Binti akatoa ile Mimba.

kande kavu

JF-Expert Member
Sep 17, 2011
234
86
Ni mabinti wawili mapacha na jirani zetu. Wazuriiii kwa sura na maumbile hasa yule wa pili.Wa kwanza ni mzungumzaji na mcheshi sana, mwingine ni mkimya na mwenye soni tele.Kisa hiki cha kweli kinamhusu yule binti wa pili.

Wakiwa kidato cha pili na binti wa kwanza akivuma kwa kugawa pipi, sifa nyingi zikapelekwa kwa huyu binti wa pili kwa utulivu. Hakuwahi kusimama atumwapo sokoni wala kisimani, hakuna mtu anashuhudia kuwa aliwahi kumuona huyu binti kasimama au kuongea na yeyote wa jinsia tofauti naye, kwani hata hao mabinti wenzie ilikuwa nadra.Wakati huo balekhe ikichanganya watu tulijaribu bahati zetu tukaambulia patupu kwani binti ni kakakuona.

Mimba jamani mimba! Mimba ni ngumu kuificha kumbe! Huyu binti wa pili akanasa mimba.Sijajua mpaka leo huyo kaka/baba/babu aliyemjaza mimba ile.Habari ikaenea kijiji chote, kwamba yule mpole,mkimya kapewa mimba ukizingatia enzi hizo mimba shuleni ilikuwa bado ni janga na msamiati. Sijui yule binti alizingatia ushauri wa nani, akaamua kwenda kutoa mimba ile. Alisafiri mpaka mkoa fulani hivi ambao sasa ni jiji. Baada ya mawiki kupita, siku moja basi la kutoka mjini likamshusha akiwa amekooonda na kupauka. Waliojua dalili za kutoa mimba wakashudia kuwa ile ni habari ya kweli.

Baada ya siku chache tangu kuwasili kwake kijijini, taarifa kamili ya habari ikaenea kijijini kuwa, zoezi la utoaji mimba awali halikufanikiwa kama ilivyotarajiwa. Baada ya mtumbo kuzidi kumuuma, akapelekwa kwa wataalamu zaidi. Huko akafahamishwa kuwa sehemu ya tumbo la uzazi imeoza na kuwa ikishughulikiwa hatazaa tena. Matibabu yakakamilishwa!

Binti huyu wa pili kuzaliwa ameshaolewa mara mbili na kuachika kwa sababu ya kutoshika mimba, na jamaa za karibu wanasema amekata tamaa sana, na kama angalizo imebidi dada yake mkubwa aishi naye nyumbani kwake japo binti anaweza kujitegemea kwa kipato chake!

SWALI:
Ni kweli watu wakimya huwa ni noooma kwa mikakati ya porini?
Mbona yule binti wa kwanza pamoja na machepele yake hayakumpata haya,je kuzungumza kwake kulisaidia kupatiwa njia za kukwepa mimba?
Ni kweli kuwa wanawake wengi inawawia vigumu kuishi bila mume?
 
3. Si kweli, Mwanamke anaweza tu kuishi bila ya mume pia bila ya kufanya ngono kwa muda mrefu tofauti na wanaume.
1. Sio wote wakimya wana tabia za ajabu "mikakati ya porini", uhuni/umalaya ni tabia ya mtu.
 
Ukimya wa mtu haumzuii kufanya madudu, wala uchangamfu haumlazimishi kufanya madudu.

Pole yake, wale wanaotarajia kutoa mimba na wasome hapa kujua kwamba madhara hua hayaishii kwenye kutokua na mtoto tu. Hiyo kitu inaweza ikakufuata maisha yako yote.
 
natural law, ukiwa mpiganaji lazima unajifunza kujilinda, huyu mpole labda hakuwa na experince.
Upole na mimba au mistakes hazihusiani.

Kuishi bila mume kama inawezekana au haiwezekani inategemea na malezi na ulivyoaminishwa mume ana nafasi gani kwa mwanamke.
Sio universal law japo % kubwa mume muhimu. Ni sehemu ya kupunguzia mipresha ya maisha.
 
kuwa mkimya au mcheshi hakumfanyi mtu kufanya madudu
kunasa mimba sio kipimo cha uchakaramu, si ajabu binti wa kwaza kwa sababu ya ucheshi na kujichanganya alijua jinsi ya kujikinga na mimba kwa kuongea na watu tofautitofauti wakati mpoleeeeeeee hana wa kumfundisha au kuzungumza nae akacheza mpaka kanasa.

pili wanawake wana uwezo wa kukaa muda mrefu bila kuwa na mwanaume, inawezekana kinachomkosesha raha binti wa kwanza ni guilty, na kujua kwamba hawezi kuzaa kwa kosa alolifanya la kutoa ujauzito. anahitaji ushauri wa kisaikolojia huyo
 
Ukimya/uchangamfu siyo determinant ya tabia chafu ya mtu, tabia itabaki kuwa ni tabia.
suala la kupata mimba au kutopata kwa huyo mwingine kunategemea mambo mengi ikiwemo elimu ya kujikinga na mimba, muda wanaokutana na hao wenzi wao, uwezo wa hao wenzi wao kumpachika mimba, uwezo wa yeye kupokea mimba nk.

tunawahsuari wadada wasitoe mimba, uzazi wa siku hizi ni mgumu, mtoto ni baraka jamani, kitanda hakizai haramu!!!
 
Hapa ndio tunaona madhara ya kutoa mimba..
Kuhusu ukimya wa huyo binti, hauna uhusiano wowote na kupata au kutopata mimba.
 
Mmmh ngoja namim kunamapacha nawajua na wanatabia hzo. Ntawafuatilia kwa umakin zaidi.
 
1. kuwa mkimya sio sababu kutokufanya madogol
2.kuolewa/kuwa na mume ni heshima kwa familia na jami kwa ujumla
 
Back
Top Bottom