Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Kuna mama mmoja jirani yangu ambaye siku hizi tabasamu halimtoki mdomoni...............nilipomwuuliza hizi nderemo ni za nini jibu alilonipa liliniacha kinywa wazi nikapigwa na butwaa..........................akaniambia jeuri yake sasa kwisha.....................nilipomwuuliza nani huyo akasema si huyu mzee wake sasa "vijisenti" hana na amekuwa na kauli nzuri na hana dharau tena............akaniambia sasa hivi ni muungwana sana.........na akaongeza kashika adabu na Mungu ni mkubwa.......sala zake Mwenyezi Mungu amezisikiliza............na ya kuwa mumewe sasa anahangaika kutafuta ugali wa watoto wake bila zengwe.............Ama kwa hakika kumbe "vijisenti" tunavipenda lakini kumbe vyaweza kuleta mtafaruku ndani ya familia........................lol