Binafsi Namkubali Sana Rostam Aziz na sina chuki naye!

Mkuu naunga mkono hoja yako....KATIBA mpya ndio suluhisho la haya yote yatokeayo Tanzania, ndio mwongozo wa maisha ya kila mtanzania...kelele, matusi, kashfa, mabishano, ushabiki, malumbano ya sisi kwa sisi hayatatusaidia kuinusuru nchi hii huko tunakoelekea hasa kama hatutaki kumwaga damu...tujenge hoja kwa midahalo na makongamano, tujiulize na kujadili nini kiandikwe katika katiba, nini kiachwe, adhabu gani itolewe kwa mtoa rushwa na mla rushwa (wenzetu China wananyonga hawa), mafisadi, na masuala yote yanayoihusu nchi hii. Rostam anabebwa na mapungufu na udhaifu wa katiba yetu, anatumia mwanya wa tamaa waliyonayo ndugu zetu tuliowapa dhamana ya uongozi kuitafuna nchi hii, anawahonga, anawaingiza katika biashara zake kwa kuwapa pato fulani matokeo yake wanajisahau na kumwacha mtu huyu afanye anavyotaka katika hii nchi....

Wengi wetu (watanzania) hatuna uelewa wa katiba hata tukisema ianze kuandikwa leo tutashindwa hata kutoa maoni...tuisome katiba ya sasa na tujue mapungufu yako wapi ili tuandikapo katiba mpya asitokee mtu wa kuchezea watanzania na rasilimali zetu...TUNISIA Rais kakimbilia uhamishoni lakini je hilo ndio suluhisho la kuleta maendeleo, kumuua Rostam na mtandao wake si kuua vimelea vyote vya ufisadi nchi hii, kuna watu leo tunawaona wenzetu ila kesho tukiwapa nafasi hatutoamini kama ndio hawa tuliokuwa nao jana kundini

Asante mkuu! hapo mwishoni umemalizia vizuri sana!!!
 
For your information there are so many Rostams around wengine probably wapo makini na wanachokifanya thats why hatuwajui..., I repeat I call him a thief (not stronger) lakini he is still surving sio kwa ujanja bali (because we are weaker)...., angekuwa genious mpaka leo mtoto mdogo angejua kwamba huyu jamaa ni mwizi....., that means some of deals he was making were not wisely constructed ni kwamba he is dealing na mazuzu....

Mkuu tunazi-feel hasira zako lakini kubali pia kwamba jamaa kashika karata ya turufu kiasi kwamba hata hahitaji kujificha sana anapotengeneza madili yake kwani jina lake tu linatosha kuwatia mchecheto akina mkwere, mgosi, hosea na convoy lao lote! Hata mtoto wa mkulima yuko tayari kusulubiwa kuliko kugusa mauzauza ya RA. Kwenye vikao vya CC tu utamkuta kakaa kwa mapozi huku akina mkwere jasho jembamba likiwatoka jinsi ya kushughulikia ajenda zinazomhusu!
 
Mbona unakataa na kukubali kiaina? Alichotushinda RA ndilo tatizo la nchi hii na siyo yeye. Tafakari. Chukua hatua......

Kushindana na amateurs does not make you a genious...., Its being a big fish in small pond..., na sio kwamba wananchi wameshindwa ni viongozi ndio sio mahili na kuutoa uongozi ni process its not a one days job... It took us generations kuuondoa ukoloni.., au na wenyewe walikuwa geniouses..., (lets not underestimate the word genious..... please)
 
Naomba unielimishe jinsi gani katiba mpya inatatua tatizo la rushwa nchini?
mkuu endapo itaandikwa katiba mpya ikatamka kuwa mtu yeyote atakayekutwa na hatia ya kutoa au kupokea rushwa atakuwa ametenda kosa ambalo hukumu yake ni kunyongwa hadi kufa nadhani hii itasaidia kupunguza rushwa kwa kiwango kilichopo sasa. Pia zikatungwa By-laws ambazo zitazuia au kutoa adhabu kali kwa mtu atakayepatikana na hatia ya kutoa au kupokea rushwa, hii pia itasaidia kupunguza tatizo hili
 
