Bongofleva........utata wa muziki wetu!

jouneGwalu

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
2,687
1,780

Imeshakuwa kawaida, kama kawaida yetu watz, Saiv ukisikiliza redio, ukisoma magazeti na karibia media zote zinapokuwa zina ripoti mambo ya burudani na hasa muziki, utasikia neno muziki wa "bongo fleva"

Bongofleva, inatafsirika kama ni muziki wa kibongo yaani wa kitanzania sababu saiv neno bongo limekuwa na maana ya Tanzania.
Sina tatizo kabisa na neno "bongofleva".

Binafsi linanikumbusha kipindi cha Mike Mhagama wa Radio One enzi zile za mwanzoni sana mwa miaka ya 2000,
Yeah, bongofleva lilikuwa jina la lipindi cha Mike Mhagama wa Radio One, Na hakukuwa na cha kukushtusha sababu karibia redio zote zilikuwa na vipindi vyake vilivyokuwa vinaenda na kasi ya mabadiliko ya kimuziki hasa hapa nyumbani.

Nakumbuka Eastafrika Redio kulikuwa na Dj JD kwenye kipindi chake cha The cruise alikuwa na session ya "bongo explosion"
Clouds fm kulikuwa na Boneventure Kilosa na Dj Steve B, wao kipindi chao kilikuwa kinaitwa "fleva ya bongo"

Redio Uhuru alikuwepo Sebastian Maganga, sikumbuki jina la kipindi na Times Fm simkumbuki mtangazaji wao maarufu wa kipindi hicho ila wao walikiita "bongo hits"

Vipindi hivyo vyote vilianzishwa sababu kwa muda husika muamko wa vijana wa kibongo kurekod nyimbo za "kisasa" ulikuwa mkubwa.

Hivyo nyimbo za wasanii wanaoimba "nyimbo za kisasa" (bila kuzingatia aina ya muzik msanii anaofanya) zikawa nyingi na zikawa na wapenzi wengi sana, hii ndio ilipelekea kuwepo kwa vipindi hivyo maalum.Kwa kutokea hapo naona unaweza ukaona kuwa kumbe "bongo fleva" ilimaanisha kuwa mkusanyiko wa nyimbo za vijana wa kitanzania, "kizazi kipya".

Kwa kulijua hilo waendeshaji wa vipindi hivyo, walivigawa vipindi vyao kwenye aina ya miziki kutokana na mwanamuziki alivyojitambulisha na alivyokidhi aina husika ya muziki, kwenye kipindi cha bongofleva au hivyo kukawa na bongo hip hop, bongo R n' B (hiyo ndio ilikuwa sanasana) na baadae ikaja bongo zouk.

Kwa mtiririko huo, ni inashangaza leo hii kusema Bongofleva ni aina ya mziki unaoimbwa na vijana wa kitz.
Aina Fulani ya muziki unatakiwa uwe na sifa za kufanana kimaadhi, vionjo, mpangilio, mirindimo na vitu vingine vyote vinavyoufafanua muziki husika ndio maana hip hop hata iimbwe kona gani ya dunia bado utajua tu hii ni hip hop, kitu hicho hamna kwenye bongofleva yetu.

Pia kuna mfano mzuri wa "GENGE" hii ni aina ya uimbaji (unahusisha aina ya rap) unaofanywa na jamaa wa Kenya, kwa kiasi fulani kikubwa wamefanikiwa sana kutengeneza aina ya muziki ambayo inasifa zinazoendana, kutokea kwenye mfano huo naona kwa wenzetu imekuwa rahisi sana kuliko wangejikita na "Kenya fleva" na uwepo wa GENGE haujazuia aina zingine za muziki.

Wadau husika hapa kwetu bongo, nadhani wanahitaji kuweka sawa vitu kwenye soko, hiyo itasaidia sana wanamuziki wenyewe, kwani kwa sasa ni kama wanafanya kitu wasichokifahamu hivyo ni vigumu wao kuwa bora sababu hamna standard za kuwapimia hii nayo inachangia sana wasanii (hasa wa hiyo bongofleva) wetu kufanya vibaya kwenye anga za kimataifa.

