BODI ya Chakula, Dawa na Vipodozi Zanzibar imefanikiwa kukamata tani mbili za tende zilizokwisha muda wake katika maghala mawili Mjini Zanzibar.Tende hizo zimegunduliwa zikiuzwa na wafanyabiashara wadogo wadogo (wamachinga) katika maeneo ya Darajani kwa bei ya Sh500 kwa nusu kilo na kupigwa Muhuri wa bandia kuwa zinafikia kikomo cha matumizi yake mwaka 2012.
Ukamatwaji wa tende hizo unatokana na Operesheni ya kukagua bidhaa katika Mabucha mbali mbali ya Nyama kulikofanywa na Bodi hiyo jana katika maeneo mbali mbali ya Mjini Zanzibar.
Ukamatwaji wa tende hizo unatokana na Operesheni ya kukagua bidhaa katika Mabucha mbali mbali ya Nyama kulikofanywa na Bodi hiyo jana katika maeneo mbali mbali ya Mjini Zanzibar.