Mkuu tunazi-feel hasira zako lakini kubali pia kwamba jamaa kashika karata ya turufu kiasi kwamba hata hahitaji kujificha sana anapotengeneza madili yake kwani jina lake tu linatosha kuwatia mchecheto akina mkwere, mgozi, hosea na convoy lao lote! Hata mtoto wa mkulima yuko tayari kusulubiwa kuliko kugusa mauzauza ya RA. Kwenye vikao vya CC tu utamkuta kakaa kwa mapozi huku akina mkwere jasho jembamba likiwatoka jinsi ya kushughulikia ajenda zinazomhusu!
Now this makes him powerfull but not clever...? kuna watu ambao wamekula madeal makubwa ila kwa kutumia akili hawa watu watakufa and people will call them heroes.., I have got a lot of examples za kina Rostam (Mabutu, Mugabe, et al) hawa watu wameuzi watu kwa ufujaji wao na mwisho wao sio mzuri...., kumbe huyu jamaa angepata advisors akafanya deals lakini aka-share nchini na kuwekeza kwenye nyanja tofauti maybe people could have been singing a different tune right now.., Dont you think the Guys behind Rostam are the really clever ones au unadhani there is no one pulling his strings???
 
Now this makes him powerfull but not clever...? kuna watu ambao wamekula madeal makubwa ila kwa kutumia akili hawa watu watakufa and people will call them heroes.., I have got a lot of examples za kina Rostam (Mabutu, Mugabe, et al) hawa watu wameuzi watu kwa ufujaji wao na mwisho wao sio mzuri...., kumbe huyu jamaa angepata advisors akafanya deals lakini aka-share nchini na kuwekeza kwenye nyanja tofauti maybe people could have been singing a different tune right now.., Dont you think the Guys behind Rostam are the really clever ones au unadhani there is no one pulling his strings???
Mkuu Rostam ni genious!!! sana tena sana...na tunatakiwa tujifunze kupitia yeye...wapi tulipojikwaa na jamaa akatumia hiyo chance kutengeneza deal zake. Jambazi, Mwizi, Fisadi these are just trivial names with bad connotation!!! lakini lazima tuende deep tuangalie kilicho nyuma ya pazia.

Kama unapenda movie angalia ile ya jamaa mmoja ambaye baadae alikuja kuajiriwa na FBI " catch me if You can " utajua nina maanisha nini.
 
Namkubali sana Rostam ( Nasisitiza), Wana JF wengi wanaamini Rostam sio raia wa Tanzania na ana passport zaidi ya moja ( contrary to our immigration act). Iweje mgeni ( kama ni kweli) aje nchi ya watu aweze kupewa hadi wadhifa serikalini, afanye umafia wa kuteketeza uchumi wa nchi...huku ninyi wenyeji mnamuangalia??? Mtu wa aina hiyo anakuwa kashughilisha ubongo wake to the extent kwamba kaenda far beyond normal circumstances??? au wewe tafsiri yako ya mtu genious ni nini???
Mkuu pengine watu hawajakuelewa philosophy yako, kwa nilivyokusoma wewe unaweza kuwa ndio unachukia ufisadi unaoendelea katika nchi hii pengine kuliko hata hao wanaopaza sauti zao kwa sauti ya juu... wewe uko kifalsafa zaidi wakati sisi wengine tuko kihalisia, tunataka mtu asimame na kusema kuwa 'tunamchukia Rostam ndio katufikisha hapa' huyu atapigiwa makofi na kila mtu...lakini wewe unaetumia falsafa kuwaeleza kuwa mbaya si Rostam wabaya ni sisi na mfumo unaotuongoza utachukiwa na kila mtu na kuonekana msaliti, na uliyenunuliwa au unatumiwa...kujinusuru inabidi kwenda sawa na matakwa ya sisi watanzania na hakika kwa njia hii tutachelewa sana kufika.....

mkuu hoja hii ina mantiki
 
Mkuu, kama sijakosea, niseme umenikosha kwa kuleta mada kwa mtindo mbadala. Ila ujue ukigusia kumtaja Rostam kwa misingi "chanya" basi huna rafiki hapa. Lakini ukweli utabaki kwamba, "kwa upande wa pili", Rostam is a genius. Vinginenvyo, utamuelezeaje mtu anayeweza kuja na dili zinazoongoza kwa ukubwa na mikanganyiko (complexities), kisha akawafunga kamba viongozi wakuu wa nchi wa awamu tofauti tofauti; wengine wakiwa hata hawaivi pamoja; halafu akajumuisha na baadhi ya wanasiasa nyota wa upinzani na kuacha taifa zima linaumia kichwa juu yake?

