Boarding school za Tanzania nyingi zimeanzishwa kwa wigo wa jela ya watoto, kuna nadharia ya kijinga iliyoota mizizi kuwa boarding schools ni kwa ajili ya watoto watukutu na watundu wasiosikia.
Ni chache sana ambazo zinaanzishwa kwa nadharia kuwa mwanafunzi anaepelekwa ni kwa ajili apate utulivu na aondokane na vishawishi vya mitaani ili apate ku "concentrate" na masomo.
Ni wakati muafaka nyingi ya hizi shule zibadili nadharia, muundo na hata muelekeo. Shule hizi za boarding ziundwe kwa nadharia ya kuwapatia wanafunzi "comfort" ya hali ya juu, kimalazi, makazi, lishe bora na nzuri, michezo ya kuwajenga miili na akili na kuwafanya wawe wanaipenda shule na masomo kuliko nyumbani na vishawishi vya mitaani.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.