Bodi ya Mikopo na utoaji mikopo

NeutralPolitics

New Member
Nov 2, 2016
1
3
Kwa Bodi ya Mikopo. Je, hii ni haki?

Hii ni habari ya kweli. Mimi ni mtumishi wa uma kwa miaka 20 sasa. Kwa kuwa hali ya taaluma katika shule zetu za msingi na o-level haikuwa njema kwa kipindi kirefu, ambapo ni jambo ambalo halikuwa limepewa kipaumbele na mamlaza zilizopaswa, ilinilazimu kuwapeleka watoto wangu ambao wamefikia wanne sasa,katika shule za kulipia hadi kidato cha nne.

Hivi sasa wawili wameingia vyuo vikuu katika michepuo ya utabibu, lakini kilichowapata ni kuwa hawana mikopo eti kwa kuwa walisoma shule za kulipia wana uwezo.
Hii si haki kwa sababu zifuatazo.

1. Kunyimwa mkopo mtoto wangu, mtu ambaye nimekuwa nikilipa kodi ya PAYE hadi sasa sio kunitendea haki hata kidogo. Je nitafutiwa PAYE ili badala yake nilipe Milion 5 (mara watoto wawili sasa walioingia vyuoni) karo ya watoto wangu? Kama sivyo kwa nini niendelee kulipia wengine?

2. Gharama za karo kwa shule za awali ilikuwa mwisho Milion 2.5 kwa mtoto. Hii tulijitahidi kujinyima kama familia ili angalau tuwafikishe watoto katika ndoto zao. Leo hii karo ya mafunzo kozi za utabibu ni Million 5 na laki moja hadi Million 6 na laki saba. Je hapa uwezo wangu mimi umepimwaje na kuniona eti kwa kuwa watoto walisoma private o-level basi wazazi tuna uwezo, na hivi naelekea kustaafu?

2. Ukweli ni kuwa wakati wote wa kusomesha watoto wangu shule za awali tumejinyima sana sana kwa kila hali. Chakula chetu, matumizi mengine yote yamekuwa ni kwa dhiki tukijitahidi kwa ajili ya watoto hawa.

3. Mimi nadhani kila kijana anayeingia chuo, kwa kuwa anakuwa amepita umri wa miaka 18, na atakapomaliza anajenga taifa, anapaswa kuonwa kama raia mwenye haki zake sawa na raia wengine. Tofauti na hapo ni ubaguzi kwake pasipo sababu. Nasi wazazi baada ya kujitoa kwa awali basi tuachwe tujiandalie maisha ya kustaafu sio tena tuje kuishi kwa dhiki, ukizingatia kuwa hawa watoto nao watakuwa na maisha yao na wajibu kwa familia zao baada ya kumaliza. Mishahara ya nchi yetu kulingana na uduni wa uchumi inajulikana. Kipato ni kidogo na hatuwezi wote kukimbilia katika siasa ili tukachume posho.
 
Pole sana mkuu , hii ndio nchi ya viwanda ambavo vinajengwa baada ya raia wake hasa wa hali ya chini na kati kusomeshwa namba.
 
Hivi sasa wawili wameingia vyuo vikuu katika michepuo ya utabibu, lakini kilichowapata ni kuwa hawana mikopo eti kwa kuwa walisoma shule za kulipia wana uwezo.
Nimekuelewa lakini hawa jamaa hawataki kuelewa wao wanaangalia mtoto kasoma wapi wala hawaangalii alikuwa analipiwaje. Serikali hii kama inakopesha wazazi na si vijana. Hiyo means test yao sijui inavigezo vingapi? Leo nimemwambia kijana wangu hata asihangaike kukata rufaa kwani hajataarifiwa kisa cha kukosa mkopo. Sasa aki-appeal anaandika nini? Nimemuambia tufunge mkanda tuone tutafika wapi. Serikali inadai tuna uwezo lakini inalimbikiza stahiki zetu.
 
Hata mimi nimekosa mkopo na nikisoma government zote. Na nimechaguliwa kcmc ada m4.4 naona nyumbani pananihusu.
 
Kwa Bodi ya Mikopo. Je, hii ni haki?

Hii ni habari ya kweli. Mimi ni mtumishi wa uma kwa miaka 20 sasa. Kwa kuwa hali ya taaluma katika shule zetu za msingi na o-level haikuwa njema kwa kipindi kirefu, ambapo ni jambo ambalo halikuwa limepewa kipaumbele na mamlaza zilizopaswa, ilinilazimu kuwapeleka watoto wangu ambao wamefikia wanne sasa,katika shule za kulipia hadi kidato cha nne.

