Bomoa-Bomoa ya UFUKWENI si bure

Ni wazi kuwa ubomoaji wa majumba ya kifahari kwenye fukwe ya Bahari ya Hindi,Dar es Salaam inavuta hisia za wengi.Wengine tunafuatilia tukishangaa namna wahuni wachache wa nchi hii walivyojilimbikizia mali na kujenga majumba ya thamani kubwa. Serikali inafanya kusudi kuvuta 'attention' ya watu ili wasahau mambo muhimu kama ya migomo na maisha bora.Serikali inajipalilia moto zaidi.Inaongeza chuki kwa wananchi.Kwanini isifanye sirini?

Tunafaidikaje kuangalia matingatinga yao? Ukweli ni kwamba,kila anayevunjiwa nyumba yake ameshalipwa. Serikali pale inafanya maigizo.Fahamuni kuwa Serikali iko kwenye harakati za kuwaaminisha watanzania kuwa yenyewe na viongozi wake si dhaifu.


Lakini siwalishaambiwa wabomoe tangu mwanzoni wa mwezi wa 4 na wengine waliambiwa waache kujenga wakakaidi sababu ya pesa zao sasa wajue sheria ni msumeno unakata kote kote, na hata ule mkutano wa mei 15 wa nemc na waandishi wa habari na mama tibaijuka waliwaabarisha kuwa wanatakiwa wabomoe nyumba zao wakakaidi
 
Duh..kumbe wameshalipwa..aisee..kwahiyo ni maigizo tu kama ya tamthilia vile..oke..marudio lini na mimi nicheki hilo muvi..
 
Naunga mkono huu uzi 100% inawezekana kabisa pasi na shaka yoyote!!
 
Hili walilolifanya ni kosa ,kuvunja nyumba kandokando ya bahari ,hivi Tanzania au waTanzania hatujawahi kuona huko ughaibuni nyumba kujengwa kandokando ya bahari au hata mawimbi ya bahari kugonga kuta za nyumba ?

Hivi ni chanzo gani cha mto kinachoanzia au kilichoko pwani baharini ? Eti wanaharibu vianzio vya mito ,hapa anadanganywa nani ? Hivi serikali ya Tanzania na viongozi wake hawajatembea nchi za wingine ? Kwa nchi yetu ambayo haina miamba inayozuia maji ya bahari kumomonyoa ufukwe ,je serikali inaweza kujenga uzio wa kuzuia nguvu za mawimbi ya bahari kwa pwani yote ya Tanzania

Tunaambiwa Zanzibar itatoweka baada ya miaka 89 dawa ya kuzuia mmomonyoko ni kuzungusha ukuta kwa kisiwa kizima ,sasa kama serikali haiwezi kwa nini isigawe viwanja katika fukwe ambazo wajenzi watajenga nyumba na kuzuia mawinmi yasichukue udongo ?

Jengine inaonyesha kuna pengo katika wizara za ujenzi ,ufuatiliaji hakuna na kama uou umejaa rushwa ,mtu anajenga tokea msingi mpaka anahamia miaka inapita ,wizara ipo wapi ,kutoa notice haitoshi kwa nini isiwafungulie kesi wanaokiuka amri na kuanza kuchimba misingi ,ikiwa wamevunja taratibu. Sidhani kama hawa watu wamekurupuka tu na kuanza kujenga lazima watakuwa wamepitia kwenye serikali za mitaa na wizarani ,huu ni uonevu na inasikitisha sana sana ,nchi yenyewe masikini watu wake masikini ,leo baada ya kuwajengea nyumba unawavunjia eti wamevunja sheria ,kama wamevunja sheria kwa nini hamuwapeleki mahakamani mnawavamia na sheria zilizopo mikononi mwenu ?
 
Tuwapongeze wale wote ambao hawana nia ya kutuhadaa bali kuhakikisha sheria zinasimamiwa na kufuatwa inavyotakiwa
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom