Binti akisema amekufananisha na kaka yake!

Gaijin; Umesema huyo mtu alikufananisha na akasema alishawahi kukuona mahali. Sasa mimi nimefananishwa na nikahoji kabisa vigezo vilivyotumika hadi nikafananishwa na jibu nililiambulia ni "Sijui" ..... Suala la kwa nini hakuniambia sababu hasa ya kunifananisha, hapo ndipo nahisi kufumbiwa fumbo! Waswahili wanasema fumbo mfumbie mjinga, mwerevu ataling'amua.. Isije ikawa hapa napimwa werevu au ujinga wangu hapa:teeth::teeth:

Huyu sikumuuliza kanifananisha nini maana sikumuuliza maybe angenambia hajui pia.

Yeye kakumbuka kuwa keshawahi kuniona kwa sababu Mara ya kwanza aliponiona alinifananisha ATI

Unaweza mtu ukamjua miezi na usijue umemfananisha kiti gani hasa kama hamna mazowea.

Besides inaweza kuwa imemclick time hiyo kuwa kakufananisha
 
Kama ujaoa sasa kama kichwa hicho mzee kimeshaingia chenyewe ! ukikutana nacho kiambie dada yangu yale maneno yako bado nayakumbuka akisema kwanini mwambie hujui kwanini? Siku ipo ataongea ukweli alikuwa anamaanisha nini!
 
Nashukuru kwa ushauri mkuu, kwa hiyo wewe ulimpotezea au?
Mimi huyu hajawahi kunililia shida so far na wala hatujawahi kualikana makwetu zaidi ya kukutana kazini labda na mtaani sometimes.
Ila nimependa penye red na nitaufanyia kazi ushauri wako kaka....

mimi nlimpotezea japo alikuwa mzuri ila mi niliona hatuendani. Ngeweza kufanya lolote ila skupenda kumchezea mana sijawa tayari kwa ndoa,na najua yeye alikuwa akisaka ndoa. Kaka mtu anakuja anakaa kwako leo mpaka usiku,kesho mpaka usiku n.k sasa unategemea nini,ukidhubutu si ndo anafuata mizigo yake nyumbani kwao? Kaka kama uko interested we weka mitego yako akianguka umo ujue wako. Kaka ama huna software ya kutegea?! Hawa ndugu ni weak sana huwezi amini! Unataka software?sema kaka usione noma,kwa sekta hii ata mkuu wa nchi mwenyewe huwa anaitegea sikio labda mapadre tu ndo hawausiki apa!
 
Huyu sikumuuliza kanifananisha nini maana sikumuuliza maybe angenambia hajui pia.

Yeye kakumbuka kuwa keshawahi kuniona kwa sababu Mara ya kwanza aliponiona alinifananisha ATI

Unaweza mtu ukamjua miezi na usijue umemfananisha kiti gani hasa kama hamna mazowea.

Besides inaweza kuwa imemclick time hiyo kuwa kakufananisha

Gaijin; nashukuru kwa mtazamo wako Dada yangu. Ila penye red nadhani ndiyo sababu yenyewe ya huyo mtu wako kukufananisha.
Mwenzio niliambiwa tu tena nje kabisa ya mazungumzo yetu ya awali (akakaa kimya ghafla halafu akaonesha sura ya msisitizo nimsikilize), nanukuu:
Binti: TANMO nakufananisha kweli na kaka yangu!
Mimi: Kwa nini umesema hivyo?
Binti: Sijui kwa nini, ila naona kama mnafanana (akacheka).
Mimi: (nikiwa na butwaa) Hehe, haya Bana, basi twenzetu tukaendelee na kazi..

Kama ujaoa sasa kama kichwa hicho mzee kimeshaingia chenyewe ! ukikutana nacho kiambie dada yangu yale maneno yako bado nayakumbuka akisema kwanini mwambie hujui kwanini? Siku ipo ataongea ukweli alikuwa anamaanisha nini!

