Bila safari taifa halitaendelea?

kalikumtima

Member
Aug 13, 2009
45
0
Jameni, mkuu wa kaya JK anasema safari zake za nje hazina mbadala? je ni kweli kuwa bila hizi safari za nje Tanzania kama taifa haliwezi kuendelea? je ni kweli kama taifa tunafaidika na hizi safari? Je hizi safari za nje ndio suruhisho la matatizo ya Tanzania kama taifa?
Au hizi safari ni kwa maslahi binafsi ya JK na hivyo kwake hazina mbadala?
Kama si kwa maslahi binafsi ya JK , hatuwezi kuwatumia viongezi wetu wengine km mawaziri na Mabarozi kutusaidia ktk hili? Naomba tuelimishane jamani.


“Na wiki chache zijazo ninatarajia kwenda nchini Denmark kuhudhuria mkutano wa Capenhagen.” [JK]
source: http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=16520
 
Tungekuwa na time frame kama taifa kwamba utendaji kazi wa rais unafanyiwa tathmini baada ya muda fulani ingetusaidia sana. Na suala hapa sio safari za nje peke yake bali utendaji mzima. Tuamini kwa suala la safari za nje ana washauri wa kutosha na huwa wanashauriana kabla hajapanga safari.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Kuna mikutano mingine inahusisha Heads of States...hii hakuna jinsi ataacha kuhudhuria na ni kweli haina mbadala.Kama huu wa Copenhage ni moja ya aina hiyo ya mikutano.
Sina hakika na ziara kama alizofanya Cuba, Trinidad & Tobago na kumalizia America.
 
Kuna mikutano mingine inahusisha Heads of States...hii hakuna jinsi ataacha kuhudhuria na ni kweli haina mbadala.Kama huu wa Copenhage ni moja ya aina hiyo ya mikutano.
Sina hakika na ziara kama alizofanya Cuba, Trinidad & Tobago na kumalizia America.

VC

Tatizo au uzuri, siku hizi wachache wameenda shule kwa hiyo hawadanganyiki kirahisi kwa mambo ambayo yako wazi. Hivi unataka kuniambia nchi wanachama wa UN 190 na ushee..wote watakwenda Copenhagen? After all ni Kikwete huyu huyu chini ya uongozi wake wa AU waliteua kamati ya kuiwakilisha/kuisemea Africa ikiongozwa na Zenawi. SASA YEYE ANAENDA KUFANYA NINI? Kuwakilisha maslahi ya Tanzania? yapi? Well, I have nothing against his trip....after all Copenhagen is more appealing than Bongo...I am just against huu uongo wa jinsi gani viongozi wetu wanatufanya wajinga kama vile shule hatukwenda.

Na hakika mtaniambia..matokeo ya Copenhagen..waafrika wanaenda huko kulia lia tuu na kutembeza bakuli....Sema tuu ni kwa sababu na wazungu wana interests na hii climate change otherwise...I dont see them getting involved.

Climate change kwa sasa imekuwa priority/deal Africa kwa sababu viongozi wetu wanajua hapa kuna pesa ya bure itakayoletwa na wazungu...(wonder if there is pesa ya bure in this world anyway).itakayoishia mifukoni mwao. Ukweli ni kwamba Africa....kama ni njaa, ukame na matatizo mengineyo..yameanza zama hizoo....unakumbuka njaa iliyoua maelfu huko Ethiopia? Infact mpaka leo tunakufa kwa njaa...ila kwa sababu mzungu kesha penyeza rupia..leo tunasema njaa imesababishwa na climate change.....wakati njaa tumekuwa nayo miaka nenda rudi...

I wonder kama iko siku waafrika tutaanza kufikiria.

Masanja
 
Back
Top Bottom