kanga
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 1,025
- 493
Katika kufanya uchambuzi wa usimamizi na uendeshaji wa mashirika na taasisi za umma nimegundua kuwa bodi hizo hazifanyi kazi kama inavyotakiwa bali bodi hizo zimegeuka kuwa magenge ya wezi na majambazi wa mali ya umma.Bodi zimeshindwa kusimamia uawala bora wa uongozi wa raslimali watu na fedha katika taasisi hizo, hivyo kusababisha matumizi mabaya ya madaraka,rushwa na ufisadi wa kutisha.Namshauri JK rais wa nchi ambaye amekuwa akiteua wenyeviti wa Bodi kufanya yafuatayo.
1.kuvunja mara moja bodi za wakurugenzi wa taasisi nyingi ambazo zimekuwa zikitawaliwa na matumizi mabaya ya raslimali.
2.Kuagiza ukaguzi maalum kwenye matumizi ya bodi na wajumbe wake hasa bodi za mazao zote,TANAPA,MIFUKO ya JAMII yote, mamlaka ya Ngorongoro ,TPA
3.Kuhakikisha mjumbe wa bodi anawakilisha bodi siyo zaidi ya moja. kuna watu wanakaa kwenye bodi zaidi ya moja kama akina Prof. Luhanga,Eve Sinare,Juma Kaboyonga,Jenerali Mboma..............................
4.Wabunge kukoma kuwa wajumbe wa bodi yoyote ya taasis ya umma.
5.Waraka wa malipo ya wajumbe wa Bodi yanawekwa rasmi kisheria kwa bodi zote kuwa sawa kuliko ilivyo sasa ambapo yanatofautiana sana
RAISI WANGU LAZIMA UCHUKUE MAAMUZI MAGUMU ILI KULINDA RASLIMALI ZA NCHI.
Haiwezekani mashirika yanakusanya fedha lakini hayatoi gawiwo kwa serikali iliyotoa mtaji bali fedha zinazolishwa zinaliwa tu na wafanyikazi na Bodi. Tazama Bandari wanakusanya fedha nyingi lakini hata miundo mbinu kwenye bandari ni dhaifu sana ,barabara kupitia kule Malawi cargo ni mbaya lakini watu wanatafuna fedha.Bodi za mazao wakulima wanalia tu lakini bodi za mazao hasa Kahawa,Pamb,korosho wajumbe wanalipana mamilion ya fedha in xpense of mkulima , lazima tukomeshe UMAFIA HUU WA BODI NA NI JK TU TUNAKUTUMA.
Wabilahh Tawfiquh
1.kuvunja mara moja bodi za wakurugenzi wa taasisi nyingi ambazo zimekuwa zikitawaliwa na matumizi mabaya ya raslimali.
2.Kuagiza ukaguzi maalum kwenye matumizi ya bodi na wajumbe wake hasa bodi za mazao zote,TANAPA,MIFUKO ya JAMII yote, mamlaka ya Ngorongoro ,TPA
3.Kuhakikisha mjumbe wa bodi anawakilisha bodi siyo zaidi ya moja. kuna watu wanakaa kwenye bodi zaidi ya moja kama akina Prof. Luhanga,Eve Sinare,Juma Kaboyonga,Jenerali Mboma..............................
4.Wabunge kukoma kuwa wajumbe wa bodi yoyote ya taasis ya umma.
5.Waraka wa malipo ya wajumbe wa Bodi yanawekwa rasmi kisheria kwa bodi zote kuwa sawa kuliko ilivyo sasa ambapo yanatofautiana sana
RAISI WANGU LAZIMA UCHUKUE MAAMUZI MAGUMU ILI KULINDA RASLIMALI ZA NCHI.
Haiwezekani mashirika yanakusanya fedha lakini hayatoi gawiwo kwa serikali iliyotoa mtaji bali fedha zinazolishwa zinaliwa tu na wafanyikazi na Bodi. Tazama Bandari wanakusanya fedha nyingi lakini hata miundo mbinu kwenye bandari ni dhaifu sana ,barabara kupitia kule Malawi cargo ni mbaya lakini watu wanatafuna fedha.Bodi za mazao wakulima wanalia tu lakini bodi za mazao hasa Kahawa,Pamb,korosho wajumbe wanalipana mamilion ya fedha in xpense of mkulima , lazima tukomeshe UMAFIA HUU WA BODI NA NI JK TU TUNAKUTUMA.
Wabilahh Tawfiquh