Kaka ushauri nimeusikia, naahidi kuufanyia kazi...
 
mimi nlimpotezea japo alikuwa mzuri ila mi niliona hatuendani. Ngeweza kufanya lolote ila skupenda kumchezea mana sijawa tayari kwa ndoa,na najua yeye alikuwa akisaka ndoa. Kaka mtu anakuja anakaa kwako leo mpaka usiku,kesho mpaka usiku n.k sasa unategemea nini,ukidhubutu si ndo anafuata mizigo yake nyumbani kwao? Kaka kama uko interested we weka mitego yako akianguka umo ujue wako. Kaka ama huna software ya kutegea?! Hawa ndugu ni weak sana huwezi amini! Unataka software?sema kaka usione noma,kwa sekta hii ata mkuu wa nchi mwenyewe huwa anaitegea sikio labda mapadre tu ndo hawausiki apa!

Mamaaaa!!! mbavu zangu..
Mkuu nihitaji software itakayonisaidia ku-crack system ya huyu binti ili nijue hasa alikusudia nini kunipa kauli kama ile.......
 
Wakuu kuna binti ameniambia huwa ananifananisha na kaka yake na nimeshindwa kabisa kumuelewa anamaanisha nini.

Huyu binti tunafanya naye kazi sehemu moja na tuna mazoea ya kawaida kabisa ya kikazi zaidi. Kwa kweli ni binti mzuri na yuko singo. Binafsi sijawahi kumuonesha interest yeyote ingawa wakati mwingine huwa tunakuwa na matani ya hapa na pale (mara nyingine kuhusu mapenzi na maisha). Siku moja nikiwa nataniana naye mara ghafla akabadilisha topiki na kwa sauti ya msisitizo kabisa akaniambia kuwa huwa ananifananisha na kaka yake, nilivyomuuliza kwa nini akasema hata yeye mwenyewe hajui. Sikutaka kuendelea zaidi manake hata mimi nilipigwa na butwaa (kutokana na jinsi alivyosema kimsisitizo), tukaendelea na maongezi mengine.

Baada ya lile tukio huwa mara kwa mara najiuliza kuwa yule binti alikusudia nini, hasa ukizingatia kuwa sikuwahi kutegemea kwamba itafika siku ataniambia maneno hayo (tena kwa jinsi alivyoonesha kumaanisha anachokisema). Kama ameniambia kujilinda zaidi najiuliza kwa nini? wakati sijawahi kuonesha kumtaka? Au matani yangu yanamfanya adhani kuwa namtaka? Kama hakukusudia kujilinda ina maana ndo nimepewa taarifa kuwa milango ipo wazi?

Msaada wandugu!!!
Wewe kwani mtu akikufananisha ndio anakutaka kimapenzi?tena kakufananisha na kaka yake ina maana muheshimiane kama mtu na dada yake,na je kama angekuwa mwanaume mwenzako kakufananisha na dada yake ungesema anakuta kimapenzi?
 
Wewe kwani mtu akikufananisha ndio anakutaka kimapenzi?tena kakufananisha na kaka yake ina maana muheshimiane kama mtu na dada yake,na je kama angekuwa mwanaume mwenzako kakufananisha na dada yake ungesema anakuta kimapenzi?

Wataalamu wanasema kuwa binaadamu tunakuwa attracted kimapenzi na watu wanaofanana na familia zetu :)
 
Wewe kwani mtu akikufananisha ndio anakutaka kimapenzi?tena kakufananisha na kaka yake ina maana muheshimiane kama mtu na dada yake

Inawezekana ndiyo maana nataka kupata mtazamo wa Great thinkers mkuu, manake penye wengi unaweza kupata mawazo tofauti na ya msingi..

na je kama angekuwa mwanaume mwenzako kakufananisha na dada yake ungesema anakuta kimapenzi?

Dah! Si mchezo. Ila sintoshangaa kama akinipa na sababu (labda dada anatabia kama zangu - "let's say ni mkimya" au "Mkorofi" hii ni kwa mfano tu). Ila akiniambia tu na kuishia kusema hajui kwa nini tunafanana basi nitamshangaa. Na cha kufanya au kufikiria nitakipata kulingana na jinsi atakavyo iwasilisha kauli yake.

