Jatropha
JF-Expert Member
- Apr 9, 2009
- 1,151
- 199
Ndugu wana bodi,
Kwa muda mrefu sasa umekuwepo upotoshaji wa madai ya madaktari kwa lengo la kutaka kuwaaminisha wananchi kuwa madaktari wanapigania maslahi yao pekee. Jana Dr Chitage wa Jumuia ya Madakatari alitoa ufafanuzi mzuri katika taarifa ya habari kuwa katika vikao 6 vilivyofanyika baina ya madaktari na Serikali, 66% ya muda huo ulitumika kujadili namna Serikali itakavyoboresha sekta ya afya ikiwemo kuzifanyia hospitali zote hapa nchini ukarabati na kuzipatia vifaa vya tiba. Alitoa mfano kuwa katika madai yao madaktari walikuwa wakitaka kila hospitali ya wilaya ipatiwe mtambo wa X-ray, na akaenda mbali zaidi kwa kudai kuwa hivi tunavyozungumza hakuna hata hospitali hata moja ya umma ikiwemo Muhimbili yenye mtambo wa CT Scan.
Kwa kuwa juzi Mhe Raisi Jakaya Kikwete akihutubia taifa alidai kuwa Serikali haina uwezo wa kifedha wa kutekeleza madaia ya madakatari, kwa hakika taarifa hizi za madakatari zimenifikirisha sana hasa kizingatiwa kauli ya Mtukufu Rais. Kwa hakika nilijiuliza maswali mengi sana Je ni kweli Tanzania ni nchi maskini kama Rasi anavyotaka wananchi tuamini?
Ili kuzitendea haki pande zote mbili yaani Seikali inayodai haina uwezo wa kifedha kutekeleza madai ya madakatari; na madakatari wanaotaka kila hospitali ya wilaya ipatiwe mtambo wa X-ray pamoja na vifa vingine vya tiba niliamua kutazama upya vipaumbele vyeti kama taifa ili niweze kuunga mkono mdaia ya bRaisi Jakaya Kikwete kuwa Tanzania ni nchi maskini; ama kuwaunga mkono madaktari kuwa Seikali inao uwezo wa kutekeleza madai yao ikiwemo kuboreshwa maradafu kwa sekta ya afya ikiwemo kuboreshwa kwa miundo mbinu, mupatikanaji wa madawa na maslahi ya watumishi wa sekya ya afya.
Katika kufanya hilo nilikumbuka hivi karibuni takribani miezi 6 iliyopita Serikali lilitumia takribani Bilioni 27.5 katika kuadhimisha sherehe za miaka 50 ya uhuru. kwa kuzingatia kuwa moja ya madaia ya madakatari ni kuwa kila hospiatalia katika ngazi ya wilaya ipatiwe mtambo wa X-ray kwa ajili ya uchunguzi wa wagonjwa. Kabla ya kuanzisha kwa mikoa mipya Tanznaia inakadiriwa kuwa wilaya 128. Hivyo niliingia katika mtandao na kutafuta bei ya mtambo mmoja wa X-ray na kugundua mtambo wa kisasa kabisa wa X-ray ni sawa na Dola 140,000 tu. Hivyo Bilioni 27.5 zilizotumika katika maadhimisho ya miaka 50m ya uhuru zingeweza kununua miatambo 125 kama hiyo pichani hapo chini.
Kwa namna yoyoite ile kiwango kilichotumiwqa na Serikali inyoongozwa na Raisi Jakaya Kikwete miezi 6 iliyopita cha Bilioni 27.5 kwa maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru ni kikubwa mn. Hivyo sio sahihi kabisa kwa nchi inayoweza kutumia kiasi hiki cha fedha kwa sherhe tuu kudai kuwa ni nchi maskini. Kwa hakika ningewelewa zaidi Mhe Raisi Jakaya Kikwete kama kabla ya kufanya matumizi haya ya anasa angelihutubia taifa na kutuambia kuwa kutokana na uwezo mdogo wa kifedha wa Serikali ya Tanzania, nchi yetu itaadhimisha sherehe za miaka 50 ya uhuru kimya kimya lakini fedha zilizotengwa kwa ajili ya sherehe hizo kiasi cha Bilioni 27.5 zitatumika kununulia mitambo mipya ya X-ray ya kisasa kwa ajili ya hospitali za ngazi ya wilaya 125.
Ndugu wanjf naomba tujiulize kwa kina ni nini athari za huu wimbo wa kila siku wa viongozi wetu hususan kutoka CCM kuwa sisi watanzania tu watu maskini na nchi yetu Tanzania ni maskini?
