Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Binafsi sioni mantiki ya kulipisha ada ya maombi ya sh elfu 30 kwa waombaji wa mikopo kwenye bodi ya mikopo ya wanafunzi. Bodi hii inagaramiwa na serikali hivyo haihitaji kuwakamua wanafunzi hawa ambao wengi wao wanatokea familia masikini. Bodi inapata zaidi ya bilioni 2 kama ada ya waombaji, hela ambazo ukiongeza na ruzuku wanayopata serikalini, zinachochea ufisadi kwa bodi hii yenye utendaji mbovu.