Pamoja kaka...
 
Wataalamu wanasema kuwa binaadamu tunakuwa attracted kimapenzi na watu wanaofanana na familia zetu :)

Gaijin; kweli?
Nipe somo dada yangu nisijekuwa simtendei haki binti wa watu...
 
Gaijin; kweli?
Nipe somo dada yangu nisijekuwa simtendei haki binti wa watu...

Hiyo ni kweli kwa mujibu wa watafiti. Na wanasema inatokea unconsciously.
Watu wana tendency ya kutafuta partners wanaofanana na familia zao au watu waliokuwapo around walipokuwa wadogo

*note: sisemi kuwa huyo kawa attracted na wewe au kila binaadamu akimfananisha binaadamu mwenziwe na familia yake ni kuwa ana sexual feelings.
 
Tukiwa bado kwenye kufananishwa..vipi kama mtu kakufananisha na mtu aliye cheat na mwenzake halafu atake kukupa kibano?

Mimi nishawahi kufananishwa na watu mara nyingi sana. Vitoto vishawahi kunifananisha na baba zao, kuna demu alishawahi kunifananisha na ex wake (nami nikapata upenyo wa kurusha ndoano hapo hapo lol).

Kufananishwa kuna faida na hasara zake bwana.
 
Mimi sipendi kufananishwa hasa na mtu ambaye yupo kwenye position ya kuonana nae mara kwa mara.

Nahisi kama ndo 'nalazimika' kuwa rafiki yake kwa kuwa nimefanana na dada yake japo sikuwa na mpango huo. :s

( hata akiwa mfananishaji ni mwanamke mwenzangu)
 
ina maana wewe ni sawa na kaka yake!huwezi kumu approach.ndiyo maana wanaume wengi hawataki salamu ya shikamoo toka kwa mabinti,maana binti ukimuomba atakuambia ninakufananisha au kukuheshimu kama baba au kaka
 
Kwa maoni yangu binafsi, sina tatizo na ufananisho huo, si kufananishwa tu? mi nilidhani ungeishia hapo kuliko kupeleka mawazo mbali zaidi, kwa mfano, angekuja akaku-kiss shavuni, just a simple kissing, je ungesema anakupenda? au akikukumbatia? mpwa, dalili ya mvua ni mawingu, usilazimishe mvua kuja kabla ya mawingu, yaweza kukuletea aibu! simba mwenda pole.....
 
Wakuu kuna binti ameniambia huwa ananifananisha na kaka yake na nimeshindwa kabisa kumuelewa anamaanisha nini.

Huyu binti tunafanya naye kazi sehemu moja na tuna mazoea ya kawaida kabisa ya kikazi zaidi. Kwa kweli ni binti mzuri na yuko singo. Binafsi sijawahi kumuonesha interest yeyote ingawa wakati mwingine huwa tunakuwa na matani ya hapa na pale (mara nyingine kuhusu mapenzi na maisha). Siku moja nikiwa nataniana naye mara ghafla akabadilisha topiki na kwa sauti ya msisitizo kabisa akaniambia kuwa huwa ananifananisha na kaka yake, nilivyomuuliza kwa nini akasema hata yeye mwenyewe hajui. Sikutaka kuendelea zaidi manake hata mimi nilipigwa na butwaa (kutokana na jinsi alivyosema kimsisitizo), tukaendelea na maongezi mengine.

Baada ya lile tukio huwa mara kwa mara najiuliza kuwa yule binti alikusudia nini, hasa ukizingatia kuwa sikuwahi kutegemea kwamba itafika siku ataniambia maneno hayo (tena kwa jinsi alivyoonesha kumaanisha anachokisema). Kama ameniambia kujilinda zaidi najiuliza kwa nini? wakati sijawahi kuonesha kumtaka? Au matani yangu yanamfanya adhani kuwa namtaka? Kama hakukusudia kujilinda ina maana ndo nimepewa taarifa kuwa milango ipo wazi?