Kuna mchambuzi mmoja wa kimataifa alieendesha utafiti dhidi ya wanasayansi makatili wa kijerumani enzi za Hitler - akina Wernher Von Braun na Josef Mengele walioiwezesha Marekani kuwa ya kwanza kumfikisha binadamu mwezini. Kwa jinsi walivyotesa na kuangamiza binadamu wenzao kwa njia zisizomithilika ili kufanikisha tafiti zilizotoa matokeo ya hali ya juu kabisa kisayansi, alisema: These guys were true geniuses but utterly despicable bastards! Marekani iliyomtorosha na kumwepusha Von Braun na hukumu ya Nuremberg imemjengea hata makumbusho!

Natumaini nimekusoma vyema na kumkubali kwako RA ni kwa misingi ya aina hiyo.

Huyo jamaa kwenye color alikuwa sio wa kawaida. Ni watu wenye kuweza kuangalia vitu upande wa pili kama walivyofanya wamarekani ndio walioweza kuelewa jamaa alikuwa genius.!

Nakupa credit Rich Dad kwa kuuona ukweli wa RA upande wa pili!
 
lengo lako ni zuri binafsi nimekuelewa mtazamo wako ila umejichanganya kudai kuwa unamkubali, sasa unamkubalije alafu hapo hopo unataka restructuring ya system au katiba kwa influence ya mtu kama huyo unayedai unamkubali unadhani hizo restructuring za katiba zitawezekana? pia hujajieleza unamkubalije kubalije inawezekana kabisa mimi na wadau wengine hatujakuelewa namna unavyomkubali tukabaki kukulaumu bure tu..
 
Mkuu, kama sijakosea, niseme umenikosha kwa kuleta mada kwa mtindo mbadala. Ila ujue ukigusia kumtaja Rostam kwa misingi "chanya" basi huna rafiki hapa. Lakini ukweli utabaki kwamba, "kwa upande wa pili", Rostam is a genius. Vinginenvyo, utamuelezeaje mtu anayeweza kuja na dili zinazoongoza kwa ukubwa na mikanganyiko (complexities), kisha akawafunga kamba viongozi wakuu wa nchi wa awamu tofauti tofauti; wengine wakiwa hata hawaivi pamoja; halafu akajumuisha na baadhi ya wanasiasa nyota wa upinzani na kuacha taifa zima linaumia kichwa juu yake?

Kuna mchambuzi mmoja wa kimataifa alieendesha utafiti dhidi ya wanasayansi makatili wa kijerumani enzi za Hitler - akina Wernher Von Braun na Josef Mengele walioiwezesha Marekani kuwa ya kwanza kumfikisha binadamu mwezini. Kwa jinsi walivyotesa na kuangamiza binadamu wenzao kwa njia zisizomithilika ili kufanikisha tafiti zilizotoa matokeo ya hali ya juu kabisa kisayansi, alisema: These guys were true geniuses but utterly despicable bastards! Marekani iliyomtorosha na kumwepusha Von Braun na hukumu ya Nuremberg imemjengea hata makumbusho!

Natumaini nimekusoma vyema na kumkubali kwako RA ni kwa misingi ya aina hiyo.

Mkuu nakubaliana na wewe. Nilishasema hii kitu hapa jamvini kuwa twendeni mbele turudi nyuma, Rostam ni kichwa!! Najua hapa JF watu mtapinga kutokana na huyu jamaa kuhusishwa na kila dili kubwa ambalo lina mashaka juu ya umma wa Tanzania kunufaika.

Binafsi namfananisha Rostam Aziz na kijana Kamlesh Pattni ambaye miezi michache tu baada ya kumaliza Bcom yake akiwa na miaka 24 na pamoja na kutoka kwenye very poor family aka manage kuestablish kuwa na link ya moja kwa moja na Rais Moi na viongozi wengine wakuu wa serikali na baada ya muda mfupi akawa ni bilionea wa kutupwa!! Pattni ndo alikuwa mastermind kwenye dili la Goldenberg ambalo lilivuruga kabisa uchumi wa nchi ya Kenya mwishoni mwa miaka ya 1990s!!
 
Kila mbuyu una shetani wake. Ngoma inayolia sana hupasuka. Ukiona watu wengi wanakunyooshea kidole kaa chonjo si dalili njema. Jirekebishe tu, mbona ni rahisi. Zamani nilielezwa kwamba ninapoona watu wengi sana wanazungumzia juu yangu basi nijue kuna jambo nikae chini nitafakari jinsi ya kuishi nao.
 
Kila mbuyu una shetani wake. Ngoma inayolia sana hupasuka. Ukiona watu wengi wanakunyooshea kidole kaa chonjo si dalili njema. Jirekebishe tu, mbona ni rahisi. Zamani nilielezwa kwamba ninapoona watu wengi sana wanazungumzia juu yangu basi nijue kuna jambo nikae chini nitafakari jinsi ya kuishi nao.

That is not a rule of thumb, ingekuwa hivyo watu kama kina Aristotle, akina Newton, Alebrt Einstein wasingeweza kufika mbali kwa kuhofia kupingwa. Those are cheap beliefs ...na hutaweza kushughulisha ubongo wako kufikiri outside the box kwa hofu za ajabu ajabu.
 
mkuu endapo itaandikwa katiba mpya ikatamka kuwa mtu yeyote atakayekutwa na hatia ya kutoa au kupokea rushwa atakuwa ametenda kosa ambalo hukumu yake ni kunyongwa hadi kufa nadhani hii itasaidia kupunguza rushwa kwa kiwango kilichopo sasa. Pia zikatungwa By-laws ambazo zitazuia au kutoa adhabu kali kwa mtu atakayepatikana na hatia ya kutoa au kupokea rushwa, hii pia itasaidia kupunguza tatizo hili

lakini angalia isije kumaliza matrafiki na madereva wetu na kuwaacha wahusika hii ni bongo
 
Kila siku ukiangalia mada zinazorushwa hapa JF dhidi ya Rostam Aziz zinalenga zaidi kwenye chuki. Imepelekea hadi baadhi ya watu kusahau kwamba huyu jamaa ni mwanadamu kama tulivyo sisi. Wengi wametoa proposal ya kumuua wakidhani ndo suluhu ya ufisadi hapa nchini, na wengine wamediriki kumu-associate na scandals ambazo hata hakuna proof kwamba ni jinsi gani huyu jamaa alivyo facilitate.

Binafsi naona watanzania badala ya kutibu maradhi kwa kutambua ile root cause tunakimbilia kutibu dalili (sysmptoms). Hivi hujawahi kujiuliza maswali kwamba endapo ikitokea leo hii tunapata taarifa zenye kuthibitishwa ya kwamba Rostam Aziz na washirika wake wameuwawa, Je, ndo itakuwa mwisho wa ufisadi hapa nchini??? La hasha nachelea kusema ndo itakuwa mwisho wa ufisadi hapa nchini. Hiyo itakuwa ni temporary relief na Akina Rostamu wengine wengi tu wataibuka endapo tutaendelea kubakia na mfumo dhaifu wa kiutendaji.
Binafsi ninamkubali sana huyu jamaa msomi naesikia ni graduate wa havard university na ambaye baadhi ya watanzania wanadai sio raia. Endapo itakuja kudhibitika ya kwamba the guy was behind EPA, Kagoda, Meremeta, Richmond, Dowans etc nitazidi kuwa inspired na huyu jamaa. Na mpaka sasa ninamuona huyu jamaa ni zaidi ya ma-professor wangu walionifundisha kule university, ni zaidi ya madaktari, ma-engineer,lawyers ...na ni zaidi ya wataalamu wote kwenye sector yeyote uijuayo hapa Tanzania.

The other way around ni kwamba sisi watanzania ndo tunaojiroga, haiwezekani tunaendelea kupalilia na kuumwagilia maji mfumo ambao tunaujua ni wa kishenzi kwa miaka yote huku tukiishia kusemasema pembeni bila kuchukua hatua.
Kwangu mimi Katiba ndo suluhu wa yote.

... kama wanavyofanywa waizi wenzao kule China, waizi wote style ya allegations dhidi RA wanastahili kupigwa risasi bila blindfold
... kama RA ni mwizi as per allegations changanya yeye na mfumo unaomwezesha yeye na wenzake kufanya ujambazi huo, stahili yao ni pamoja na kuwatia kwenye kontena na kuwatumbukiza kwenye kina kirefu sana cha maji baharini na kushindilia zege hiyo sehemu. wao si binadamu, si watanzania wazalendo!
... chuki dhidi ya RA ziko in tune na uoza unaofanywa naye kama allegations ni za kweli.
.... RA hajanizidi IQ. nakataa kwa hilo. sidhani kwamba kuwa daring na kukwapua mlo wa maskini ni aina flani ya ingenuity hata kidogo. ndio, mfumo uliopo ndio mwanya wa umafia unaoendelea kuwalea kina RA. wanapeta tu bila wasiwasi. kama angekuwa that smart basi ingenuity hiyo ingetumika kufanya maajabu katika nyanja zilizo halali na wazi.
... umafia wa baadhi ya watawala sio ingenuity. ni wizi tu sawasawa na udokozi wa chakula cha maskini midomoni kwao.
... ndio mfumo wa utawala Bongo umeoza. Isisahaulike kwamba hitaji la kuendelea ni pamoja na watu. watu wengi wa Bongo ni waswahili tu. mabingwa wa mineno, ni spineless kwa maana hawana ujasiri wa kusimama kidete kuondokana na mfumo wa kishenzi, lightminded kwa uharaka wa kudanganywa na sahani ya ubwabwa kisha kuuza haki zao. Takwimu za uchaguzi ulopita zinaonyesha wazi urahisi wa kudanganyika na geographic location ya jamii zao.
... aaargh!
 
