adakiss23
JF-Expert Member
- Jan 23, 2011
- 4,474
- 4,261
http://bongostaz.blogspot.co.uk/2012/08/simba-kumkosa-mbuyu-twite-rage.html?m=1
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Rage ametoka povu na akatoa mchozi kidogo!jamani kweli mzee wa watu anaipenda Simba,duuu hapo tu anagombea mchezaji ...kazi ipo! Namshauri ajipange sawa sawa maana uchaguzi wa Tabora Mjini waja soon na anaweza asipite kwenye kura ya maoni...na pia ajipange wana Tabora wamekata tamaa na maisha yao ya kila siku,hakuna fursa za ajira vijana woote wameishia kuvuta bangi na kuwa fundi magari ingawa mkoa una shule nyingi sana za maana za sekondari ....lile wimbi la wale vijana ndio litamtesa sana pale mjini
Na mimi nimuongelee kidogo huyu BIN ZUBEIR…
Kwanza siamini kama ni mwandishi wa habari aliyehitimu na kutunukiwa kitu Fulani(either cert,dip au shahada) kwa sababu katika blog yake ameonekana ni mtu wa kuandika habari kishabiki zaidi(as if inasomwa na watu wa upande mmoja,nafananisha habari zake na habari zinazoandikwa na gazeti la UHURU,ambazo huwa zimelenga wasomaji wafuasi wa CCM na sio wananchi wote kwa ujumla)
Sina haja ya kumshauri aiandike anavyotaka kuandika….la hasha,,huyu mwandishi ana maslahi yake binafsi kwa anachokiandika na anafanya MAKUSUDI tu na bila kutafuna maneno nahisi huyu jamaa anatumiwa…..
Imefika wakati sasa sfuatilii tena blog yake kwa sababu habari zake nyingi hazina uhakika,(mfano,jana aliandika kuhusu twite kupewa dola 10000 na leo mtu huyu huyu anaandika kapewa 30000 baada ya press ya bw.Rage ya jana…uandishi wake umekaa kinazi nazi sana mpaka anaboa……
Nawashauri wale wadau wa michezo walio Neutral kama mimi…kama unahitaji habari ambazo atleast hazijakaa kishabiki,bora utembelee blog ya shaffih dauda,japokuwa sikatai kuwa nayo sio efficient for 100% lakini angalau jamaa hana ushabiki wowote katika uandishi wake……
I STAND TO BE CORRECTED. The Magnificient
Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha
Embu wadau wa michezo walio neutral kama the magnificient pateni baadhi ya habari zisizoegemea upande wowote kutoka kwa blog pendekezwa na Mdau (Blog ya TSC):-
Shaffih Dauda in Sports.: HIVI NDIVYO ADEN RAGE ALIVYOWAPIGA BAO YANGA NA KUMSAINI MBUYI TWITE
Shaffih Dauda in Sports.: SUALA LA KELVIN YONDANI KUCHEZA KAGAME NA UTATA WAKE WA KIKANUNI: IWEJE YEYE ARUHUSIWE KUCHEZA WAKATI KISIGA NA EMMANUEL GABRIEL WALIZUIWA?-
Naomba niweke hizi mbili tu kwa leo.
ok,sawa....sioni ubaya wowote hapo,au kwa kuwa amiongelea simba?
Duh!! nna mashaka sana na upeo wako wa kufikiri
Na mimi nimuongelee kidogo huyu BIN ZUBEIR
Kwanza siamini kama ni mwandishi wa habari aliyehitimu na kutunukiwa kitu Fulani(either cert,dip au shahada) kwa sababu katika blog yake ameonekana ni mtu wa kuandika habari kishabiki zaidi(as if inasomwa na watu wa upande mmoja,nafananisha habari zake na habari zinazoandikwa na gazeti la UHURU,ambazo huwa zimelenga wasomaji wafuasi wa CCM na sio wananchi wote kwa ujumla)
Sina haja ya kumshauri aiandike anavyotaka kuandika .la hasha,,huyu mwandishi ana maslahi yake binafsi kwa anachokiandika na anafanya MAKUSUDI tu na bila kutafuna maneno nahisi huyu jamaa anatumiwa ..
Imefika wakati sasa sfuatilii tena blog yake kwa sababu habari zake nyingi hazina uhakika,(mfano,jana aliandika kuhusu twite kupewa dola 10000 na leo mtu huyu huyu anaandika kapewa 30000 baada ya press ya bw.Rage ya jana uandishi wake umekaa kinazi nazi sana mpaka anaboa )
Nawashauri wale wadau wa michezo walio Neutral kama mimi kama unahitaji habari ambazo atleast hazijakaa kishabiki,bora utembelee blog ya shaffih dauda,japokuwa sikatai kuwa nayo sio efficient for 100% lakini angalau jamaa hana ushabiki wowote katika uandishi wake
I STAND TO BE CORRECTED. The Magnificient
ukisoma mfululizo wa makala yake tangu kipindi cha uchaguzi wa yanga alivyokuwa akiwanadi hasa Manji na Ben Kleb, pia alivyokuwa akiandika kuhusu Ngasa kwenda Simba na nafasi ya Azam kumchukua tena Ngasa, pia jinsi alivyokuwa wa kwanza kuandika kwamba Simba kupitia Rage walimpa Twite dola 10,000 tofauti na kauli ya Rage ya kumpa dola 30,000 na gharama zingine zinazofikia sasa Dola 39,000 na laki kadhaa, na zaidi ukifuatilia kauli ya Rage jana kuhusu kilichotokea na leo anamtaja Ridhiwani na zaidi kumshambulia Rage. Anafika mbali zaidi na kuongelea mambo ya EPA kama vile na yeye siku hizi ana uelewa wa mambo ya kisiasa tofauti na makala yake anayoandika siku zote.Utaweza kugundua kitu kimoja tu kwamba huyu jamaa Bin Zubeiry anajichanganya sana na yeye mwenyewe ndiyo anatokwa na mapovu tofauti na anavyotaka watu waamini.
Jana aliandika kwa hakika kwamba Rage au Simba walimpa Twite dola 10,000 tu na leo anakubaliana na kiasi alichotaja Rage jana cha dola 39,000, na anahitimisha kwa kuandika SAFI SANA. Pia anajenga hoja yake katika historia hafifu ya Victor Costa na sasa anasema kwamba Rage alaumiwe kwasababu gani alimuacha Twite Rwanda badala ya kuja naye moja kwa moja. Haoni sababu ya Rage kuwahi mkutano mkuu wa Simba na badala yake angerudi na Twite mkononi. Anajaribu kuonyesha kwamba kwake mkutano mkuu ilikuwa vemaifanyike bila mwenyekiti na yeye aendelee kumsubiri Twite aje naye kwasababu Yanga nao wanamfuatilia huyo mchezaji.
Bin Zubeiry inaelekea haelewi nini maana ya mkataba ambao umesainiwa kwa kuzingatia taratibu zote. Pia inaonekana haelewi ingemchukua Twite siku ngapi kukamilisha mambo yote, kwani anakuja kazini nchi nyingine, mazingira tofauti, n.k, hivyo alipaswa akaweke mambo yake sawa ikiwa ni pamoja na mambo ya familia na taratibu za safari kama hati zinazohitajika. Ndiyo maana Rage alitumia gharama zingine ya dola 9,000 nje ya dola 30,0000 alizokabidhiwa Twite ila akamilishe taratibu zote na aje ajumuike na wenzake Dar. Huyu mwandishi hawezi kutuhaminisha kwamba hilo ni kosa kwa Simba wakati tayari mchezaji ameingia mkataba na klabu na ameshapewa haki yake.
Bin Zubeiry haonyeshi uelewa hata kidogo kuhusu taratibu za kiuhamisho na mambo ya mkataba, ndiyo maana anaonekana kuunga mkono uhuni uliofanywa na Yanga, na hapa nashawishika kwamba hawezi kufanya hivi parsonal attack kwa Rage na zaidi fuatilia makala yake siku zote kuhusu Simba utaona kwamba ana maslahi binafsi katika haya yanayofanywa na viongozi wa Yanga. Kama ni makosa Rage kumuacha Rwanda kama anavyotaka tuamini, basi ni kwanini hao yanga anaowafagilia nao bado wamemuacha huko huko na hawajamleta Tanzania?
Katika sakata hili, naweza nikaona hatari zaidi kwa huyu mchezaji, japo yeye kwa akili yake na tamaa zake binafsi na kwa kudanganywa na viongozi wa Yanga hakuweza kuona hilo. Huyo mchezaji anawafanyia Simba Uhuni kiasi hicho na bado anakuja kufanya kazi Tanzania, tena Dar es Salaam, sipati picha kuhusu hali ya ulinzi atakaopewa na klabu yake mpya ya Yanga kwa kipindi chote cha mkataba wake na mazingira atakayoishi, na kwa msingi huo Yanga watalazimika kutumia gharama kubwa sana. Na uhakika wa hizo pesa chafu za viongozi au mtoto wa kigogo ambaye kwa hakika simjui, nahisi hauko mbali sana, kwani mwaka 2015 kuna mabadiliko makubwa sana na hakika Tanzania itaanza historia mpya na hata wahujumu uchumi waanze kujiandaa kwenda THE HAGUE.