Rumishaeli
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 227
- 72
Walimu 300 wasotea mishahara ya Nov | Send to a friend |
Daniel Mjema,Moshi ZAIDI ya walimu 300 katika Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, hawajalipwa mishahara yao ya mwezi uliopita.Habari zilizolifikia Mwananchi jana zilisema kwa kawaida walimu hao walipaswa kupata mishahara yao kati ya Novemba 28 na 30. Hata hivyo walimu waliopiga simu katika gazeti hili, walilalamikia usumbufu kila wanapokwenda benki na hawaelezwi kiini hasa ni nini cha tatizo hilo ni nini. Habari hizo zilisema walimu walioathiriwa na tatizo hilo ni wale wanaopokea mishahara yao kupitia Benki ya NBC. Tumekwenda benki zaidi ya mara 20 tunaambulia patupu tukiuliza tunaambiwa tumuulize mwajiri wetu tunashindwa kuelewa nini kimetokea,alisema mmoja wa walimu hao. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Bernedetta Kinabo, alikiri kuwapo kwa tatizo hilo na kwamba linafanyiwa kazi kwa uzito mkubwa. Ni kweli kwamba walimu 300 hawajapata mishahara yao, kuna makosa yamefanyika na tumeshawasiliana na benki ili tuyarekebishe,alisema. Kinabo aliwataka walimu hao kuvuta subira kwa sababu tayari tatizo limejulikana na linarekebishwa haraka ili waweze kupata mishahara yao katika kipindi kifupi kijacho. Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) katika Manispaa ya Moshi, Abdalah Kaumba, alisema tatizo lipo kati ya Benki za NBC na NMB. Kaumba alisema halmashauri ilitekeleza wajibu wake wa kupeleka hundi ya mishahara kupitia NMB lakini kuna tatizo katika kuhamishia fedha benki nyingine. SOURCE MWANANCHI Wednesday, 14 December 2011 20:17 |