Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Alitoa mfano, kwamba katika makubaliano hayo, vyuo vinapaswa kuleta orodha ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliosajiliwa ndani ya siku 30, lakini vyuo havizingatii hilo.
Kuhusu TCU, mtendaji huyo wa Bodi alisema pia imekuwa ikichelewesha taarifa za wanafunzi waliodahiliwa ili waandaliwe mkopo wao.
Alitoa mfano, kwamba zipo taarifa ambazo Bodi ilipaswa kuzipokea Novemba mwaka jana, lakini majina yaliletwa mwezi huu.
Alitoa mifano mingine ya vyuo ambavyo vilikumbwa na migomo na maandamano huku Bodi ikitajwa kuwa chanzo, kikiwemo Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE) na kusema chuo hicho kilishindwa kuwasilisha namba za akaunti za wanafunzi kwa wakati na hivyo kusababisha ucheleweshaji kwa zaidi ya wiki tatu.
vipi mikopo ya wanafunzi, ina mana wanafunzi wanakopesha kwa kwenda kusoma nje/ndani ya nchi.
halafu malipo inakuwaje, watalipa wazee wao au wakipata kazi, ndio wataanza kulipa huo mkopo/deni?