Kalumbesa
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 1,013
- 356
Tanzania tumekuwa tukijivua amani kwa miaka mingi sana na hadi leo licha ya viongozi wetu kuonyesha dhahiri akili zao zimefika mwisho wa kufikiri yaliyo na amani na kuanza kutumia njia za utawala wa vitisho,ubabe mpaka kudiriki kuua wananchi au kutoa watu uhai ki rahisi tu, wengi wetu wanaona amani tuliyo nayo itaendelea kudumu tu..Mimi naona Taifa linaelekea kubaya.Serikali yoyote ile ikishindwa kuliongoza vema Taifa,hutaka kuendelea kubaki madarakani kwa njia zote hasa wizi wa kura na mtutu wa bunduki..Haya yameanza kujitokeza Tanzania na yana ishara mbaya sana huko tuendako...Binafsi naona hata huu mwaka tulio nao unaweza usiishe bila matukio makubwa ya kulitingisha Taifa...ili Taifa hili liweze kuondokana na balaa lililo mbele,inabidi tutoe kafara..na anayestahili kutolewa kafara ili kulinusuru Taifa ni CCM..Ni jukumu letu sote wananchi kulitambua hili mapema na kuwa tayari kulikamilisha wakati utakapokua muafaka...Nimalizie kwa kusema....Kama CCM angekuwa mtu tena mwanangu basi ningemtoa kafara fasta ili kulinusuru Taifa