Einstein
Senior Member
- Dec 5, 2009
- 121
- 26
Habari zenu?
Napenda kutambulisha kwenu uanzishwaji wa jumuiya inayoitwa BONGO SCIENCE, au kwa kifupi BS..
Katika kipindi hiki ambapo nchi nyingi duniani zimekuwa zikifanikiwa kwa kutumia ipasavyo technolojia na sayansi, kuna haja ya sisi kukaa chini na kutafakari na kuchukua hatua juu ya nini tunatakiwa kufanya ili kuinua maendeleo ya technolojia katika nchi yetu Tanzania..
Kwa kipindi hiki cha karibuni, tumeshuhudia wanafunzi wakifeli sana, hasa kwenye masomo kama hesabu na mengine ya sayansi..
Kwanza tujiulize, tatizo ni nini?? Then tutafute dawa ya huu ugonjwa.
Katika dunia ya sasa, maendeleo ya ki-technolojia yanaambatana na kuwepo na wanataaluma mahiri katika nyanja mbali mbali za technolojia.. Pia tunatambua ya kuwa maendeleo ya nchi yanaambatana na uwepo wa technolojia..
Kwa kuanzia, mwanataaluma ameamua kuja na BONGO SCIENCE itakayowaunganisha wanataaluma wachanga na wakubwa katika kubadilishana maoni na kuchukua hatua juu ya uendelezwaji wa technolojia katika nchi yetu Tanzania..
Sasa huu ni mwanzo, ila lengo hasa ni kuweza kuwafikia wanafunzi wa Secondary na vyuoni ili kutafuta ufumbuzi wa jinsi ya kuinua wanasayansi wa Tanzania..
Je, nini kifanyike hasa? Tupeane maoni, na tuchukue hatua..
Naomba maoni yenu, Nawasilisha..
website: http://jgagah.blogspot.com
Napenda kutambulisha kwenu uanzishwaji wa jumuiya inayoitwa BONGO SCIENCE, au kwa kifupi BS..
Katika kipindi hiki ambapo nchi nyingi duniani zimekuwa zikifanikiwa kwa kutumia ipasavyo technolojia na sayansi, kuna haja ya sisi kukaa chini na kutafakari na kuchukua hatua juu ya nini tunatakiwa kufanya ili kuinua maendeleo ya technolojia katika nchi yetu Tanzania..
Kwa kipindi hiki cha karibuni, tumeshuhudia wanafunzi wakifeli sana, hasa kwenye masomo kama hesabu na mengine ya sayansi..
Kwanza tujiulize, tatizo ni nini?? Then tutafute dawa ya huu ugonjwa.
Katika dunia ya sasa, maendeleo ya ki-technolojia yanaambatana na kuwepo na wanataaluma mahiri katika nyanja mbali mbali za technolojia.. Pia tunatambua ya kuwa maendeleo ya nchi yanaambatana na uwepo wa technolojia..
Kwa kuanzia, mwanataaluma ameamua kuja na BONGO SCIENCE itakayowaunganisha wanataaluma wachanga na wakubwa katika kubadilishana maoni na kuchukua hatua juu ya uendelezwaji wa technolojia katika nchi yetu Tanzania..
Sasa huu ni mwanzo, ila lengo hasa ni kuweza kuwafikia wanafunzi wa Secondary na vyuoni ili kutafuta ufumbuzi wa jinsi ya kuinua wanasayansi wa Tanzania..
Je, nini kifanyike hasa? Tupeane maoni, na tuchukue hatua..
Naomba maoni yenu, Nawasilisha..
website: http://jgagah.blogspot.com