Bravo Ismail Aden Rage.......

Sajenti

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
3,651
412
Huenda kauli hii ikawa imeweka historia katika medani ya soka Tanzania. Mwenyekiti wa timu ya Simba Ismail Aden Rage amekanusha taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa timu hiyo ina panga kuwafungia baadhi wachezaji wake tegemeo kwa tuhuma za kuhujumu timu hiyo katika mchezo na watani wao Yanga wa ngao ya hisani.

Rage kwa mara ya kwanza kwa kumbukumbu zangu kwa kiongozi wa timu kama Simba alisema kuwa kufungwa kwao kulikuwa ni kimchezo tu na hakuna hujuma yoyote iliyofanywa na mchezaji au wachezaji wake. Alienda mbali zaidi kwa kuwaomba radhi wachezaji wote waliokumbwa na kashfa hiyo, ndugu na familia zao kutokana na usumbufu wowote walioupata kutokana na habari hizo.

Tumezoa Simba au Yanga moja inapofungwa na mwenzie basi vumbi hutimka klabuni kwa wachezaji kutishwa, kusimamishwa, hata viongozi wenyewe kutimuliwa madarakani. Mfano mzuri kutimuliwa kwa Amiri Maftaha kutoka Yanga kufuatia timu hiyo kufungwa na Simba magoli 4-3.


My take:
Huu ndio uwanamichezo. Ni aibu katika karne hii kiongozi kushindwa kuelezea kushindwa kwa timu yake katika upande wa kiufundi zaidi na badala yake kupeleka tuhuma kwa wachezaji tu. Namshauri mtani pia Nchunga kujifunza kutoka Rage!!
 
Huenda kauli hii ikawa imeweka historia katika medani ya soka Tanzania. Mwenyekiti wa timu ya Simba Ismail Aden Rage amekanusha taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa timu hiyo ina panga kuwafungia baadhi wachezaji wake tegemeo kwa tuhuma za kuhujumu timu hiyo katika mchezo na watani wao Yanga wa ngao ya hisani.

Rage kwa mara ya kwanza kwa kumbukumbu zangu kwa kiongozi wa timu kama Simba alisema kuwa kufungwa kwao kulikuwa ni kimchezo tu na hakuna hujuma yoyote iliyofanywa na mchezaji au wachezaji wake. Alienda mbali zaidi kwa kuwaomba radhi wachezaji wote waliokumbwa na kashfa hiyo, ndugu na familia zao kutokana na usumbufu wowote walioupata kutokana na habari hizo.

Tumezoa Simba au Yanga moja inapofungwa na mwenzie basi vumbi hutimka klabuni kwa wachezaji kutishwa, kusimamishwa, hata viongozi wenyewe kutimuliwa madarakani. Mfano mzuri kutimuliwa kwa Amiri Maftaha kutoka Yanga kufuatia timu hiyo kufungwa na Simba magoli 4-3.


My take:
Huu ndio uwanamichezo. Ni aibu katika karne hii kiongozi kushindwa kuelezea kushindwa kwa timu yake katika upande wa kiufundi zaidi na badala yake kupeleka tuhuma kwa wachezaji tu. Namshauri mtani pia Nchunga kujifunza kutoka Rage!!
Rage ni mwanamichezo halisi anaeishi in the game of football na huko ndiko hata sisi mashabiki tunapaswa kuelekea,watu wanatunga sentesi za uongo na wanataka tuamini hivyo!! Mgosi kukosa goli la wazi hakuanza leo, kwa hiyo kila anapokosa goli kachukua mshiko? Siyo Nchunga tu aige ,hii msg iwafikie mashabiki wote wa soka ambao wanapenda kusikiliza majungu.
 
Rage ni mwanamichezo halisi anaeishi in the game of football na huko ndiko hata sisi mashabiki tunapaswa kuelekea,watu wanatunga sentesi za uongo na wanataka tuamini hivyo!! Mgosi kukosa goli la wazi hakuanza leo, kwa hiyo kila anapokosa goli kachukua mshiko? Siyo Nchunga tu aige ,hii msg iwafikie mashabiki wote wa soka ambao wanapenda kusikiliza majungu.
...Fabulous!!!..Zile karne za watu kuchapana mikwaju kisa eti timu imefungwa na mtaniwa jadi zimepita.
 
well, interesting to hear that Rage Mkomavu kwa issue moja tu wakati managing sports is a heck of responsibilities. Rage ameogoza FAT na kuleta madudu makubwa, na leo kufanya jambo moja zuri aonekane mkomavu? Kwnai tusisubiri? Soon tutaanza kusikia ameiba milioni 50 au 60.
 
mimi alichonifurahisha ni kuwaomba msamaha
wachezaji waliotuhumiwa kuhujumu.....
 
Back
Top Bottom