Lutala
JF-Expert Member
- Jun 17, 2010
- 848
- 103
TMK waanza kebehi kwa waliofulia
na Ruhazi Ruhazi
KUNDI la muziki wa kizazi kipya la TMK Wanaume Family la Temeke Dar es Salaam, limeachia wimbo wake mpya uitwao ‘Wapinzani', unaoonekana kama kebehi kwa makundi yaliyofifia.
Akizungumza na gazeti hili jana, Meneja wa kundi hilo Said Fella, alisema kuwa, sababu ya kuutoa wimbo huo ni kutaka kuwahamasisha wasanii wa makundi mengine kuwa wavumilivu kama wao.
Fella alisema, katika wimbo huo ulioimbwa na wasanii wote wa kundi hilo, pia wameamua kumshirikisha msanii Shaban Katwila ‘Q. Chilla, kwa nia ya kuonyesha mshikamano wao na wasanii binafsi au makundi mengine.
"Mkubwa tumeachia wimbo mpya unaitwa ‘Wapinzani' tumeshausambaza kwenye vituo vya radio, hatujamtukana mtu, ila tunachokifanya ni kuwapa wenzetu ushauri wa kufanya kazi kwa bidii na bila kuchoka kwa faida ya muziki wetu," alisema Fella.
Alisema, wimbo huo utakuwa katika albamu ijayo ya kundi hilo, ambayo wameanza kuiandaa wakitarajia kuitoa baadaye mwaka huu.
TMK kundi ambalo lilikuwa likichuana vikali na East Coast Team, lililokuwa likiundwa na watoto wa Upanga, lilikosa mpinzani baada ya wapinzani wao kutoweka.
Pia kujitoa kwa wasanii kadhaa wakiongozwa na Juma Kassim ‘Sir Nature' kulionekana kungeleta mtikisiko kwa TMK Family, lakini kundi jipya la TMK Wanaume Halisi nalo limeonekana kushindwa kuleta upinzani wa haja.
na Ruhazi Ruhazi
KUNDI la muziki wa kizazi kipya la TMK Wanaume Family la Temeke Dar es Salaam, limeachia wimbo wake mpya uitwao ‘Wapinzani', unaoonekana kama kebehi kwa makundi yaliyofifia.
Akizungumza na gazeti hili jana, Meneja wa kundi hilo Said Fella, alisema kuwa, sababu ya kuutoa wimbo huo ni kutaka kuwahamasisha wasanii wa makundi mengine kuwa wavumilivu kama wao.
Fella alisema, katika wimbo huo ulioimbwa na wasanii wote wa kundi hilo, pia wameamua kumshirikisha msanii Shaban Katwila ‘Q. Chilla, kwa nia ya kuonyesha mshikamano wao na wasanii binafsi au makundi mengine.
"Mkubwa tumeachia wimbo mpya unaitwa ‘Wapinzani' tumeshausambaza kwenye vituo vya radio, hatujamtukana mtu, ila tunachokifanya ni kuwapa wenzetu ushauri wa kufanya kazi kwa bidii na bila kuchoka kwa faida ya muziki wetu," alisema Fella.
Alisema, wimbo huo utakuwa katika albamu ijayo ya kundi hilo, ambayo wameanza kuiandaa wakitarajia kuitoa baadaye mwaka huu.
TMK kundi ambalo lilikuwa likichuana vikali na East Coast Team, lililokuwa likiundwa na watoto wa Upanga, lilikosa mpinzani baada ya wapinzani wao kutoweka.
Pia kujitoa kwa wasanii kadhaa wakiongozwa na Juma Kassim ‘Sir Nature' kulionekana kungeleta mtikisiko kwa TMK Family, lakini kundi jipya la TMK Wanaume Halisi nalo limeonekana kushindwa kuleta upinzani wa haja.