Mpui Lyazumbi
JF-Expert Member
- Sep 1, 2010
- 1,856
- 371
Wakuu heshima mbele. Nimeanza mwezi wa kumi na mbili kwa faraja kuu. Kwamba ifikapo tarehe 09 natimiza umri wa miaka 50-sambamba na uhuru wa Tanganyika. Kwa kweli ni safari ndefu sana, na naomba nilete kwenu siku yangu muhimu kabisa. Na kwa kawaida yake, wanabodi mtazungumza mengi hasa yenye kunijenga mkizingatia kuwa miaka 50 si haba. Kuna wengi hawakuisogelea kiasi changu na kuna waliozidi hapa. Nasema binafsi nimekuwa na mafanikio kiasi katika MAISHA na mchango wangu umekuwa wa kuridhisha katika ujenzi wa TAIFA. Hata hivyo kasi ya kujiletea maendeleo kama taifa bado ni ndogo sana. Tufanye nini kwa ajili ya mafanikio ya kizazi kijacho?
NAWASILISHA.
NAWASILISHA.