Bila kuandika Dr Kikwete, Karume na sasa hata Jaka mwambi ujumbe haufiki?

Father of All

JF-Expert Member
Feb 26, 2012
6,376
6,720
Hakuna kitu kinachonikera kama baadhi ya waandishi hasa wale wasiokwenda shule vilivyo kupenda kutumia neno Dakta Jakaya Kikwete, Dakta Karume na sasa nimesoma kwenye blog ya vuvuzela aitwaye michuzi akiandika Dakta Jaka Mwambi. Je hii inatokana na ufinyu au ukosefu wa elimu wahusika au kujikomba kwa wahusika? Je inakuwaje wanaoitwa madaktari wakati si chochote si lolote nao wanapenda sifa za uongo? Ningependa sana kusoma Kanali Kikwete kuliko Dakta Kikwete kwa vile ukanali ndio aliosotea hata kama ni kinamna.
 
Tatizo ni bongo la waandishi kuingiliwa na virus wa kujikomba. Kama wangekuwa makini Cheo cha Urais ni kikubwa kupita heshima zote, kwa maana kuingiza neno Dr (PHD) ni kwa namna nyingine ni dhalilisho. Marais wangi huandikwa kwa kutangulisha Rais cheo ambacho ni juu ya heshima zote katika nchi na duniani. Waandishi na wanablog wengi ufikiri wao umefikia kikomo hapo kufikiria DR ndio cheo cha juu kumbe Mwenyekiti wa Kijiji ni juu ya Dr kwani mtaani anapoishi mwenye elimu ya PHD yuko chini ya huyo mwenyekiti wa serikali ya mtaa. Rais wa nchi je?

Dr. ni kitambulisho cha kiwango cha elimu yake katika mazingira ya majukumu (carrier) yake, lakini si kitambulisho cha Heshima ya cheo ambacho hakitokani na kiwango cha elimu. Rais hachaguliwi kwa kuangalia kiwango cha elimu ingawa elimu ni moja ya vigezo vya kuangaliwa upeo wake wa uongozi. Kinachoelendelea na waandishi wa habari na baadhi ya mablogers ni kumpaka mafuta Rais Kikwete kwa mgongo wa chupa. Na labda wamegundua Kikwete mwenyewe anapenda hivyo basi wameamua kujipendekeza hivyo.
 
Sasa wewe kwa akili yako finyu unawalaumu wanaowaita jk na karume madokta badala ya kulaumu vyuo vilivyowatunuku hizo PHD!! Kama chuo kinachotambulika kimemtunuku mtu PHD kwa nn watu wasitumie hiyo title? Kama unahoja jenga kwa waliotunuku sio wanaotumia title!
 
Hii kitu ya udaktari ni namna mojawapo ya kuongeza umaarufu mf: Baba Riz alipogundua atakayeshindana naye ni Dr (w kusomea) akaenda kutunukiwa U-Dokta w heshima BAADA tu y uchaguzi hilo jina halisikiki sana.TBC walikuwa hawarushi habari wkti wa uchaguzi kumhusu jamaa bila kutumia Dokta LAKINI cha kushangaza siku hizi wanamwita tu jina lake bila hiyo cheo! Kama alivyosema Songoro, wakulaumu ni VYUO vinavyotunuku hizo PhD z heshima LAKINI naamini hilo linakuwa shinikizo na sio ombi kwa vyuo vinavyotunuku
 
Ni kweli unachosema lakini naomba nikutaarifu Jaka Mwambi amegraduate 2011 PHD na si kama hao wengine.
Hakuna kitu kinachonikera kama baadhi ya waandishi hasa wale wasiokwenda shule vilivyo kupenda kutumia neno Dakta Jakaya Kikwete, Dakta Karume na sasa nimesoma kwenye blog ya vuvuzela aitwaye michuzi akiandika Dakta Jaka Mwambi. Je hii inatokana na ufinyu au ukosefu wa elimu wahusika au kujikomba kwa wahusika? Je inakuwaje wanaoitwa madaktari wakati si chochote si lolote nao wanapenda sifa za uongo? Ningependa sana kusoma Kanali Kikwete kuliko Dakta Kikwete kwa vile ukanali ndio aliosotea hata kama ni kinamna.
 
Mie sina ugomvi na vyuo kutoa shahada za heshima, kwa mfano, kwa Kikwete na Karume. Ugomvi wangu ni matumizi mabaya ya heshima husika. Mbona Mwalimu Nyerere na Mkapa walitunikiwa shahada nyingi za PhD lakini hawakuzitumia? Kwa vile walikwenda shule, walijua madhara na maana ya shahada husika. Ni kutojua au kujifanya kutojua kutetea uovu huu hasa wakati huu ambapo tuna mawaziri wengi waliozighushi bila kushughukiwa. Tunaipeleka wapi nchi na taaluma kwa ujumla kama watu wasio na taaluma kama michuzi watatuamria kutukana na kudhalilisha taaluma?
 
Hii kitu ya udaktari ni namna mojawapo ya kuongeza umaarufu mf: Baba Riz alipogundua atakayeshindana naye ni Dr (w kusomea) akaenda kutunukiwa U-Dokta w heshima BAADA tu y uchaguzi hilo jina halisikiki sana.TBC walikuwa hawarushi habari wkti wa uchaguzi kumhusu jamaa bila kutumia Dokta LAKINI cha kushangaza siku hizi wanamwita tu jina lake bila hiyo cheo! Kama alivyosema Songoro, wakulaumu ni VYUO vinavyotunuku hizo PhD z heshima LAKINI naamini hilo linakuwa shinikizo na sio ombi kwa vyuo vinavyotunuku

Huyo unae dai dr wa kusomea ambae PHD yake ina utata mtupu.PHD ya kusomea bila hata kupita ngazi km Bachelor Degree yoyote MISIFA TUUU! Hana tofauti na prof MALENGA MATALI
 
Back
Top Bottom