zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,910
Boko Haram ni jina ambalo limehusishwa na Uislaam na Waislaam na ugaidi kama ilivyo kwa kila kikundi ambacho kinadai haki za nchi zao.
Nelson Mandela na ANC ilipachikwa uharamia wakuwa ni magaidi na Mandela akahukumiwa kifungo cha maisha kwa kusingiziwa ugaidi. Kwa kuwa tu, alikuwa akigombea kukomeshwa kwa ubaguzi wa rangi na madaraka kuhodhiwa na wa Afrika ya Kusini wenye asili ya kizungu na wenye nacho wachache.
Boko Haram ni kikundi kinachopinga wageni wachache na Waafrika wachache wanaokuwa ni vikaragosi vya wageni kuhodhi uchumi wote wakati wengi wa wananchi wao wakiwa hawafaidiki kikamilifu na utajiri wa mafuta uliopo.
Jee, ni halali kuwa Boko Haram ni magaidi kwa kutaka majimbo yao na utajiri wao wa mafuta wauhodhi wenyewe na si wageni na vikaragosi wachache?
Tujadili.
Nelson Mandela na ANC ilipachikwa uharamia wakuwa ni magaidi na Mandela akahukumiwa kifungo cha maisha kwa kusingiziwa ugaidi. Kwa kuwa tu, alikuwa akigombea kukomeshwa kwa ubaguzi wa rangi na madaraka kuhodhiwa na wa Afrika ya Kusini wenye asili ya kizungu na wenye nacho wachache.
Boko Haram ni kikundi kinachopinga wageni wachache na Waafrika wachache wanaokuwa ni vikaragosi vya wageni kuhodhi uchumi wote wakati wengi wa wananchi wao wakiwa hawafaidiki kikamilifu na utajiri wa mafuta uliopo.
Jee, ni halali kuwa Boko Haram ni magaidi kwa kutaka majimbo yao na utajiri wao wa mafuta wauhodhi wenyewe na si wageni na vikaragosi wachache?
Tujadili.