Bongofleva ni kitu tata bado, ndio maana wanamuziki wote makini na wanaojitambua hawapendi uwaite kwamba wanaimba bongofleva. Ndio maana Kikosi Cha Mizinga walikuwa watata sana katika kujenga mahusiano na wanaoimba hiyo Bongofleva, hata sasa kuna mstari wa wazi kati ya wanaoimba R n' B ( mfano Ramma D, Steve, Ben Pol nk) Hip-hop (mfano One, Stereo, Nickmbishi, Kala Pina, FidQ, Joh Makini nk)

Kwa wadau kuendekeza hii Bongofleva inapelekea hata watu wanaoimba aina nyingine kabisa ya muziki ambayo haijazoeleka hapa kwetu kusahaulika, kitu ambacho sio kizuri kwa jamii yetu, mfano wabongo wengi hatumjui Corolla Kinasha!

Huyo dada ni azina kubwa sana, nadhani ni miongoni mwa wanamziki wachache sana wanawake wa kiafrika wanaoimba Afrikan Jazz.
Tukifungua milango, nje ya Bongofleva kuna aina nyingi sana za muziki ambazo nadhani wabongo wanastahili kujifunza na kuzijua kwa kadiri inavyofahamika kuwa hatuna aina yetu ya muziki kama taifa na tusidanganyane, aina ya muziki wa taifa haitungwi kama tunavyotaka kulazimisha kupitia Bongofleva bali ni matokeo ya historia yenyewe!
 
Very will said jG but hata hivyo kurudisha mweleko kwasasa kwa jinsi huo muziki wa Bongo flava ulivyokua promoted inakua ni vigumu saana.

Music katika taifa letu changa hili ungekua umechukuliwa serious kama an investment kwa kupitia private na government sectors ingekua bora zaidi na ingeingiza pesa nyingi kwa waimbaji na hata serkali pia.

But bahati mbaya hata huo muziki unaokubaliwa ndio umeshamiri una mwelekeo ndio but hauko steady wala secure... Inabidi hili walifanyie kazi haraka.

Hapa am saying my take is waboreshe hio Bongo flava ikae sawa before they they introduce anything else.... Simfahamu huyo Corolla Kinasha but if you are saying anaimba African Jazz then she is good... Kwa yeye sasa kutoka ni issue.

Wangapi wanasikiliza African jazz hapa kwetu jG? wachache mno... Most even dont know what kind of music it is... Me am thinking it is more associated with few elders and few exposed oftenly well-off people... (excuse my saying so but thats what I know)
 
Very will said jG but hata hivyo kurudisha mweleko kwasasa kwa jinsi huo muziki wa Bongo flava ulivyokua promoted inakua ni vigumu saana.

Music katika taifa letu changa hili ungekua umechukuliwa serious kama an investment kwa kupitia private na government sectors ingekua bora zaidi na ingeingiza pesa nyingi kwa waimbaji na hata serkali pia.

But bahati mbaya hata huo muziki unaokubaliwa ndio umeshamiri una mwelekeo ndio but hauko steady wala secure... Inabidi hili walifanyie kazi haraka. Hapa am saying my take is waboreshe hio Bongo flava ikae sawa before they they introduce anything else.... Simfahamu huyo Corolla Kinasha but if you are saying anaimba African Jazz then she is good... Kwa yeye sasa kutoka ni issue. Wangapi wanasikiliza African jazz hapa kwetu jG? wachache mno... Most even dont know what kind of music it is... Me am thinking it is more associated with few elders and few exposed oftenly well-off people... (excuse my saying so but thats what I know)


Hey, Asha D!

Thanks tupo pamoja.

Point yangu ni tu kuwa wadau wauache music ujipambanue tu kama music,
Hamna kitu kama bongofleva eti kama ni aina ya muziki specifically, ndio maana nikaeleza hapo awali tulianzaje hadi kuwa na bongofleva.

Lakini kwa sababu tumejijenga kama ni jamii ya walipuaji (hasa saiv) sababu hapo mwanzo wanamuziki wetu walianzaga vizuri tu!

Kama wakina Dr Remmy walikuwa wanajiita Orchestra (japo walikuwa hawapigi pure orchestra), wakina OTTU Jazz Band na bendi zingine kibao za zamani naona zilikuwa makini sana kimuziki, sasa tatizo la kizazi chetu tunadhani kilakitu cha zamani ni kibaya matokeo yake mambo kibao mazuri ya zamani tumekuwa tunayaacha badala ya kuboresha.

"Wadau" wangeboresha zaidi hizo muziki za hao wazee saiv ingekuwa poa sana, hata wasanii hawa vizazi vipya wasingepata shida kwenye kusimamia bendi zao na aina ya muziki wanayoimba.

Ila muziki ni kitu ambacho ni universal, so nadhani tutajirekebisha baada ya hichi tunachojaribu kuendelea kushindwa, tutarudi kwenye muziki wa dunia.... namaanisha wasanii wanaoukana u-bongofleva wataongezeka.
 
Hey, Asha D!
Thanks tupo pamoja.
Point yangu ni tu kuwa wadau wauache music ujipambanue tu kama music,
Hamna kitu kama bongofleva eti kama ni aina ya muziki specifically, ndio maana nikaeleza hapo awali tulianzaje hadi kuwa na bongofleva.
Lakini kwa sababu tumejijenga kama ni jamii ya walipuaji (hasa saiv) sababu hapo mwanzo wanamuziki wetu walianzaga vizuri tu!
kama wakina Dr Remmy walikuwa wanajiita Orchestra (japo walikuwa hawapigi pure orchestra), wakina OTTU Jazz Band na bendi zingine kibao za zamani naona zilikuwa makini sana kimuziki, sasa tatizo la kizazi chetu tunadhani kilakitu cha zamani ni kibaya matokeo yake mambo kibao mazuri ya zamani tumekuwa tunayaacha badala ya kuboresha.
"Wadau" wangeboresha zaidi hizo muziki za hao wazee saiv ingekuwa poa sana, hata wasanii hawa vizazi vipya wasingepata shida kwenye kusimamia bendi zao na aina ya muziki wanayoimba.
Ila muziki ni kitu ambacho ni universal, so nadhani tutajirekebisha baada ya hichi tunachojaribu kuendelea kushindwa, tutarudi kwenye muziki wa dunia.... namaanisha wasanii wanaoukana u-bongofleva wataongezeka.


Sasa naona nimekupata... Umenifurahisha on the above highlighted;

JG tatizo la wanamuziki wetu hasa chipukizi ni washamba mno or should i say limbukeni? (sorry but ndo ukweli nimeshindwa neno laini zaidi ya hilo-alternative lenyewe ni kali).

Especially hawa wanamuziki wapya ambao wanaone kupendeza with pamba and beautiful cheap girls is everything.... Wanatia huruma hawaheshimu wanamuziki wazamani acha tu hawa wa early 2000, wanajiona ni bora kuliko wao wanasahau hao walotangulia hata kama majina sio maarufu anymore ndio waliwawekea foundation ya hapo walipo.

How can you possibly successed kama hujui kwenu wapi ili uji define ??? Yes miziki imetoka mingi mizuri but inapita kila siku na na-apply quote ya Kiba ya kutema big G....

Personally naona wangekuwepo wale wajuzi kweli kweli wa muziku kwa ajili ya quality assurance wakizingatia pia kutafuta nyimbo ambazo zaweza define TZ (kama vile ukisikis kwaito u know its S.

African au imeigwa...) Kwa mtazamo wangu for insance nyimbo kama Goma la Mansese ina more flava na it can last longer kuliko nyimbo zoote ambazo wamegundua kuimba in pairs and kuhusu mapenzi - ni nzuri maskioni but zinapita tu... where is Diamond's mbagala??
 
