Boarding school

uncle

JF-Expert Member
Dec 10, 2007
322
184
Poleni na shughuli nyingi wana JF.
Ndugu wana JF ,nina watoto wawili wa darasa la pili na la tatu,nawatafutia shule ya boarding (mchanganyiko wa kiume na wakike ),maeneo ya Dar au mkoa wa Pwani.
Aina ya shule ningependa iwe ile inayotoa elimu bora na inayozinagtia maadili mema na uangalizi mzuri kwa watoto wakati wote wawapo shuleni.
Tafadhalini wana JF mwenye taarifa naomba anipatie mawasiliano.
 
mwanzo walikuwa wanasoma wapi? kwanini unawahamisha na kutafugta boarding??
nakushauri tafuta primary school iliyo karibu yako n a uwapeleke hapo, na watasoma na kuwa kama wewe iwapo tu utawapatia mazingira mazuri kaka.then hiyo pesa ya boarding kama wana account benk nendas ukawawekee kama hawana fungua account kwa ajili yao zitawasaidia baadae, na ukiziweka huko benk usitie mkono wala mguu kuzichukua na kuzifanyia mambo yako hata kama ni mambo ya familia.
 
Hatari!
Jamani nilisikiliza kipindi kwenye radio on sunday,nilibaki nasikitika tu. Mtoto wa darasa la pili alikuwa akiingiliwa na mzee wa miaka 74 kwa miaka kadhaa. Na mpaka wazazi wanagundua ni baada ya kukuta alikuwa hajaandika notes kwa zaidi ya miezi 6. Huyo Fisadi alikuwa anavyo vitoto kama 6 na alikuwa akivishawishi mpaka vinaiba chakula nyumbani vinakwenda vinajipikia kwake kabla hajavianza kuvishugulikia,lakini baya zaidi ana UKIMWI! Wazazi tuzitafute hizi pesa na kazi lakini ni muhimu kumuuliza mtoto kila siku hali ya shule na kuwauliza walimu,la sivyo hamna haja ya kuwa bussy na kazi huku mtoto anaumizwa.Na hilo ni la muhimu kulijua wakati unatafuta shule.
 
Watoto wa darasa la pili Boarding? Mzazi utapata wapi muda wa kumfahamu mwanao? Jamani tuangalie sana watoto wasije wakafunzwa na ulimwengu wakiwa bado wachanga kabisa
 
Wapeleke bagamoyo kwa father bayo ......ana shule nzuri sana ya boarding ya primary..pia bagamoyo kuna shule ingine inaitwa..Mwasama ni nzuri sana na ina wanafunzi wachache sana.......huwa wanafaulu woote..kazi kwako.
 
Back
Top Bottom