Bomoabomoa Dodoma imenihuzunisha sana.

huyo sinana ndio nani na anawekeza nini jangwani?

SINANA INTERP.
ANAUZA MATREKTA YA KILIMO KWANZA.
Ndo aliwahonga CDA,POLICE na Mahakama ya ARDHI.Haingii akilini kwanini LUKUVI aliwambia eneo hlo msiliguse,Msekela nae alikataa kuhamishwa kwa wananch

Huyu Mr Maimu ndo mwenye kampuni hyo ya Sinana interpr,nyuma yake kuna AGREY MWANRI HUYU NI NANI PALE TAMISEMI
 
Kusema ukweli lazima tuwaulize CDA,
Kwanini hawakuzuia nyumba ya kwanza kujengwa hadi zikajengwa nyumba 181 kwenye eneo walilo uza kwa mwekezaji wao?
Hivi ni fikra gani inatumika kuboa nyumba 181 bila kuzingatia ubinadamu na amani inayotajwa Tanzania?
Ama kweli TZ tutaandamwa na laana zisizo kuwa na mwisho.
Haya ndio maisha bora kwa kila mdanganyika
 
Nimeumizwa na kitendo cha serikali kuwabomolea wananchi jumbazao huko dodoma eti kumpisha mwekezaji.Nimemsikia mama mmoja kwenye taarifa ya habari ya ITV akilia baada ya nyumba yake kuvunjwa huku akisema amani Tanzania haipo.Hii inamaana gani?

Hapo ndipo tulipofika watanzania. Kwa kutumia kisingizio cha kutovuruga amani, serikali ya ccm imelkuwa ikiwakandamiza wananchi wake na kila anayesimama kujaribu kuwatetea anabandikwa jina la mvuruga amani. Kuna wakati nilishawahi kuandika humu jamvini kuwa 'peace is not the absence of war'. Kwa kiswahili ni kusema kutokuwa na vita hakumaanishi kuwa na amani. Amani ya kweli itakuja tu wakati wananchi wanaishi bila ya kuwa na hofu katika maisha yao. Hawana hofu ya kesho watakula nini, watakaa wapi, watoto wao watasoma wapi na kupata elimu ya namna gani, hawana hofu ya kwamba wakiugua watatibiwa wapi na watapata huduma gani ya afya. Tanzania haiwezi kuitwa nchi ya amani wakati kuna matabaka ya walio nacho na wasio nacho. Wengine wakiugua wanapelekwa kutibiwa India, Afrika Kusini au nchi za Ulaya, wakati walio wengi hata uwezo wa kupata huduma kwenye zahanati karibu na wanapoishi hawana. Watoto wa walio wengi hawategemei hata kupata elimu wakati watu wachache wana uwezo wa kuwasomesha watoto wao kwenye shule za gharama kubwa ndani na nje ya nchi. Nchi haiwezi kuwa na amani wakati wawekezaji wanapewa kipaumbele wakati wananchi wanateseka.
Tuamke watanzania. Tumefika mahali pabaya sana. Panapofuka moshi, panawaka moto!
 
chagueni chama cha upinzani....hoo... watatuletea vita
kwani nchi yetu ina amani.....sasa mwalalamika nini?
kazi kwenu, maisha yamepanda bei...nyumba mmebomolewa
bado mtang'ang'ania ccm. dhambi zingine tunaadhibiwa
hapahapa duniani. nadhani hili liwe fundisho kwa watz
wendine...kwamba magamba yanakufa na watu wake.
 
huyo sinana ndio nani na anawekeza nini jangwani?

Hee! eti mwekezaji anataka kujenga shule ktk eneo hilo,halafu kajimilikisha eneo kubwa km la UDOM vile! Halafu cha kushangaza shule zilizopo ktk eneo hilo zinakosa W/funzi.Je huu ndo UWEKEZAJI?
 
Back
Top Bottom