Yani nimeandika kwa kirefu alafu hichi kimeo changu kikaleta mbwembwe....

Nwy my dear mwanafunzi and partner naona uko kwenye harakati za kuichambua bongo fleva!!!Yani MBAGARAAAA kama zilivyo nyimbo nyingi za wasanii wetu zinachuja haraka sana kama nguo ya mchina!!Na sababu haswa ni kwamba wanachoimba hakitofautiani kimaudhui...muonekano wala kimtazamo!Kwahiyo ikitoka mpya tu unahamia kule unaachana na iliyopita!!!

JG naungana na wewe unaposema kwamba bongo flava sio aina ya mziki wetu bila ni mchanganyiko wa mziki wenye maudhui tofauti tofauti unaoimbwa na wabongo.Sio sawa na Kenya walivyo na GENGE au Ghana walivyo na HIPLIFE...ngoja nikuwekee ngoma moja ya Reggie Rockstone usikie YouTube - Broadcast Yourself.
 
Jamaa wakipunguza njaa tu mziki utakua poa,yaani sikuhizi wasanii wanaigana sana na wengi hawana identity yao. wabana pua wakiwa juu kila mtu anataka kuimba yaani watu wanaiga hadi YOUNG MONEY STYLE kuimba kiduku.Taabu kweli yaani wasipojitambua wenyewe nani atawatambua.............
 
jouneGwalu tatizo la soko huru ndio hilo-mwenye nguvu mpishe. Kulikuwa na enzi za muziki wa dansi nchini. Wakawepo wee wakati huo pakiwepo na ombwe la bururani ya kukata kiu. Na walipotokea vijana ndio haya unayoona yakatokea.

Kuna kitu tunaita niche. Hii unayoona katika bongofleva ni niche. Na kilichosababisha hili ni wimbi kubwa la radio na tv stations zilizoibuka kama uyoga miaka ya karibuni na kuajiri %90 ya vijana ambao walipata msasa kidogo tu kuhusu mass communication then wakawa watangazaji kwenye hivi vyombo. Wao wanajitazama wao kama vijana. Sasa wazee wakifuata mkumbo na mwishowe kuanza kulalama ni juu yao. Narudia tena na huku. Ni nani aliwanyima hizi niche zingine (rege, dansi,) kujenga kasi ya ushindani? Mbona taarabu na gospel zimeshamiri kati ya hiyo bongofleva?

Umemtaja Kinasha. Namuheshimu huyu mama ila nae ana matatizo yake. Kwa nini akubali kuishia kuimba kwenye kumbi huko mahotelini? Huyu na mzee kitime na mzee Zoro na wakongwe wengine. Wanaijua tasnia vizuri sana. Kwa nini hawataki kutoa kazi ambazo zitapendwa na kuchezwa kwenye media? Tunabaki kuwapa sifa watu ambao hatujui kazi zao! Si bora unamsikia Diamond kila leo? Kinasha ana mchango gani kwenye muziki wa Tanzania? Ni wimbo wake mmoja tu naujua, na ana sauti nzito na nzuri sana! Kitime sijui kama nimewahi kumsikia akiimba. Hata kwenye bendi maarufu sijawahi kumsikia huko, na sijui ugwiji wake unatoka wapi.

Kama vijana wamelishika soko ina maana kazi zao zinapendwa. Hapa ni kuwasaidia miongozo ya namna ya kufanya kazi zao kiumakini zaidi. Mziki wotw wa vijana kuitwa bongo fleva sina tatizo nalo. Bongofleva ni mwamvuli na chini yake kuna hizo categories. Kenya kuna kitu wanaita CHIPUKU. Jaribu kuifuatilia, sidhani kama ina tofauti na bongofleva. Wazee nao watoke huko mahotelini walikozubaa waje wapambane kwenye soko.
 
Last edited by a moderator:
Hiyo CHIPUKU ya Kenya ndio ipi Kaka??