Picha ya hapo chini ni moja ya mtambo wa kisasa wa X-ray unaoweza kununuliwa kwa Dola 140,000 tu Philips Diagnost 94 Remote Control System
Kwa muda mrefu sasa umekuwepo upotoshaji wa madai ya madaktari kwa lengo la kutaka kuwaaminisha wananchi kuwa madaktari wanapigania maslahi yao pekee. Jana Dr Chitage wa Jumuia ya Madakatari alitoa ufafanuzi mzuri katika taarifa ya habari kuwa katika vikao 6 vilivyofanyika baina ya madaktari na Serikali, 66% ya muda huo ulitumika kujadili namna Serikali itakavyoboresha sekta ya afya ikiwemo kuzifanyia hospitali zote hapa nchini ukarabati na kuzipatia vifaa vya tiba. Alitoa mfano kuwa katika madai yao madaktari walikuwa wakitaka kila hospitali ya wilaya ipatiwe mtambo wa X-ray, na akaenda mbali zaidi kwa kudai kuwa hivi tunavyozungumza hakuna hata hospitali hata moja ya umma ikiwemo Muhimbili yenye mtambo wa CT Scan.
Kwa kuwa juzi Mhe Raisi Jakaya Kikwete akihutubia taifa alidai kuwa Serikali haina uwezo wa kifedha wa kutekeleza madaia ya madakatari, kwa hakika taarifa hizi za madakatari zimenifikirisha sana hasa kizingatiwa kauli ya Mtukufu Rais. Kwa hakika nilijiuliza maswali mengi sana Je ni kweli Tanzania ni nchi maskini kama Rasi anavyotaka wananchi tuamini?
Ili kuzitendea haki pande zote mbili yaani Seikali inayodai haina uwezo wa kifedha kutekeleza madai ya madakatari; na madakatari wanaotaka kila hospitali ya wilaya ipatiwe mtambo wa X-ray pamoja na vifa vingine vya tiba niliamua kutazama upya vipaumbele vyeti kama taifa ili niweze kuunga mkono mdaia ya bRaisi Jakaya Kikwete kuwa Tanzania ni nchi maskini; ama kuwaunga mkono madaktari kuwa Seikali inao uwezo wa kutekeleza madai yao ikiwemo kuboreshwa maradafu kwa sekta ya afya ikiwemo kuboreshwa kwa miundo mbinu, mupatikanaji wa madawa na maslahi ya watumishi wa sekya ya afya.
Katika kufanya hilo nilikumbuka hivi karibuni takribani miezi 6 iliyopita Serikali lilitumia takribani Bilioni 27.5 katika kuadhimisha sherehe za miaka 50 ya uhuru. kwa kuzingatia kuwa moja ya madaia ya madakatari ni kuwa kila hospiatalia katika ngazi ya wilaya ipatiwe mtambo wa X-ray kwa ajili ya uchunguzi wa wagonjwa. Kabla ya kuanzisha kwa mikoa mipya Tanznaia inakadiriwa kuwa wilaya 128. Hivyo niliingia katika mtandao na kutafuta bei ya mtambo mmoja wa X-ray na kugundua mtambo wa kisasa kabisa wa X-ray ni sawa na Dola 140,000 tu. Hivyo Bilioni 27.5 zilizotumika katika maadhimisho ya miaka 50m ya uhuru zingeweza kununua miatambo 125 kama hiyo pichani hapo chini.
Kwa namna yoyoite ile kiwango kilichotumiwqa na Serikali inyoongozwa na Raisi Jakaya Kikwete miezi 6 iliyopita cha Bilioni 27.5 kwa maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru ni kikubwa mn. Hivyo sio sahihi kabisa kwa nchi inayoweza kutumia kiasi hiki cha fedha kwa sherhe tuu kudai kuwa ni nchi maskini. Kwa hakika ningewelewa zaidi Mhe Raisi Jakaya Kikwete kama kabla ya kufanya matumizi haya ya anasa angelihutubia taifa na kutuambia kuwa kutokana na uwezo mdogo wa kifedha wa Serikali ya Tanzania, nchi yetu itaadhimisha sherehe za miaka 50 ya uhuru kimya kimya lakini fedha zilizotengwa kwa ajili ya sherehe hizo kiasi cha Bilioni 27.5 zitatumika kununulia mitambo mipya ya X-ray ya kisasa kwa ajili ya hospitali za ngazi ya wilaya 125.
Dola kwa kila mtambo mmoja wa wa Xray | Kiwango cha kubadili Dola kwa Tz Shs | Jumla ya Shilingi za Kitanzania zinzohitajika kununua mtamo mmoja wa X-ray | Kiasi cha fedha zilizotumika katika Sherehe za miaka 50 ya Uhuru Tar 09 Desemba 2011 | Mitambo ya X-ray ya kisasa ambayo ingeweza kununuliwa na fedha hizo |
140,000 | 1,570 | 219,800,000 | 27,500,000,000 | 125 |
Ndugu wanjf naomba tujiulize kwa kina ni nini athari za huu wimbo wa kila siku wa viongozi wetu hususan kutoka CCM kuwa sisi watanzania tu watu maskini na nchi yetu Tanzania ni maskini?
Picha ya hapo chini ni moja ya mtambo wa kisasa wa X-ray unaoweza kununuliwa kwa Dola 140,000 tu Philips Diagnost 94 Remote Control System