Bima ya afya imekuwa inajitanua kila siku ila kwa bahati mbaya huduma zake kwa baadhi yetu ni mbaya sana. Yaani ni sawa na wizi wa mchana. Tunakatwa hela kwenye mishara yetu lakini hatupati huduma. Ukienda hospitali uaambiwa ukanunue dawa au kipimo hiki lipia. Kwa hiyo wengine tumeshindwa na tumeamua kukata tamaa na kujilipia bila kujali kwamba tuna bima, vitambulisho tulivyo navyo ni ushahidi tu wa wizi wa NHIF.
Hata hivyo kwa jinsi nchi yetu ilivyo wakati wa kuwa na kitu kama bima ya afya ulikuwa haujafika, ufisadi na kutokuwajibika ni kwa hali ya juu sana. Hili linanifanya nihisi kwamba hata aliyebuni na kuanzisha mfumo huu hapa nchini ni fisadi papa na lengo lake ni yeye kunufaika binafsi. Na ndio maana sasa bima ya afya badala ya kuboresha huduma zake imegeuka na kuwa chombo cha kudhamini mambo yasiyo na faida kwa wachangiaji.
Ningependa kujitoa kwenye bima ya afya hata hivi leo. Kama kuna anayejua utaratibu wa kujitoa aniaambie kwani atakuwa ameniepusha na ubarazuli wa kunufaisha kundi la wanaokula bila kunawa.
Hata hivyo kwa jinsi nchi yetu ilivyo wakati wa kuwa na kitu kama bima ya afya ulikuwa haujafika, ufisadi na kutokuwajibika ni kwa hali ya juu sana. Hili linanifanya nihisi kwamba hata aliyebuni na kuanzisha mfumo huu hapa nchini ni fisadi papa na lengo lake ni yeye kunufaika binafsi. Na ndio maana sasa bima ya afya badala ya kuboresha huduma zake imegeuka na kuwa chombo cha kudhamini mambo yasiyo na faida kwa wachangiaji.
Ningependa kujitoa kwenye bima ya afya hata hivi leo. Kama kuna anayejua utaratibu wa kujitoa aniaambie kwani atakuwa ameniepusha na ubarazuli wa kunufaisha kundi la wanaokula bila kunawa.