Nakumbuka mara ya mwisho kulikuwa na "KAPUKA" ambayo kiukweli ni aina ya music inayodharaurika sana pale Kenya hata waimbaji wake wengi wamepotea kwenye game na wengi wameenda kwenye GENGE mfano Col Mustapha.
Mkuu Raia Fulani hivi unaifuatilia game ya Kenya au??

Afu unanifurahisha unawaponda hao "wakongwe" afu hapo hapo unasema huzijui kazi zao!!

Unasema watu wafanye music kwa maslahi lakini hapo hapo unaponda wanavyoimba kwenye mahotel sasa sijui unazungumzia maslahi gani??

Nimejaribu kukuonyesha mfano wa soko linavyoendeshwa kwa giriba za hata "mastaa" wanavyotumia hela kubaki juu sasa sijui ni namna gani hao wa kwenye mahotel watoke kwenye mahotel ambako wanaitwa na kubembelezwa watoke huko waje kulipa malaki yapesa eti ili tu wasikike hewani!!!!
Sipati mantiki yako kwenye hilo kwakweli....
Mkuu wangu, music sio kurekodi nyimbo mpya kila siku....
Nilimtaja Kinasha sio kwamba vipi ila ni taswira halisi ya wanamuziki inavyotakiwa kuwa....
Hivi kwa mfano Angelique Kidjo ana nyimbo ngapi mkuu??
Bahati mbaya sana mimi sio mwalimu mzuri sana na kwa namna ya mtazamo ninayoiona toka kwako, ni wazi kuwa siwezi kukufikisha kwenye ngazi ya uelewa ninayotamani uione!!

Pia nilisema sina tatizo na neno Bongofleva ila naomba nisome kwenye mistari maana nimejaribu sana kuweka kitu clear kuwa ili kwenda sawa na kasi ya dunia na kutengeneza nafasi ya wao kuingia kwenye soko la kimataifa kiurahisi, au nikasema kama hii Bongofleva tumeamua iwe "genre" basi tuiratibu iwe na standard zetu ambapo mtu yeyote akiimba itoe utambulisho wa moja kwa moja mfano leo wanaijeria na aina yao ya uimbaji hadi raha wakina Jmartins wamefanya vitu vizuri sana na dunia imeheshimu sana.....

Na uwepo wa bongofleva usilazimishe tu watu wote waimbe bongofleva huu ni uzuzu!

Kuhusu taarabu nadhani umesahau tu kuwa ni music yenye miziz yake ya kimwambao toka enzi hizo za Kina Mzee Matona na kizuri kwenye music ya taarab ni kuwa inaendeshwa na wadau wa taarab wenyewe, kwa mfano walioasisi mipasho ni wakina Bi Khadija Kopa na Marehemu Bi Nasma Kidogo hiki kisa chake kinaweza kuwa sawa na Reggae na Ragga Muffin au Hardcore Hiphop na Commercial Hiphop... Sasa sijui ulikuwa unataka kusema nini kwenye hili Mkuu!

Nadhani case ya Gospel niiache kidogo sababu hiyo ni industry inayojitegemea sana tutaipigia stori siku nyingine.

Tunayafanyaje yote hayo??
Hilo ni swali gumu sana kwasasa kwa namna ya mambo yalivyo sababu jinsi soko lilivyo kwamba hata BASATA wapepoteza function zao na wala hatujui wanasimamia nini na katika namna kuna watu wameshikilia mpini kwa kujitambulisha kama wao ndio wadau halisi huku wakihujumu ngazi zote za uhai wa sanaa na watu hawa wameaminika sana hata mpaka kwenye ngazi ya Taifa (wanaandaa bezdei ya Rais lol)...

Kwakweli ni ngumu sana japo tu ukweli uendelee kuhuburiwa tu na watu wajue mambo yalivyo!
 
Last edited by a moderator:
Dah! JG Naona imeiibua upya thread with the help of Raia mwema... lol ... Its really good.

