Bongo Movie ni Kitivyo cha Utovu wa Nidhamu?

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
Ukifatilia kwa karibu, wasanii wa bongo movie, wanakuwa wa kwanza kuonyesha mfano mbaya kwenye jamii, hasa pale wanapokuwa kwenye kumbi za starehe au wanapokuwa wanaigiza, kwanza wameutupa kabisa mchenzo wenye maadili wa wazee wao wakaiga ule wa majuu, hasa uvaaji hovyo, kuigiza uchawi uliopitiliza, jambo ambalo halina mafunzo yoyote.
Kwa sasa tunaomba BASATA, ikae nao kupitia upya mikanda yao kabla ya kuitoa, Tanzania tumejifunza upendo na Amani, wao wanaigiza uchawi, roho mbaya na vituko vingi.
Kwa hivi sasa wanaigiza na watoto wadogo, nao baadaye wanajifanya mastaa wanashindwa kuwaeshimu wazazi,wanashindwa kuwaeshimu walimu, kisa usitaa. Kwani kama wanataka kuigiza na hakuna nafasi ya mtoto, mbona kuna watu vijeba au wenye mapungufu ya ukuzi ,wako kama watoto wapo wengi tu, si wachukue wao.
Katika Bongo movie tumemzaa Wema, ini Kabla, Aunt,Lulu na wengine wenye tabia mbovu. Angalia picha zao kwenye magazeti, kwenye starehe, full kuvua, mwanamke inabidi kuvaaa kistaha bwana.
 
Back
Top Bottom