Msaada wandugu!!!

kwa sisi wataalamu wa fasihi tunasema hicho ni kibuti kitakatifu na cha kidiplomasia , wewe ulishaona wapi dada akaolewa na kaka yake? umepewa cheo cha u kaka ili utulie bana. mdada kaona unampigia misere kidizaini. umeongea kwamba haujaonesha dalili ya kumtaka lakini hayo majokes yako pengine yamempa tafsiri nyengine. karibuni nitaanzisha sredi kule jukwaa la lugha kuelezea matumizi ya neno "kaka", nimeona upo umuhimu huo.

-THE END-
 
Hiyo ni kweli kwa mujibu wa watafiti. Na wanasema inatokea unconsciously.
Watu wana tendency ya kutafuta partners wanaofanana na familia zao au watu waliokuwapo around walipokuwa wadogo

*note: sisemi kuwa huyo kawa attracted na wewe au kila binaadamu akimfananisha binaadamu mwenziwe na familia yake ni kuwa ana sexual feelings.

Nashukuru kwa ufafanuzi dada yangu (hasa kwenye red), basi ngoja nifanye kautafiti halafu nitakuja kukupa feedback..
 
kwa sisi wataalamu wa fasihi tunasema hicho ni kibuti kitakatifu na cha kidiplomasia , wewe ulishaona wapi dada akaolewa na kaka yake? umepewa cheo cha u kaka ili utulie bana. mdada kaona unampigia misere kidizaini. umeongea kwamba haujaonesha dalili ya kumtaka lakini hayo majokes yako pengine yamempa tafsiri nyengine. karibuni nitaanzisha sredi kule jukwaa la lugha kuelezea matumizi ya neno "kaka", nimeona upo umuhimu huo.

-THE END-

Hapana...ni mapema mno kwa yeye kukonkludi hivyo. Yeye ni avute tu subira kwani kama totoz kweli anampenda jamaa basi ataonesha hints zaidi.

Kuna watu mahusiano yao wakikusimulia jinsi walivyoanza utabaki mdomo wazi. Hii ya kaka-dada ni ishu mdogo kabisa.
 
ina maana wewe ni sawa na kaka yake!huwezi kumu approach.ndiyo maana wanaume wengi hawataki salamu ya shikamoo toka kwa mabinti,maana binti ukimuomba atakuambia ninakufananisha au kukuheshimu kama baba au kaka

Nashukuru kwa ufafanuzi mkuu. Nitaufanyia kazi.....

Amekuona hakuna mwelekeo wowote wa yeye na wewe kuwa wapenzi!!

Kwa maoni yangu binafsi, sina tatizo na ufananisho huo, si kufananishwa tu? mi nilidhani ungeishia hapo kuliko kupeleka mawazo mbali zaidi, kwa mfano, angekuja akaku-kiss shavuni, just a simple kissing, je ungesema anakupenda? au akikukumbatia? mpwa, dalili ya mvua ni mawingu, usilazimishe mvua kuja kabla ya mawingu, yaweza kukuletea aibu! simba mwenda pole.....

Naam, nimekupata Bandugu.. Ushauri wako utazingatiwa.....

kwa sisi wataalamu wa fasihi tunasema hicho ni kibuti kitakatifu na cha kidiplomasia , wewe ulishaona wapi dada akaolewa na kaka yake? umepewa cheo cha u kaka ili utulie bana. mdada kaona unampigia misere kidizaini. umeongea kwamba haujaonesha dalili ya kumtaka lakini hayo majokes yako pengine yamempa tafsiri nyengine. karibuni nitaanzisha sredi kule jukwaa la lugha kuelezea matumizi ya neno "kaka", nimeona upo umuhimu huo.

-THE END-

Bwana Mtaalamu wa Fasihi, naomba ufanye hima kuanzisha hiyo sredi angalau itasaidia kuondoa mkanganyiko...
Ila kama ulivyosema, kutaniana kwetu labda mwenzangu alikuchukulia kama mitego ya kumnasa na ameamua kujihami kabisa....
Nitalishughulikia hili suala ili nipate ufumbuzi though.
 
Back
Top Bottom