Jamani Angie!!

Lol mi RF tuna kazi kweli, kuna kamjadala kakaanzisha hapo juu basi naona akaja kuchimba hadi huku baada ya kumpa link.

I think i miss u so much AshaDii
 
Last edited by a moderator:
Jamani Angie!!

Lol mi RF tuna kazi kweli, kuna kamjadala kakaanzisha hapo juu basi naona akaja kuchimba hadi huku baada ya kumpa link.

I think i miss u so much AshaDii


Nimeona huo mjadala, nikaona content ni intensive it will need my attention. Nina mpango wa kutembelea na kuchangia soon. Najua I will enjoy nikisoma hasa ukizingatia sometimes Raia ni mtata. Angle zake hua ziko intereresting... Have missed u too pal. Take care, mie napumzika sasa...lol. Uzee umeingia... hahaha. nachoka haraka.
 
Ndugu JG kifupi nimekusoma. Halafu ni CHIPUKA. Hii kitu nilisikia wanazungumzia kwenye kipindi cha strictly Kenyan ila nilikuta wanamalizia.

Muziki wa Kenya mbali na Genge na hiyo chipuka hakuna muziki! Miziki mingi ya huko ni ya kilugha zaidi pia. Ukiacha mwanamuziki kama Wainaina na The mushroom (kama bado wapo), pamoja na kizazi kipya cha huko, hakuna kitu pale. Uganda the same ila sijajua muziki wao unaitwaje. Nao kwa kiasi kikubwa na kizazi kipya.

Kuhusu hawa malejendari wetu ukweli unabaki palepale. Suala la kukimbilia mahotelini ni suala la kukwepa wajibu. Kama Kitime alianzia kwenye bendi ni nini kilimuondoa kwenye mfumo huo? Hivi leo Kitime utamuweka katika kategori gani katika suala zima la tuzo za muziki. Labda utunzi kama anawatungia wengine. Ni nini kinachowafanya wahofie hata kutoa zingzong wasikike? Hivi leo hii wakitoa nyimbo zao kadhaa hawatapata watu wa rika lao wa kununua?

Hivi leo kuna ombwe la burudani kama ulikuwa hujui. Kuna kizazi kinakosa ladha ambayo walikuwa wakiipata zamani na ambayo kwa sasa imevamiwa na bongofleva pamoja na bolingo. Ilikuwa ni jukumu la hawa wakongwe kuhakikisha kuwa pamoja na kupatia riziki zao mahotelini, wawape wapenzi wa burudani kile walicho nacho. Mwisho wa siku msanii anafariki na watu wanamuenzi. Wanamuenzii kwa lipi? Naomba nirudie kusema tena kuwa sizijui kazi zao! Na wangekuwa nazo zingeonekana! Ya nini kuishi na historia? Naomba nitajie kazi tatu za Kitime na Kinasha nitafurahi sana. Ila nataka kazi za miaka japo 10 iliyopita.

Bado naamini kabisa kuwa hawa wazee wana nafasi ya kutosha ya wao kukubalika tena. Natamani kusikia kazi zao maana inafika wakati naona soni kusikiliza bongofleva maana ni watoto sana wanaimba siku hizi, na mengi ya maudhui yao yanaendana na rika zao na ndio maana nikasema kuna OMBWE la burudani katika rika kadhaa

na kama hawa jamaa wanaomuandalia rais besdei wameweza kuteka soko, wengine washindwe kwa lipi? Naamini kabisa kuwa katika nchi hii kuna watu wamekaa wakitenga vinywa vyao kusubiri kuwekewa vinywani. Kwa mtaji huu wacha wahindi wanyonye, wacha mawingu wanyonye, maana wanaonyonywa wameridhika.
 
Ok nimekumbuka kuwa ni CHIPUKA!!

Hilo KAPUKA lilikuwa linatumiwa na baadhi ya watu wa hiphop kuitusi hiyo CHIPUKA...

