bongo fleva ziinaboa sana

Hivi inakuwaje msanii wa kiume anaamua kuimba kama mwanamke. Mfano wimbo wa msanii mmoja ambaye hata simjui eti analalamika anateswa na mumewe kwa hiyo anaona bora arudi kwao kijijini akaendelee kukata mkaa, halafu eti anasema labda atayempenda hajazaliwa (realistically mwanamke hawezi kuwa na mawazo kama haya maana wao wanazeeka haraka kuliko wanaume kwa kawaida) muziki unatungwa bila kufikiri, halafu utashangaa eti wimbo kama huo una vuma na kuchukua nafasi kwenye chati zetu za kichovu za kibongo.

Kwa zamani nisingeshangaa kwa sababu hatukuwa na wasanii wa kike ndo maana hata kina Remmy ongala waliimba kama wanawake, lakini sio leo ambapo mtu unaweza kutunga wimbo na kuajiri mwimbaji wa kike.
Am so frustrated.
Jadili.
Ni zimwi la cameroon limewaingia hawa vijana babangu!
 
kuna wimbo mwingine unaitwa muhogo maandazi takataka jtupu


paulss unaujua wimbo huu, una maoni gani, labda nikusaidie tu huu ndio upumbavu ninaolalamikia

thanks dedam for seeing this
 
Mbona kina Eminen wanaimba vya ajabu, tena na matusi lakini ndo mnazipendaaa. Acheni unazi.
Jamaa kaimba, mwenyewe alidhani kaoa kumbe kaolewa. Ametoka ameingiza chake mfukoni, maisha yake yanaendelea. Wewe endelea kukereka.

ahhaaaa kumbe ndo ninyi mnaowapigia kura wasanii wa Bongo Staa Sachi ambao, ambao mara baada ya mashindano kuisha hawasikiki tena! hebu niambie Jumanne Idi katoa single yake ya mwisho lini? huyu alishinda shindano hilo miaka michache iliyopita kwa kura zako na watanzania wengine wenye mawazo kama yako
 
Ze komedy nayo je wanavaa kama wanawake? mi nadhani ndo maana ya sanaa unakamata uhusika mahala ambapo wewe sio muhusika, unaweza ukaimba wewe kama simba au mnyama
 
ahhaaaa kumbe ndo ninyi mnaowapigia kura wasanii wa bongo staa sachi ambao, ambao mara baada ya mashindano kuisha hawasikiki tena! Hebu niambie jumanne idi katoa single yake ya mwisho lini? Huyu alishinda shindano hilo miaka michache iliyopita kwa kura zako na watanzania wengine wenye mawazo kama yako

according to my poor knowledge msanii kuendelea kisanii si kipaji pekee,,,,, vingine vingi vinahitajika mfano kama management inayoelewa biashara ya mziki,,, wapo wanaoimba pumba kila kukicha ila hawatoki maskioni mwetu... Ila wapo wale wenye uwezo wapo doro...
 
Hivi inakuwaje msanii wa kiume anaamua kuimba kama mwanamke. Mfano wimbo wa msanii mmoja ambaye hata simjui eti analalamika anateswa na mumewe kwa hiyo anaona bora arudi kwao kijijini akaendelee kukata mkaa, halafu eti anasema labda atayempenda hajazaliwa (realistically mwanamke hawezi kuwa na mawazo kama haya maana wao wanazeeka haraka kuliko wanaume kwa kawaida) muziki unatungwa bila kufikiri, halafu utashangaa eti wimbo kama huo una vuma na kuchukua nafasi kwenye chati zetu za kichovu za kibongo.

Kwa zamani nisingeshangaa kwa sababu hatukuwa na wasanii wa kike ndo maana hata kina Remmy ongala waliimba kama wanawake, lakini sio leo ambapo mtu unaweza kutunga wimbo na kuajiri mwimbaji wa kike.
Am so frustrated.
Jadili.

Mkuu si kwamba anayelalamika kuteswa na kutishia kurudi kuchoma mkaa kijijini ni mwanaume?. Mtesaji ni mwanamke ambaye ana kipato si haba. Na ukiitazama video ya nyimbo hii nafasi ya mwanamke huyo inachezwa na Anti Ezekieli ambaye anafikia hadi hatua ya kumnyanyasa/kumfukuza mama wa mwanaume ndani ya video hiyo.
 
ahhaaaa kumbe ndo ninyi mnaowapigia kura wasanii wa Bongo Staa Sachi ambao, ambao mara baada ya mashindano kuisha hawasikiki tena! hebu niambie Jumanne Idi katoa single yake ya mwisho lini? huyu alishinda shindano hilo miaka michache iliyopita kwa kura zako na watanzania wengine wenye mawazo kama yako

SIJAWAH KTK MAISHA YANGUB KUMPIGIA KURA MSHINDANI YEYOTE WA BONGO STAR SEARCH. ILA SIWEZI KUWA AGAINST NA MTU ALIEAMUA KUJIPINDA KATENGENEZA WIMBO WAKE HTA KM NI MMOJA UKAMTOA NA AKAPATA CHOCHOTE CHA KUERN LIVING.
katika matsha huwezi ukawfurahisha au kuwapendezesha wote. Na sidhani km ni fahari kusifia vya wenzako badala ya kusaidia kuboresha vya kwenu
 
Mkuu si kwamba anayelalamika kuteswa na kutishia kurudi kuchoma mkaa kijijini ni mwanaume?. Mtesaji ni mwanamke ambaye ana kipato si haba. Na ukiitazama video ya nyimbo hii nafasi ya mwanamke huyo inachezwa na Anti Ezekieli ambaye anafikia hadi hatua ya kumnyanyasa/kumfukuza mama wa mwanaume ndani ya video hiyo.

Afadhali umeelewesha, maana wameumissunderstood/
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom