whizkid
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 357
- 240
Katika hali iliyowashtua wengi, mbunge wa upinzani katika bunge la Korea ya Kusini, arusha bomu la machozi katika harakati za kupinga kupitshwa kwa makubaliano ya biashara ya soko huria (FTA) na USA ambayo hatimaye yalipitishwa jioni ya leo nchini mwao. Mabadiliko hayo yatakayofungua milango ya soko huria kati ya nchi yao na USA, EU, India na mataifa mengine yanayotumia sheria ya kimataifa ya masoko, yamepitishwa leo baada ya kupitia upinzani mkali tangu 2007 nchini humo. Bunge liliitishwa ghafla ili wabunge kujadili na kupiga kura, ambapo chama tawala (Grand National Party) kina wabunge wengi hivyo kushinda kwa kura 151 - 7. Waziri mkuu mstaafu Han Myeong-Sook anayetokea chama kikuu cha upinzani nchini humo (Democratic Party) anasema kupitishwa kwa makubaliano hayo si halali kwa sababu ni kinyume na matakwa ya wananchi.
Fundisho Tanzania?
Ama kweli kuwa mpinzani sehemu yoyote duniani ni shughuli nzito. Jamaa hadi karusha bomu la machozi bungeni lakini wapi, kitu kimepita. Kambi rasmi ya upinzani bongo wamesusia bunge lakini wapi. Muswada umepita!
Kimantiki, bunge lililohitimishwa Jumamosi iliyopita halina tofauti sana na hali hii ya Korea Kusini. Kote mijadala ni mambo yenye maslahi kwa taifa husika. Tofauti tu huku hayakuwa mabomu ya machozi katika harakati. Bali ni bomu zito la hotuba ya kambi rasmi ya upinzani alilolitoa Tundu Lissu kupitia hotuba yake kisha kususia vikao vya bunge, yeye na wenzie. Baada ya wabunge waliobaki Bungeni asilimia kubwa kutumia muda wao kuongea mipasho badala ya hoja, hatimaye muswada ulipitishwa. Kwa mbwembwe zote, shangwe na vigelegele.
Wapinzani na wapenda mabadiliko wanatambua kuwa hatua zote zitapitiwa lakini mwisho wa siku, CCM wana agenda yao ambayo lazima wataisimamia. Mkuu wa kaya ameshasema isiwe nongwa tunamuandama yeye mbona wengine waliomtangulia wamepitisha katiba? Ameonyesha mtazamo na msimamo wake. Kilichobaki ni nini? Tuingie mtaani kama Tahrir square? Au tuendelee kungoja kwanza? Wahenga na methali zao wachokozi sana. Eti ngoja ngoja yaumiza matumbo. Simba mwenda pole ndie mla nyama. Wananchi tumekuwa simba waenda pole kwa muda mrefu na matumbo yanauma, wakati nyama tunajua ipo wapi! TUKALE NYAMA!
**UPDATE:**
Mwaka 2008, wapinzani walienda na nyundo kuvunja mlango wa chumba ambapo kikao cha kamati ya bunge kilikuwa kinajadili muswada huu uliopitishwa leo. Hawa wapinzani wa South Korea ni noma!