Mkuu kama hujaipenda music ya Kenya ni useme tu huipendi na wala huifuatilii kuliko kusema eti "hamna kitu pale"....

Kenya kaka wanfanya music na tena wana audince yenye msisimuko balaa...

Umetaja kipindi cha "strictly Kenyan" ningekushauri uwe unakiangalia (ila kama we ni mpenzi wa music) utaona wanachofanya wakenya kwenye music....
Unasema Kenya hamna kitu ila unasahau kuwa Channel O na MTv wanafanya matamasha yao pale na wanamuziki wa Kenya wanafanya mambo balaa!
Wametoka nje ya box na wanaimba music ya aina zote karibia na bado vijana wa kisasa wanamusic yao hiyo sijui CHIPUKA na hiyo haijalazimisha eti kila mkenya lazima aimbe hivyo....
Sikumoja niliona show ya Jazz imeandaliwa na watu walikuwepo wengi tu kwenye ukumbi ule na hao jamaa ilikuwa ndio kama mwaka huo wanaanza ku-introduce Jazz Kenya nadhani ilikuwa mwaka jana..!!

Ahsante kwa kunitajia Erick Wainaina, kipenzi changu sana sasa unawezaje kusema Kenya hamna kitu...!!

Uganda wanafanya aina yao ya Ragga na wanamuziki wa uganda wana mafanikio makubwa sana kipesa, sasa kama unataka tujadili music na hata hufuatilii music yenyewe kaka hapa tunajadili au we umeweka ligi ya kubishana na mimi tu nikupe ushindi??

Sawa kama unataka kubaki na msimamo wako (pia sio lengo langu kukubadilisha msimamo) ni sawa tu pia sababu hamna mabadiliko ya karibuni kwenye music yetu hivyo kukaa na misimamo kama yangu inaweza kuwa ngumu kidogo.
Ila mi naeleza kile ninachodhani ni UKWELI kuhusu music!!

Suala la hao watu wazima kutofanya music kama unavyotamani wewe tu nimelieza kule,
Unataka nikupe kazi zao za miaka 10 ndugu yangu wakati Kinasha alikuwepo juzi Feb tu kwenye Tamasha la Sauti za Busara pale Zanzibar, pia tulikuwa naye mwaka jana kwenye KIGODA CHA MWALIMU pale UDSM na alifanya kazi zake kibao na hadhira ile inajua kilichofanyika pale...
Mzee Kitine si bado yupo Kilimanjaro Band?? Au ulikuwa unataka afanyaje sasa?? The Kilimanjaro Band si inafanya shughuli zake bado, wanaimba na wanazunguka sehemu mbalimbali duniani... pole mkuu kama hauna taarifa....

Unataka kazi za miaka 10 wakati huo huo unasema wanaimba kwenye mahotel, haya huko kwenye mahotel wameimba miaka 10 iliyopita?? Sasa wanaimba nini?? Mbona wanalipwa pesa na hayo mahotel!!

Kweli hao watu wanakubalika sana tu ndio maana na wao hawajaacha music na ndio maana bado wanafanya na wanaitwa kwenye sehemu za hadhira zenye upenzi wa music yao...

Maana ya kukubalika sio eti kwa mwanamuziki kutuoa nyimbo mpya kila siku kutangazwa maredioni na kupigwa nyimbo zao kila mda, tusikariri hivyo Mtu mzima!

Ni kweli kuna Ombwe la burudani ila sio kosa la hao wakongwe ila ni suala ambalo tatizo lake limeanzia mbali sana na mpaka sasa limefika mbali sababu kuna wajasiriamali wana hati miliki ya burudani na wana-dictate kwa kutumia mbinu za ki-marketing kwamba jamii nzima ipende nyimbo za aina fulani, ukiimba tofauti unaambiwa "hiyo haiuzi" (utafikiri kuna zinazouza hata hizo wanazozipigia promo)...