Hivi sasa wawili wameingia vyuo vikuu katika michepuo ya utabibu, lakini kilichowapata ni kuwa hawana mikopo eti kwa kuwa walisoma shule za kulipia wana uwezo.
Hii si haki kwa sababu zifuatazo.

1. Kunyimwa mkopo mtoto wangu, mtu ambaye nimekuwa nikilipa kodi ya PAYE hadi sasa sio kunitendea haki hata kidogo. Je nitafutiwa PAYE ili badala yake nilipe Milion 5 (mara watoto wawili sasa walioingia vyuoni) karo ya watoto wangu? Kama sivyo kwa nini niendelee kulipia wengine?

2. Gharama za karo kwa shule za awali ilikuwa mwisho Milion 2.5 kwa mtoto. Hii tulijitahidi kujinyima kama familia ili angalau tuwafikishe watoto katika ndoto zao. Leo hii karo ya mafunzo kozi za utabibu ni Million 5 na laki moja hadi Million 6 na laki saba. Je hapa uwezo wangu mimi umepimwaje na kuniona eti kwa kuwa watoto walisoma private o-level basi wazazi tuna uwezo, na hivi naelekea kustaafu?

2. Ukweli ni kuwa wakati wote wa kusomesha watoto wangu shule za awali tumejinyima sana sana kwa kila hali. Chakula chetu, matumizi mengine yote yamekuwa ni kwa dhiki tukijitahidi kwa ajili ya watoto hawa.

3. Mimi nadhani kila kijana anayeingia chuo, kwa kuwa anakuwa amepita umri wa miaka 18, na atakapomaliza anajenga taifa, anapaswa kuonwa kama raia mwenye haki zake sawa na raia wengine. Tofauti na hapo ni ubaguzi kwake pasipo sababu. Nasi wazazi baada ya kujitoa kwa awali basi tuachwe tujiandalie maisha ya kustaafu sio tena tuje kuishi kwa dhiki, ukizingatia kuwa hawa watoto nao watakuwa na maisha yao na wajibu kwa familia zao baada ya kumaliza. Mishahara ya nchi yetu kulingana na uduni wa uchumi inajulikana. Kipato ni kidogo na hatuwezi wote kukimbilia katika siasa ili tukachume posho.
Pole sana ndugu yangu. Bahati mbaya hili limekugusa moja kwa moja lakini pia huwezi jua kesho utaguswa na lipi ktk serikali hii. Tunahitaji kubadilisha mfumo, ccm imechoka na haina jipya. Tujaribu kuwa kama marekani, tukubali kufanya mabadiliko kwa maslahi yetu watanzania. Pole sana
 
Tena hapo ukute unakatwa PAYE laki 5/6 kwa mwezi ni pesa nyingiii. .
Hawajui kuwa kuna wengine kwasababu mbalimbali hawakuweza soma serikalini...mfano kuchelewa kuripoti...kukosa nafasi shule ya serikali nk ...so mtu akifeli la 7 abaki home asijiongeze kwenda private
 
Tena hapo ukute unakatwa PAYE laki 5/6 kwa mwezi ni pesa nyingiii. .
Hawajui kuwa kuna wengine kwasababu mbalimbali hawakuweza soma serikalini...mfano kuchelewa kuripoti...kukosa nafasi shule ya serikali nk ...so mtu akifeli la 7 abaki home asijiongeze kwenda private
Bora na huyo wa private .
Sasa mm nmeanza kusoma shule za serikal kuanzia chekechea mpaka advance lakn n mwendo wa not allocated. Ata sielew sasa watoto wa maskin waliopata n kina nan?
Jpm watoto wa nchi yako tunaangamia tuangalie na Sisi huku Kama hela hamna mbona ata bakheresa anaweza kutoa msaada tu au ndio mmetuamulia tu mwaka huu wasom wawe wachache.
 
Iv kwel kuna second batch, sasa kama hamna c waandike tu kua tumekosa mkopo sio not allocated in first batch
 
km unastaafu utamsomesha tu maana pesa utapewa au 75million utafanyia nini?
Mkuu kwenu kuna mtu aliyestaafu ukaona hali anayopitia?. Wabunge wanalipwa mamilioni ya fedha lakini bado hawataki kustaafu sembuse mtumishi wa kawaida?. Medical school ada yake ni kubwa sana kwa watoto wawili bila mkopo ndani ya miaka mitano itamgharimu sana. Ada, chakula, malazi, vifaa na mengineyo, yeye mwenyewe ana familia na mambo kibao milioni 75 sio kitu hapo.
Zingatia;: ukistaafu pesa inayotoka ni kubwa kuliko inayoingia otherwise uwe ulijiajiri kwenye sekta nyingine.
 
Back
Top Bottom