Breaking News. Babu wa Loliondo asitisha kutoa kikombe hadi tarehe 02.05.2011

Mzee wa Rula

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
8,171
3,346
Babu wa Loliondo mchungaji Mwasapile amesitisha huduma ya kutoa dawa alimaarufu kikombe baada ya kufiwa na mwanae mkoani Manyara - Babati. Vibali vya magari kwenda huko vimesitishwa hadi hapo huduma itakapoanza tena.
Changamoto iliyopo ni msururu wa wagonjwa waliopo huko ambao wanaosubiri huduma ya kikombe toka 26.04 - 02.05.2011. Poleni wote mliopo Loliondo ambao bado hamjapata kikombe na babu ndiyo kafiwa na mwanae, najua maisha yatakuwa magumu sana kwa siku hizo zote.
Mwisho ni pole kwa babu, wapo wajinga wengi watakaohoji kwa nini mwanao amefariki dunia? Wanafikiri wewe unatoa kikombe kuzuia kifo, pole kwa msiba mzito ulikukumba.
Source TBC1
 
Nasikia babu ataondoka jioni ya leo kuelekea Babati kwa helicopter ili akafanye mazishi kisha baadae kurejea kwenye shunguli zake baada ya tarehe 02.05.
 
Back
Top Bottom