Taratibu za kurithisha watu zipo sana ndio maana Carola na wakina sister Jack (wa udsm) na watu wengine wa music wana kitu kinaitwa "Music Crossroads" na wanafanya vitu vyao na wanawafundisha madogo pale safi sana na wanfanya matamasha ya kimataifa hamna fitna wala mizengwe tatizo ni kuwa hapa bongo kama unafanya harakati za burudani huku hao watu wako hujawapa fungu lao basi hamna mmbongo atakayekijua, hatuwezi kwenda namna hiyo!

Na wabongo wote wametega masikio huko clouds.... wakati tangazo linatangazwa Times Fm... utasema oohh jamaa washamba kwanini wasitangaze na redio inayosikilizwa na wengi hahahahahahahah full uzuzu wa watu wetu!

Njenje wanawaandaa wakina Aboubakari Mzuri na vijana wengine kibao wapo pale wanafundishwa music ya ukweli....
Ila sababu hawatangazwi na redio yenu ya "wajanja" mtasema oh dogo katoka bss kafulia wala hasikiki redioni hahahahahahaha

Unazungumzia kategori ya music, mi sitakutajia kategori ila tu nitakwambia anafanya music ambayo ipo real na live... full set ikisindikizwa na sauti ya anayejua sauti yake na mirindimo ya mpangilio wa instruments sawia.. Waitikiaji safi wanaojua jukumu lao, jukwaa lipo maridhawa sanaa iliyokamilika na mbwembwe za muimbaji kushirikisha hadhira yake...
Katika uwasilishaji huu sitajali aina ya music wala kategori inayoimbwa hapo ila tu ntaingia kati na mimi kuwa kichaa sababu tunaposema music hiyo ndio music yenyewe kaka!....

Mara nyingi huwa naogopa kuiita bongofleva eti ni music hahahahahahaha

Watu wa bongo hawana hatia wao ni walaji wanokula kilichopo mezani hata kama wamewekewa sumu, sikatai hayo mawingu kuwanyonya watu ndio maana nikasema kuwa tumepotea sana kiasi kwa mtu mwingine kuona tupo njia sahihi, ila maswali yanayojitokeza kwenye uendeshaji huu wa muziki ndio baadhi wanaanza kujua kuwa kweli tumepotea...

Mimi naweka kile ninachoamini kuwa ni ukweli ndio maana najiita mjumbe tu... Am just a Messanger bro!

Kuna tofauti kati ya "mambo yalivyo sasa" na "namna mambo yanavyotikiwa kuwa"....

 
Najua hapa kwenye tasnia ya muziki nimechokoza mzinga wa nyuki maana kila engo uko. Yawezekana hawa unaowakingia kifua; Kitime, karola, Njenje, Kilimanjaro, etc wameshindwa ushindani na kuamua kujifanya kitu kinaitwa differentiation. Hawa watu hawako katika maisha ya kawaida ya mtanzania bali wako kwa ajili ya kumburudisha mtalii na mtanzania mwenye pesa ya kutumia katika mazingira ya pesa. Katika mazingira kama haya ni vigumu njenje ama Kilimanjaro kusmama na twanga katika ushindani, na ndio maana ikatamalaki hiyo bongofleva na muziki wa dansi/bolingo.

Kama hao wasanii wameamua kujitenga na jumuia kubwa ya watanzania, hakuna sababu ya kusema kuwa tunathamini michango yao katika sanaa nchini. mazingira wanayofanyia kazi zao ni adimu kwa mtanzania wa kawaida kuona ana umuhimu wa kufika. sauti za Busara wanaenda wangapi kama si wazanzibari na wasanii na wabara wachache?

Sasa imetosha tuzungumzie namna gani hili ombwe litaondoka na hawa ma lejendi washuke toka huko juu waje katika maisha ya kawaida ya watanzania ili kazi zao ziweze kuthaminiwa na umma na wala si kikundi cha watu wachache waliokaa pale UDSM ama White sand ama huko zanzibar.

Kadhalika ningependa unipatie ratiba za kisanaa za hawa wakongwe kama Kinasha ili nijue undani wa kazi zao
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom