Wana-JF,
Baada ya majuzi tu kuwa na makala iliyoandikwa zaidi ikimdhalilisha mwenyekiti wa Simba S.C, ndugu Aden Rage, na pia kuwa na mifululizo ya habari za kuikashfu Simba hasa Viongozi wake mara simba wamewapigia magoti viongozi wa Azam kuhusu Redondo, na baada ya muda mfupi huyo huyo anaibuka tena kwenye blog yake ya Bin Zubeiry na kukanusha habari hizo anazoziandika mwenyewe, leo tena kuna makala kaiandika tena na hasa akimshambulia benchi la ufundi la Simba chini ya Maestro. ebu som amwenyewe na hasa kwenye alama nyekundu hapo chini. Swali moja najiuliza na sijapata jibu lake, kwamba kuna nini kati ya viongozi au klabu ya Simba na huyu Bin Zubeiry?
Na Mahmoud Zubeiry
KATIKA Simba Day, Agosti 8, mwaka huu Simba SC ilitangaza usajili na kuonyesha jezi za wachezaji zikiwa na majina mgongoni kupitia screen kubwa la Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam- lakini wakati dirisha la usajili linafungwa leo saa 6:00 usiku, klabu hiyo inatarajiwa kufanyia editing video ya Simba Day.
Katika Simba Day, ilionekana jezi ya Mbuyu Twite, Danny Mrwanda na Kanu Mbivayanga, lakini hivyo ni vipande ambavyo leo vinatolewa na kuingizwa vipande vipya kama vya picha za Paschal Ochieng kutoka AFC Leopard ya Kenya na Daniel Akuffo kutoka Hearts Of Oak ya Ghana.
Simba imelazimika kurekebisha usajili wake dakika za mwishoni, baada ya kugundua mapungufu makubwa, yaliyotokana na ushauri mbaya wa Kamati yake dhaifu ya Ufundi, inayoongozwa na Mwenyekiti asiye na uzoefu wala ujuzi wa kuendana na hadhi ya klabu hiyo, Ibrahim Masoud Maestro.
Katika marekebisho hayo, Simba imewatema beki Lino Masombo na kiungo Mbivayanga kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ili kuwasajili Ochieng na Akuffo. Lakini pia, Simba imemtema Mrwanda wakati habari zaidi zinasema kuna wachezaji wengine watatu, wawili kutoka Mali na mwingine mmoja kutoka Ivory Coast, miongoni mwao wanaweza kusajiliwa.
Mapema jana, ilielezwa kiungo Mganda, Mussa Mudde angetemwa, lakini baadaye ikaelezwa huyo hataaachwa tena, badala yake wanasubiriwa wachezaji kutoka Mali na Ivory Coast waonekane, kisha walinganishwe na Ochieng kabla ya klabu kuamua imsajili nani.
Simba ina kutwa moja tu hadi saa 6:00 usiku wa leo kuhakikisha inakamilisha usajili wake, tayari kwa msimu mpya wa Ligi Kuu, wao wakiwa mabingwa watetezi.
Source: Bin Zubeiry blogpot.com
Baada ya majuzi tu kuwa na makala iliyoandikwa zaidi ikimdhalilisha mwenyekiti wa Simba S.C, ndugu Aden Rage, na pia kuwa na mifululizo ya habari za kuikashfu Simba hasa Viongozi wake mara simba wamewapigia magoti viongozi wa Azam kuhusu Redondo, na baada ya muda mfupi huyo huyo anaibuka tena kwenye blog yake ya Bin Zubeiry na kukanusha habari hizo anazoziandika mwenyewe, leo tena kuna makala kaiandika tena na hasa akimshambulia benchi la ufundi la Simba chini ya Maestro. ebu som amwenyewe na hasa kwenye alama nyekundu hapo chini. Swali moja najiuliza na sijapata jibu lake, kwamba kuna nini kati ya viongozi au klabu ya Simba na huyu Bin Zubeiry?
Na Mahmoud Zubeiry
KATIKA Simba Day, Agosti 8, mwaka huu Simba SC ilitangaza usajili na kuonyesha jezi za wachezaji zikiwa na majina mgongoni kupitia screen kubwa la Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam- lakini wakati dirisha la usajili linafungwa leo saa 6:00 usiku, klabu hiyo inatarajiwa kufanyia editing video ya Simba Day.
Katika Simba Day, ilionekana jezi ya Mbuyu Twite, Danny Mrwanda na Kanu Mbivayanga, lakini hivyo ni vipande ambavyo leo vinatolewa na kuingizwa vipande vipya kama vya picha za Paschal Ochieng kutoka AFC Leopard ya Kenya na Daniel Akuffo kutoka Hearts Of Oak ya Ghana.
Simba imelazimika kurekebisha usajili wake dakika za mwishoni, baada ya kugundua mapungufu makubwa, yaliyotokana na ushauri mbaya wa Kamati yake dhaifu ya Ufundi, inayoongozwa na Mwenyekiti asiye na uzoefu wala ujuzi wa kuendana na hadhi ya klabu hiyo, Ibrahim Masoud Maestro.
Katika marekebisho hayo, Simba imewatema beki Lino Masombo na kiungo Mbivayanga kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ili kuwasajili Ochieng na Akuffo. Lakini pia, Simba imemtema Mrwanda wakati habari zaidi zinasema kuna wachezaji wengine watatu, wawili kutoka Mali na mwingine mmoja kutoka Ivory Coast, miongoni mwao wanaweza kusajiliwa.
Mapema jana, ilielezwa kiungo Mganda, Mussa Mudde angetemwa, lakini baadaye ikaelezwa huyo hataaachwa tena, badala yake wanasubiriwa wachezaji kutoka Mali na Ivory Coast waonekane, kisha walinganishwe na Ochieng kabla ya klabu kuamua imsajili nani.
Simba ina kutwa moja tu hadi saa 6:00 usiku wa leo kuhakikisha inakamilisha usajili wake, tayari kwa msimu mpya wa Ligi Kuu, wao wakiwa mabingwa watetezi.
Source: Bin Zubeiry blogpot.com