Bongo Star Search 2009: Burudani kweli!?

SIPENDI

Member
Apr 30, 2008
45
2
Majaji (Judges) wa Bongo Star Search wanadhalilisha Washiriki

Wanajamii,

Leo kwa mara ya kwanza nashuka katika jamvi hili nikiwa na maswali ya kuuliza. Napenda kuuliza kwa kuwa sina uhakika kama ninafahamu maana ya neno la kingereza “celebrity” …yaa inaweza ikawa ni umaarufu au kusema ni mtu maarufu. Kama ndiyo hapa ndani ya nchi yetu nzuri Tanzania watakuwepo “celebrity” wengi sana. Lakini pamoja na kuwa nao kuna mambo yanafanywa na hao watu ninaowaita maarufu ambayo hayana maana kabisa katika jamii yetu. Hivi Juzi Jumapili ya tarehe 10 Mei, 2009 nilibahatika kutazama kipindi maarufu kwenye Luninga kinachokwenda kwa jina la “Bongo Star Search” kinachorushwa na Stesheni ya ITV. Kuna hawa watu maarufu…ni maarufu kweli na hata kipindi chenyewe ni maarufu lakini kwa sasa naona kama kimekwishapoteza umaarufu.

Maswali yangu ni haya: Hivi nini maana ya kipindi Hiki? Kwa ajili ya nani? Je washiriki wale wanavyotendewa na hao majaji (Judges) au kwa lugha ya kawaida waamuzi ni sahihi? Iweje kutumia lugha chafu kwa washiriki? Kuna mifano kama miwili iliyojitokeza juzi…..moja kwa mwanadada na wa pili kwa mwanakaka….. walilalilishwa kwa kweli.

Mwanadada: Aliimba kwa kadiri ya uwezo wake. Wakati wa majaji kutoa comments zao….mmoja alidiriki kumwambia huyu dada hawezi kuimba anachodhani anaweza “aende akazae tu” Hii maana yake nini? Ndio kujaji kweli?

Halikadhalika;
Mwanakaka: kama alivyofanyiwa mwanadada naye kaambiwa akatafute “ma – sugar mummy” kwa vile alikuwa “smart” Mtanashati…..inatisha…

Sikuweza kujua kama kweli huyu Jamaa ana akili nzuri. Naomba nimtaje tu kwa sababu nia ni kumrekebisha na si kumsema vibaya. Ni kati ya wale majaji watatu anajiita P Funk. Mimi Binafsi na labda baadhi ya waliobahatika kutazama kipindi kile hafurahishi kwa comments zake. Anajaribu kuwe critique kama alivyokuwa Salama Jabir lakini si ki-hivyo. Ajaribu kuwa yeye asifanye vitu kwa kuiga…lazima ataharibu.

Naomba tujadili hili kwa busara kwa ajili ya kuboresha kipindi vinginevyo sijaona maana yake kama hali itaendelea kama hivi. Umaarufu usiwe kero….
 
Mkuu umenena hawa jamaa mi naona ni mradi tu wao yaani unakuta mtu anajitahidi kuimba lakini majibu anayo pata kwakeli si ya kibinadamu kabisa ...eti hebu timua unatupotezea muda ...nenda kauze vitumbua.
Nashangaa wao wenyewe kuimba ni utata mtupu labda huyo P-funk anaweza akabahatisha je na walimu wangekuwa wanajibu hivyo wanafunzi tungekuwa tunajifunza.
Kama mtu kashindwa mpe moyo ajitahidi kwa next time majibu ya kumtia mtu moyo na si kumkatisha tamaa.
 
Yaani sijui nisemeje jumapili hii nadhani udhalilishaji ulikuwa wa kiwango cha juu sana,nakumbuka mkaka mmoja aliulizwa anafanya kazi gani akasema yeye anapiga viatu rangi,huyo P Funk akamwambia wala hafai kuwa msanii akaendelee na kazi yake ya kupiga viatu rangi,sipati picha kabisa ya hawa majaji,hivi wamelewa umaarufu? au kudhalilisha watu ni sehemu ya kazi yao? maana nachoona kinachoendelea pale ni dharau za hali ya juu sana,pia nakumbuka kuna maneno ambayo waliyaziba ili tusijue huyo judge kaongea nini,binafsi nilikasirika sana,Hivi hakuna mtu ambae anaweza kuwaeleza kuwa hawa jamaa tabia wanayofanya sio nzuri? Hivi wao wangeambiwa hayo maneno wanayowaambia hao wasanii wangejisikiaje?
 
Ama hakika washiriki waliojibiwa majibu hayo ya kudhalilisha ya huyo anayejiita P.Funk... Kama hawatapata counselling wanaweza wakapata hali ya mfadhaiko wa akili...Haswa yule dada aliyeambiwa nina-nukuu "HUJUI KUIMBA...KAZAE HUKOO...TOOOKA ...MLANGO ULEEEE..." Mimi binafsi nilisikitishwa sana na kauli ile na zaidi pale alipomuambia yule aliyekuwa akiitwa Joachim...(Master J anaiitwa Joachim) Nina nukuu "Joachim wote ni vichaa..." Bora hata Salama Jabir huyu anayejiita P.Funk... Kazidi... Rita Paulsen... Kumbuka Coca-cola Pop star ilivyokuwa bomba... Ni hayo tu
 
msameheni jamani labda ndo yale majani ya bob,in short kipindi kizima hakina mantiki, wakati ulimwengu ukibuni vitu vipya vya kuigwa sisi bado tunaandaa matamasha ya kuiga nyimbo za wenzetu!?
 
