si imesemwa kuwa hakuna aliye juu ya sheria...? tutaona kama Komba anahusika na sehemu hiyo ...
 
hiyo itakufa kabla haijaanza.....na wapinzania sidhani kama wana nafasi na pesa ya kuipigia kelele hata hivyo!
 
Komba itakuwa alikuwa ametumwa hivyo si rahisi kuchukuliwa hatua. Lakini kinachohitajika Inatakiwa wapinzani wafikishe hili suala katika vyombo vya dola halafu vijidhalilishe vyenyewe maana sheria za uchaguzi ziko wazi.

Hii ilikuwa hatari sana halafu ukichukulia yeye ni mtunga sheria(mbunge) tulitegemea anajua sheria za nchi vizuri sana.
 
Habari zinazoingia taratibu zinasema kuwa yule mpiga debe maarufu wa CCM Kapt. John Komba anatafutwa na Polisi kutokana na kufanya vurugu kwenye mkutano wa Upinzani. Kesi ya jinai imefunguliwa mjini Kibaya huko Kiteto na baadhi ya viongozi wa upinzani. Kapt. Komba alivamia mkutano wa Chadema ambapo alilazimishwa kushushwa jukwaani na FFU. Kwa mujibu wa sheria ya Uchaguzi ya 1985 (as ammended) ni marufuku kwa mtu kuingilia kampeni za uchaguzi wa chama kingine.

Mzee Mwanakijiji,

Haya ndio mapambano mimi nayaona makini tumieni sheria zilizopo kuwafundisha umakini kwenye siasa!!!

Lakini nasikitishwa na neno "kutafutwa" una maanisha hata Capt. John Komba ni mtu wa kutafuta kama member wa mtandao wa Al-caeda... mimi nadhani huyu ni wa kupigiwa simu tu... na anaenda anapohitajika.
 
Komba anatakiwa abanwe kisheria na pengine amtaje aliyemtuma kufanya vurugu hizo. Maana yeye alikiri kusema hizo ni mbino za kisiasa hivyo alikuwa anatimiza mipango ya wakubwa wake
 
Ukisha kuwa mwana CCM shina an si tawi basi uko juu ya sheria so Komba ni danganya toto yaani hwy has it taken them so long kuna kwamba alikosea ? Wapinzani ni lini walichukua muda namna hii bia ya kutafutwa na Magazeti yao kama Nipashe , Uhuru, Rai nk kuandika upuuzi ?Wanatuchezea ila kila lenye mwanzo huwa lina mwisho .
 
Nilisema kule kwenye klhnews.com,kuwa ni aibu kubwa na hatari sana kwa mtu ambaye anahusika moja kwa moja na utungaji wa sheria za nchi hii na yeye ndiye anakuwa wa kwanza kuzivunja,hii ni hatari sana. Hizi ndizo gharama tunazoingia watanzania kupeleka bungeni watu wasiokuwa na sifa kama siyo shule,ni hatari sana hii
Najiuliza,hivi angekuwa ni mbunge wa upinzani ndiyo kafanya vituko hivi,ingekuwaje? Nahisi vijana wa IGP mwema,wangembeba juu juu na kujichukulia ujiko,hatushangai,huyu huyu komba alitoa maneno yanayoonyesha mazingira ya kutumia vyombo vy dola kuilinda CCM nanukuu"tumekwisha fanya mipango kuhakikisha helkopita ya CHADEMA haitui hapa,ikitua basi msiichague CCM",unapata picha gani? Huyu ni mtu ambaye ni Ziro nyingine ndani ya bunge
 
Nilisema kule kwenye klhnews.com,kuwa ni aibu kubwa na hatari sana kwa mtu ambaye anahusika moja kwa moja na utungaji wa sheria za nchi hii na yeye ndiye anakuwa wa kwanza kuzivunja,hii ni hatari sana. Hizi ndizo gharama tunazoingia watanzania kupeleka bungeni watu wasiokuwa na sifa kama siyo shule,ni hatari sana hii
Najiuliza,hivi angekuwa ni mbunge wa upinzani ndiyo kafanya vituko hivi,ingekuwaje? Nahisi vijana wa IGP mwema,wangembeba juu juu na kujichukulia ujiko,hatushangai,huyu huyu komba alitoa maneno yanayoonyesha mazingira ya kutumia vyombo vy dola kuilinda CCM nanukuu"tumekwisha fanya mipango kuhakikisha helkopita ya CHADEMA haitui hapa,ikitua basi msiichague CCM",unapata picha gani? Huyu ni mtu ambaye ni Ziro nyingine ndani ya bunge


Wamelewa madaraka na hata wanadiriki kuwa dhihaki na kudharau vyombo vyao vya usalama .Yetu macho na tuna tunza kumbukumbu.Mwaka hu umekuwa na matukio ambayo Seikali na CCM ikija kuwa upande wa pili tutahoji kwa uwazi .
 
Ni mara yangu ya kwanza kujoin JF nimevutwa na maoni ya watu na habari za kila siku bila kusahau mijadala mbalimbali inayojadiliwa.

Nikianza na Komba unajua kuna watu huwa wanaassumption ya kuwa serikali iko mikononi mwao as a result kujifanyia mambo bila kufikilia impact yake mbele ya Jamii.

Hii kibri inatoka na usemi wao ati watanifanya nini?
Manake wanajiona kuwa wao ni above the law,tena ukichanganya na background yake ya JW basi ndo kabisa.

