Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 6,376
- 6,720
Hakuna kitu kinachonikera kama baadhi ya waandishi hasa wale wasiokwenda shule vilivyo kupenda kutumia neno Dakta Jakaya Kikwete, Dakta Karume na sasa nimesoma kwenye blog ya vuvuzela aitwaye michuzi akiandika Dakta Jaka Mwambi. Je hii inatokana na ufinyu au ukosefu wa elimu wahusika au kujikomba kwa wahusika? Je inakuwaje wanaoitwa madaktari wakati si chochote si lolote nao wanapenda sifa za uongo? Ningependa sana kusoma Kanali Kikwete kuliko Dakta Kikwete kwa vile ukanali ndio aliosotea hata kama ni kinamna.