Kweli kabisha, iko kijamaa kinaitwa P-FUNK ni kichefuchefu cha ajabu. Sijui hawa jamaa wamemtoa wapi. Inaonekana ni Bangi bangi, busara 0 everything 0.

Nashauri wamre-place huyu jamaa otherwise wataharibu.
 
Jamani.. hivi mapaka sasa hamjajua hii ni Reality show.. its meant for entrtainment.. producer wa show yeye ndo nataka vitu kama hivyo na anavi encourage kwasababu vina ongeza viewers.. ikiongeza viewers wao wana benefit though matangazo na njia nyengine.. ila the whole concept is to get u fired up vitu kama hivyo na hype..
Au hamkusika kua jaji alimjibu rudi mtoto mdogo kwenye show moja kama aina hiyo hiyo huko india. mtoto akajaribu kujiua.. akashindwa kwasababu ya remarks za jaji.. na jaji hakushtakiwa wala nini??
au aukusikia the famous show American idol ambapo Paula alimmaindi porducer kwa mui entertain a fan ambaye alikuwa stalker.. akaishia kujiua nje ya nyumba ya Abdula???
Ts for entertainment
 
Mimi pia niliangalia kipindi hicho jumapili. Kusema za ukweli hata mimi nilisikitishwa sana na comment za majaji hasa hasa huyo P funk. Na kwa bahati mbaya sana safari hii hata Madame Rita ambaye huwa anajitahidi kuwa polite kidogo safari hii amebadilika kabisa, anawaponda vijana moja kwa moja. Ningependa kuwauliza hao waandaaji, hivi wanafikiri bila ya hao vijana kujitokeza shoo yao ingeweza kuwa shoo kweli?
 
Nimekiona kipindi hiki na nasikitika kuwa majaji wana dharau kubwa.Sijui dharau inaletwa na umaarufu au pesa walizonazo lakini ni dhahiri kuwa wana aina ya dharau ambayo kwa utamaduni wetu haipaswi kuwepo.Hata hao majaji wa American Idol hawana dharau ya aina ya hawa ndugu zetu.Aibu tupu!
 
p funk zamani ilisemekana unatumia kilevi aina ya bangi sikuamini lakini kwa sasa naanza kuamini kwamba unatumia kilevi hicho..... kwanini unafanya hivyo lakini? sijakupenda hata kidogo mkubwa jirekebishe plz!!
 
p funk zamani ilisemekana unatumia kilevi aina ya bangi sikuamini lakini kwa sasa naanza kuamini kwamba unatumia kilevi hicho..... kwanini unafanya hivyo lakini? sijakupenda hata kidogo mkubwa jirekebishe plz!!
nikusahihishe bangi sio kilevi ni kiburudisho.......
....bangi inafanya uwe na akili ya ziada na mawazo mbadala sio kama ya p funky....tafadhalini sana msihukumu bangi
 
Jamani.. hivi mapaka sasa hamjajua hii ni Reality show.. its meant for entrtainment.. producer wa show yeye ndo nataka vitu kama hivyo na anavi encourage kwasababu vina ongeza viewers.. ikiongeza viewers wao wana benefit though matangazo na njia nyengine.. ila the whole concept is to get u fired up vitu kama hivyo na hype..
Au hamkusika kua jaji alimjibu rudi mtoto mdogo kwenye show moja kama aina hiyo hiyo huko india. mtoto akajaribu kujiua.. akashindwa kwasababu ya remarks za jaji.. na jaji hakushtakiwa wala nini??
au aukusikia the famous show American idol ambapo Paula alimmaindi porducer kwa mui entertain a fan ambaye alikuwa stalker.. akaishia kujiua nje ya nyumba ya Abdula???
Ts for entertainment
jamani,mimi sioni what the fuss is all about wakati mavumbini kashawaeleza hii ni reality show ambayo inaitaji viewers na in the process inagenerate income through advertisements. Bila controversial remarks hizi shows could never live up to their billing.
 
Huyu P.FUNK si ndo alitereza wakati majaji wako katika mstari kusubiri kupima NGOMA?? eti alikuwa anasikiliza simu. kwa kitendo kile tu ilibidi afukuzwe huo ujaji.Hamna kitu pale ni Bangi tu kichwani.Anatafuta umaarufu kwa Nguvu.
 
jamani,mimi sioni what the fuss is all about wakati mavumbini kashawaeleza hii ni reality show ambayo inaitaji viewers na in the process inagenerate income through advertisements. Bila controversial remarks hizi shows could never live up to their billing.

Nakubaliana na wewe on controversial remarks kama ulivyoiita lakini siyo za anazoonyesha P-FUNK. Mtu kama Salama namkubali kwa hilo la controversial lakini P-FUNK 0000000 zero------
 
nikusahihishe bangi sio kilevi ni kiburudisho.......
....bangi inafanya uwe na akili ya ziada na mawazo mbadala sio kama ya p funky....tafadhalini sana msihukumu bangi


Mhh... hii imekaaje tena! anyways that is Yo Yo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom