Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu yaanza kukata madeni kwa formula mpya!

R.Mkangala

Member
May 25, 2011
8
4
Jamani ni mwezi wa pili sasa watumishi mbalimbali wa Serikali Kuu na Taasisi zake ambao wameanza kukatwa malipo na Mfuko wa Board ya wanafunzi wameshuhudia utaratibu mpya wa makato hayo, Awali walikuwa wakikata 31,000/= flat kwa wote wanaostahili, sasa wamekuja na formular mpya ambayo wanadai wanakata 10% ya Disposable income ambayo inafikia mtu kukatwa hadi kufikia sh 150,000/- pasina kujali liabilities nyingine, huu utaratibu si sahihi na aukubaliki hata kidogo na inavyoonekana aukufanyiwa utafiti hata kidogo.

Jmani ndugu zangu wana JF naomba tushilikiane kupinga ukandamizaji huu kwa mliopo Jamvini na ambao hawapo jamvini,

Naomba kutoa hoja!
 
Kwani basis ya kulipa kuanzia 1994/95 ilikuwa ni nn hasa,kwa nn hawakuanzia before that period?.Bila shaka waliopitisha huo utaratibu walijiaangalia zaidi,wakaishia kupiga meza!.

Heri hizo pesa zingeenda kuwa nufaisha vilivyo the needy students ambao bado wapo kwenye higher learning institutions,lakini ukweli ni kwamba watu wanarudisha pesa za kampeni na uwezeshaji wa bajeti kupita(BAHASHA).Baada ya kukatwa PAE kubwa tu na bila kuzingatia thamani ya pesa kwa sasa,unakuja tena kukata 10% of disposable income? .

Vyeti venyewe vimezuiwa na vyuo in some cases na watu wanafanya kazi/wanalipwa kama form six leavers!.I can see the peak of these strategic unyonyaji around the corner
 
wadaiwa waliko private sector vipi? Hawadaiwi au ndo awamu yao inakuja? Nijuzeni, maana mimi nadiwa nijue lini naanza kukabwa.
 
Kina jairo, Luhanjo, Sitta, JK etc ndo wenye pesa za kutosha,yet hawalipi chochote kisa wamesoma chuo before 1994,wototo wao wanawalipia kwa mapato yasiyokaguliwa, kazi kupata mpaka uwe kwenye system, kifupi kila kitu kinachofanyika katika nchi hii hata uchape kazi vp ni kwa faida ya genge fulani tu!.

Morali itatoka wapi kwenye mazingira kama haya?
 
wadaiwa waliko private sector vipi? Hawadaiwi au ndo awamu yao inakuja? Nijuzeni, maana mimi nadiwa nijue lini naanza kukabwa.
Nimeiona barua inayowataka waajiri(in this case private)kupeleka details za wafanyakazi wao waliosoma kwenye higher learning institution ili wao wachambue na waone nani anadaiwa kiasi gani then waamue wakatwe kiasi gani kwa mwezi.Mwajiri atakaye shindwa kutimiza hilo anakabiliwa na faini ya 7000,000 kwa kila employee
 
Mm siwaelewi kabisa hawa jamaa. Kwanza mm nilienda mwenyewe kujua deni langu chakushangaza walinipa deni kubwa sana kana kwamba nilichukua heti pesa ya mwaka mmja mara mbili nikawambia kwamba sitaanza kulipa mpaka mfanye malekebisho. Wakasema itachukua muda heti nianze kulipa alafu nitakuja hidai serikali hapo badae. Nikaona hawa jamaa wanacheza kweli wananchi hadi wanakufa bado wanaidai serikali leo hii wanaleta sera hizo.
Inabidi tukae pamoja kama wadau wa hii kitu kwani wao wazee hawakatwi sindowalio tunga sheria hii. Kama tukivalia njuga hili litafanikiwa hila kama tukikaa kimya tutaliwa kama walivyoliwa watu wa DESI/UPATU na mambo mengine.

Tuamke jamani watz tuache kubuluzwa na wachache hawa.
 
mi siwashangai sana kwani hayo wanayoyafanya ndo hata mawaziri wanafanya!hawaheshimu makubaliano! mi kama mmoja wao lazima tutafute jinsi ya kuwajuza wananchi juu ya huu ufilauni wao na jinsi wanavoufanya! wakati wa kuchukua mkopo tulisaini fomu na bado tunazo! REPAYMENY MUST BE DONE WITH IN TEN YEARS SOON AFTER EITHER EMPLOYED/SELF EMPLOYED! sasa haya mambo ya ten percent yanatoka wapi??? najua hii ni signal kwamba nchi haina pesa hadi wanakopa na njia nyingine ni kisingizio cha kukata mishahara kwa ajili ya kufidia mikopo! hatukatai wakate na WADOGO ZETU WASOME ILA WAKATE KULINGANA NA MAKUBALIANO! MKATABA LAZIMA UHESHIMIWE! HAO NI VIONGOZI NA LAZIMA WAONESHE MFANO WA KUHESHIMU MIKATABA!!! matokeo ya kutofanya hivo ndo haya tunayoyaona sasa hivi!

LAKINI KAMA HAWAAMINI BASI WAKATE MISHAHARA YETU MWISHO WAKE WATAUONA!
 
Mbona 10% ni kidogo? Je wangekopa Banks si wangelipa zaidi ya hiyo na interest juu. Pia wengi ni vijana ambao bado majukumu hayajapandiana. Jamani DAWA YA DENI NI KULIPA, acheni kutetea hata mambo yaliyo wazi tena ni HAKI na WAJIBU.
 
Tumia akili kufikili nakwetu! Nyie ndo akina jairo wa pili!tunachosema hatukatai kulipa ila mashart yani terms and conditions must be followed!repayment has to be done with ten years sasa haya mambo ya 10% yanatoka wapi??hivi sheria ikibadilika wanaoathirika ni wote ambao wapo kwenye reli au wale ambao wanaingia soon after changes????na mbona wanafunzi hamuwapi muda wa kulipa ni pale tu anapoajiliwa hali makampuni yenu mnatoa grace period ya mamiaka!!!!!!!!!!!

Ni fikira pevu tu zitaleta ukombozi wa nchii na sio wavivu wa kufikiria!-nakwetu fikiria sana katika kujibu hoja sio kupostpost tu! Hii forum wanasoma watu wengi!
 
Mbona 10% ni kidogo? Je wangekopa Banks si wangelipa zaidi ya hiyo na interest juu. Pia wengi ni vijana ambao bado majukumu hayajapandiana. Jamani DAWA YA DENI NI KULIPA, acheni kutetea hata mambo yaliyo wazi tena ni HAKI na WAJIBU.
Mm sipingani na kulipa. sasa wewe unavyosema kwamba ss vijana majukumu hayajapandana nakushangaa sana tena sana. hujui kwamba ss ndounakuta tunalea familia zetu kama wazazi, wadogo zetu waende shule na mambo mengine halafu unasema hayo maneno. Nazani hayo maneno nikwajili ya watoto waviongozi na matajiri sio ss ambao tunajua jinsi tunavyoteseka hili ndugu na jamaa zetu wapate japo mlo wa siku.
 
mbona mimi niko private na ninalipa tayari zaidi ya maika 4 na mwisho ni miaka kumi? Je wana recalculate tena repayment yangu? Hawa sasa naona wanazidi kutuchokoza. Kama wataleta madai mapya basi nikuwafuata pale Tildo na kusambaratisha hiyo ofisi yao maana tunahitaji muundo mpya wa watu wanaofikiri kwa ubongo na si ma.....lio.
 
Hivi hawajuhi kuwa binadamu wa sasa wamebadilika kama climate change. Hawaoni kuwa sasa London's burning! Waache wabip
 
Wakati huu utaratibu wa kukopa kwa mkataba maalum unaanza miaka ya 2004/2005 mkataba ulisema kwamba mda wa chini kabisa ni miaka 10 kurudisha deni lote

Kwa utaratibu wa 10% ya sasa hivi kuna watu wanakatwa laki moja na zaidi kwa mwezi na huyo mtu anadaiwa tuseme mil 3 hivi,anatakiwa kumaliza deni katika mda usiozidi miezi 30!
 
Dawa ya deni kulipa, lipeni ili kizazi cha sasa kipate nafuu ya mkopo. Mkataba pia unabidi uheshimiwe.. Tutazame mbeleni!
 
Mbona 10% ni kidogo? Je wangekopa Banks si wangelipa zaidi ya hiyo na interest juu. Pia wengi ni vijana ambao bado majukumu hayajapandiana. Jamani DAWA YA DENI NI KULIPA, acheni kutetea hata mambo yaliyo wazi tena ni HAKI na WAJIBU.

Duuhh, sasa kumekucha. Wamefilisika
 
Wasitake tuivamie TIRDO,patachimbika si kidogo hawa wahuni wanatunyonya na bado wanataka kutuchuna ngozi kabisa,kama wanahisi ni rahisi hvyo kwanini wasijaribu kuanza na kukata ya kwao kwa hizo 10%?hizi sheria za kibaguzi eti mara 1994+ ndo walipe kwa nini?kwanini isiwe 1990s wote?sahv ndo mtu kapata kazi na wengine bado,ajira nzuri wanawapa wapenzi wao na watoto wao alafu wanataka makato bila mpango,huko migodini tunaambiwa wanasamehewa kodi,yaani opprrrrrrrrression is too big
 
wadaiwa waliko private sector vipi? Hawadaiwi au ndo awamu yao inakuja? Nijuzeni, maana mimi nadiwa nijue lini naanza kukabwa.

Mi nipo sekat binafsi, barua imekuja tunatakiwa kukatwa hiyo 10% ya basic or net i think....mbaya zaidi watu wa scheme moja wanatofautiana amounts due...dah!
 
Back
Top Bottom