Mkubwa ulifanikiwa ku graduate au uli disco?

Kwa taarifa yako sina historia ya ku-feli ( sijisifu lakini namshukuru Mungu kwa hilo)! mara kibao nimewaburuza classmates wangu wote niliosoma nao tena kwa pass mark za juu mno! mwaka wa kwanza hadi wa mwisho. Nikienda sehemu yeyote huwa najitahidi niangalie mambo kwa mtizamo wa tofauti kidogo pale inapowezekana. Hili nililo liandika sijakurupuka, nimeliona hata kwa marafiki zangu wa jirani ( bendera fuata upepo) wanatoa arguments za mambo wasiyojua background yake (shame!!!).
 
Mkuu nakubaliana na wewe. Nilishasema hii kitu hapa jamvini kuwa twendeni mbele turudi nyuma, Rostam ni kichwa!! Najua hapa JF watu mtapinga kutokana na huyu jamaa kuhusishwa na kila dili kubwa ambalo lina mashaka juu ya umma wa Tanzania kunufaika.

Binafsi namfananisha Rostam Aziz na kijana Kamlesh Pattni ambaye miezi michache tu baada ya kumaliza Bcom yake akiwa na miaka 24 na pamoja na kutoka kwenye very poor family aka manage kuestablish kuwa na link ya moja kwa moja na Rais Moi na viongozi wengine wakuu wa serikali na baada ya muda mfupi akawa ni bilionea wa kutupwa!! Pattni ndo alikuwa mastermind kwenye dili la Goldenberg ambalo lilivuruga kabisa uchumi wa nchi ya Kenya mwishoni mwa miaka ya 1990s!!

Sawa unaweza ukawa na akili sana ya ku-mastermind wizi mkubwa, ila hiyo haikufanyi uwe shujaa, nadhani hii ni kasumba ambayo imesambaa kwa watanzania kwa sasa ya kuwa-admire wezi wakubwa, hii kasumba mbaya sana na inazidi kuturudisha nyuma zaidi, just imagine rostam mwenyewe akijua kuwa kuna watanzania wanamu-admire kwa anayoyafanya atajiskiaje? tuache hii kasumba haita tufikisha popote!!! huyo mhindi uane m-admire (Kamlesh Pattni) akishuka Kibira slums alafu atembee kwa mguu unadhani nini kitamtokea?
kwa nini unashindwa ku-admire watu wanopinga ufisadi? hapo ndio napatwa na wasiwasi wa tunapoelekea, mtu anawezaje kuchukia ufisadi alafu hapo hapo eti anamsifu fisadi kwa kuiba hii haiingii akilini kabisa...
 
Unaweza kumlinganisha na Kamlesh Patni (Later baptized atsPaul) wa Kenya ambaye amehusika kwenye Goldenberg scandle ambayo bado kesi yake inanguruma.

Japo scandle ilitokea 90's, kesi ilikuja kama miaka 10 baadae. Baada ya Moi -kuachia urais.

Patni alikuwa smart, genius. Alianzisha idea ya business, Moi na wenzake wakaidaka juu kwa juu.

Msome Patni hapa kwenye blogu na uone umaskini wa wananchi unasababishwa vipi na watu wabinafsi kama hawa ma'genius'.
 
Kwa taarifa yako sina historia ya ku-feli ( sijisifu lakini namshukuru Mungu kwa hilo)! mara kibao nimewaburuza classmates wangu wote niliosoma nao tena kwa pass mark za juu mno! mwaka wa kwanza hadi wa mwisho. Nikienda sehemu yeyote huwa najitahidi niangalie mambo kwa mtizamo wa tofauti kidogo pale inapowezekana. Hili nililo liandika sijakurupuka, nimeliona hata kwa marafiki zangu wa jirani ( bendera fuata upepo) wanatoa arguments za mambo wasiyojua background yake (shame!!!).

kum-admire fisadi sio kufikiria 'outside the box' hata kidogo, unatupakaza upupu tu!!
 
Back
Top Bottom