Watz tubadilike?
 
Nilisema kule kwenye klhnews.com,kuwa ni aibu kubwa na hatari sana kwa mtu ambaye anahusika moja kwa moja na utungaji wa sheria za nchi hii na yeye ndiye anakuwa wa kwanza kuzivunja,hii ni hatari sana. Hizi ndizo gharama tunazoingia watanzania kupeleka bungeni watu wasiokuwa na sifa kama siyo shule,ni hatari sana hii
Najiuliza,hivi angekuwa ni mbunge wa upinzani ndiyo kafanya vituko hivi,ingekuwaje? Nahisi vijana wa IGP mwema,wangembeba juu juu na kujichukulia ujiko,hatushangai,huyu huyu komba alitoa maneno yanayoonyesha mazingira ya kutumia vyombo vy dola kuilinda CCM nanukuu"tumekwisha fanya mipango kuhakikisha helkopita ya CHADEMA haitui hapa,ikitua basi msiichague CCM",unapata picha gani? Huyu ni mtu ambaye ni Ziro nyingine ndani ya bunge

Ndugu yangu yaani hapa umenikuna ile mbaya.Mara tu niliposoma hizi habari na kuziona katika picha hapa JF na KLH news nilijiuliza maswali mengi sana. Ila la kwanza ilikuwa hivi angekuwa ni mtu wa upinzani kaingilia mkutano wa CCM angekuwa katika hali gani hivi sasa. Nahisi huyo mkuu wa wilaya alieenda kumbembeleza angemkuta Chumba cha wagonjwa mahututi.
Pili ilishindikana kwangu kuingia akili kuwa Komba ambaye ni mbunge mtunga sheria yeye ndo anakuwa wa kwanza kuvunja.
Hivi kweli kuna wakati hawa viongozi tunaowachagua huwa wanafikiria umuhimu wa "P" na nafasi yao katika jamii??
 
Kwa nini tukate tamaa mapema kwamba watamfanya nini Kapt wa nyimbo za SISIEM?
Atafunguliwa mashitaka ya kufanya vurugu ktk uchaguzi mdogo wa kiteto na ana kesi ya kujibu hivyo ataenda kujitetea mahakamani kwenye uwanja huru.Hapo ndipo Viongozi wa upinzani watafute wanasheria kusimamia,Hata kama kesi itaahairishwa miaka 7.

Sasa hivi duniani kote kote kuna wimbi la mageuzi ya kisiasa.Anagalia siasa za Kenya,PAKISTAN,AMERICA n.k .Kuna wakati utafika hata SISIEM,POLISI NA VYOMBO VYOTE VYA DOLA WATAJIKWAA NA KUANGUKA CHINI CHALI,MIGUU JUU,

Tusiogope kuwa oooh,SISIEM wana mkono mrefu kila sehemu,Penye ukweli uongo hujitenga.Hatuwezi mwacha akitamba mtaani eti hawatamfanya kitu.Lazima asweke ndani,tutajua huko mbele kwa mbele

Kwani walijaribu kuzima hii forum wamefikia wapi?
Fortify yourself with current weapons and let us match forward with heart courageous.
TUSIWAPATIE MAJIBU YA KUMFANYA NINI KAPT WA NYIMBO ZA SISIEM BALI TUFANYE WAJIBU WETU KWA MJIBU WA SHERIA ZILIZOPO.TUTAFIKA TU.
 
Kwa nini tukate tamaa mapema kwamba watamfanya nini Kapt wa nyimbo za SISIEM?
Atafunguliwa mashitaka ya kufanya vurugu ktk uchaguzi mdogo wa kiteto na ana kesi ya kujibu hivyo ataenda kujitetea mahakamani kwenye uwanja huru.Hapo ndipo Viongozi wa upinzani watafute wanasheria kusimamia,Hata kama kesi itaahairishwa miaka 7.



Sina uhakika kma hiyo inawezekana...kama mzee Dito alifumua kichwa cha mtu pale njia panda ya kawe na mtu akaondoka duniani...jamaa akakaa rumande kudanganyia na kesi yake ikabadilishwa sembuse hii ambayo haina kichwa wala miguu...kuna watu kibao wanasota magerezani wengine maskini kwa kesi za kubambikizwa...lakini kwa kuwa Dito ni mwana SISIEM na mwanamtandao basi ndo hivyo kesi yake ilizimwa kiaina...(je mpaka sasa hiyo kesi ilifikia wapi??)

Kwa hiyo swala la Komba (chiriku) litaishia wala sidhani kama kutakuwepo na kesi yoyote....:(
 
Mkuu Kishaju!
Tukikaa tukajikunyata haitatusaidia kitu,tupambane kwa zile silaha tulizonazo hata kama ni za zamani.
IPO SIKU TEMBO ATAKUFA KWA BUA TU TENA LA MTAMA.
Mapinduzi hayaji kwa kunyamaza kimya na kusubiri matokeo yajilete yenyewe bila sababisho.

Akiwekwa kizuizini na kuondolewa kwa hila za SISIEM,Tuna uwezo hata wa kuandama na kueleza ulimwengu dukuduku letu.
SASA KAMA UTAKAA KIMYA TU DUKU DUKU ZAKO UTAZITOLEA WAPI?VOKSI POPULI VOKSI DEI
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom