Biharamulo: Kampeni, kura na matokeo!

Mukasa aliyezaliwa Julai 1970, ni mtoto wa tano kati ya 10 katika familia ya Mzee William Mukasa na Mama Apolonia Mukasa. Alizaliwa katika kijiji cha Rukaragata kilichopo takriban kilometa tatu kutoka mji Biharamulo, barabara ya kwenda wilayani Ngara.

Baba yake ni mtumishi wa umma mstaafu ambaye amewahi kuwa Ofisa Afya wa wilaya ya Biharamulo kati ya mwaka 1977 na mwaka 1987 kabla ya kuwa Ofisa Afya wa mkoa wa Kagera kati ya mwaka 1987 na 1992 alipostaafu kwa mujibu wa sheria. Kabla ya hapo, aliwahi kuwa mtumishi wa umma sehemu mbalimbali nchini.
Niliwahi kuuliza hivi - Mukasa/Rwegasira - One and the same ? na nikauliza kulikoni ? Rekodi zote za nyuma zinaonyesha kuwa mhusika amejulikana kwa maisha yake toka utotoni kama Oscar Mukasa. Hata hivyo baada ya kuteuliwa tu, ghafla jina lilibadilishwa na kuwa Oscar Rwegasira baada ya majadiliano makali ndani ya CCM. Jina Mukasa linajulikana kama jina la Kiganda - yanikumbusha jamaa moja kwa jina la Omari kutoka Kenya alivyoweza kujipenyeza hadi kufikia uongozi wa juu kwenye Chama cha kandanda Tanzania, FAT. Wakati huo, enzi za chama kimoja, wagombea walikuwa wanapitishwa na vikao vilivyojumuisha CCM.

Tarehe 6/6/2009 nilikuwa na haya ya kusema -
Hata hivyo nauliza kitu kimoja, inaonekana kuna jitihada za kulizika jina Mukasa ingawaje mwanzoni tuliambiwa na washikaji wake kuwa anaitwa Oscar Mukasa na sasa ni Oscar Rwegasira. Je kuna kitu kinafichwa ?
Jaji Makame hata hili atalifumbia macho- ndio maana yuko pale.
 
Jamani hivi akina Jaji Makame wakanyamaza, mimi mwana biharamulo au mtanzania wa mtwara huku naruhusiwa kwenda mahakamani kumzuia?
 
Mgombea wa CCM Biharamulo awekewa pingamizi

Na Frederick Katulanda, Mwanza


WAKATI kampezi za uchaguzi mdogo wa kiti cha ubunge katika Jimbo la Biharamulo Magharibi zikiwa zimeanza, mgombea wa CCM katika kinyang’anyiro hicho, Oscar Rwegasira, amewekewa pingamizi kwa madai kuwa si raia wa Tanzania .


Habari kutoka Biharamulo na ambazo zimethibitishwa na Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, Zuberi Mbyana, zilisema pingamizi hilo limewekwa na mgombea wa Chadema Dk. Anthony Mbassa.


Mgombea huyo wa CCM, aliteuliwa baada ya kuwashinda wapinzani wake katika kura za maoni kwa kupata kura 309.


Walioshindwa katika hatua hiyo ni na kura zao katika mabano ni, Agricola Magotto (120), Mwajemi Mustapha (23), Hassan Rwabudongo (15), Mussa Matata (10) na Nitibihora Burchard (5).


Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Mbyana alikiri kupokea pingamizi hilo na kwamba tayari ofisi yake imekwishamwandikia mgombea wa CCM, kumtaka kujibu pingamizi hilo.


Alisema katika pingamizi hilo, mgombea wa Chadema anadai kuwa mgombea wa CCM, hana sifa za kuwania nafasi hiyo kwa sababu si raia wa Tanzania.


Alisema kwa mujibu wa mweka pingamizi, mgombea wa CCM ni raia wa Uganda na kwamba wazazi wake wote wa wawili walitoka Uganda.


Msimamizi huyo alisema mgombea huyo wa Chadema anadai kuwa wazazi wa mgombea mwenzake, hawajawahi kuomba uraia hapa nchini.


“Barua tuliyomwandikia mgombea wa CCM ni yenye kumbukumbu namba BBC/30/3/Vol. X/114 ya Juni 10, 2009 ambayo nimemtaka ajibu tuhuma za pingamizi alilowekewa na Chadema” alisema msimamizi huyo.



Mkuu wa operesheni ya uchaguzi wa Chadema, John Mrema, alisema katika pingamizi hilo, Chadema wamebaini kuwa mgombea wa CCM, ameshindwa kueleza mahali alikozaliwa.


“Baada ya kubaini hilo na kufuatilia uhamiaji na kwingineko, wamebaini kwamba wazazi wake mgombea huyo walingia nchini mwaka 1971 wakitokea Bunyoro nchini Uganda na kuishi eneo la Misenyi,” alidai Mrema.


Alidai kuwa mgombea huyo wa CCM, alizaliwa Uganda mwaka 1970 na si katika kijiji cha Rukalagata Biharamulo kama anavyodai.

Source:Mwananchi



My take: Je pingamizi kama hili hawezi kuwekewa RA kwenye uchaguzi wa mwaka kesho? kama uhamiaji wanaweza kueleza data hizo basi hata kwa RA
inawezekana.
 
Tafadhali mwenye picha ya Mukasa a.ka.. Rwegarira wa Oscar aiweke hapa. Nina kumbukumbu ya majina yote mawili niliwahi kusoma na wanayofanana nayo kitambo.
 
Tafadhali mwenye picha ya Mukasa a.ka.. Rwegarira wa Oscar aiweke hapa. Nina kumbukumbu ya majina yote mawili niliwahi kusoma na wanayofanana nayo kitambo.

Huyu alisoma pale Nyakato Sec. School 1985-1988 tulikaa naye Bweni Moja linaitwa Balamba alikuwa amenitangulia darasa moja.
Headmaster: Kajumulo
Konya, Luhiye (Mukafiri), Vulva, etc
 

Attachments

  • ~GE144.jpg
    ~GE144.jpg
    147.6 KB · Views: 69
  • oscar.jpg
    oscar.jpg
    3.9 KB · Views: 73
Kwa kiasi fulani naifahamu hii familia ya Mzee William Mukassa. Nimesoma na Benard Mukassa, Stella Mukassa pale B’mulo shule ya msingi. Kwa ufupi ni familia yenye malezi bora, ya kidini na watoto wenye akili za kuzaliwa.

Nakumbuka Benard akiwa dalasa la saba alikuwa akiwafundisha walimu hesabu na lugha. Miongoni mwao ni Mwalimu Kinyange ( huyu alikuwa mrundi).

Kuhusu uraia, suala la kutoka Uganda halina ubishi hata kidogo. Familia hii ilitufanya watoto wa B’mulo na Umoja P/S ku-draw two stereotype conclusions:

One: kila mtu mweusi sana ni mganda (Maana Mukassa’s wengi ni weusi)
Two: Waganda ni watu wenye akili sana (Akina Benard walishikiria no. 1 toka std 1-7)

Na kuna ndg yao mmoja aliletwa toka UG na kujiunga B’mulo p/s. Alikuwa akiitwa something like Manfredy na alimwita Mzee W.Mukassa Baba mkubwa. Huyu jamaa alikuwa na umri mkubwa sana ukilinganisha na wanadalasa wenziwe. Kama ada “watu weusi ni waganda na waganda wana akili sana” jamaa kichwani alikuwa safi. Baada ya muda fulani kina Mwl. Bwahama (M/Mkuu) wakampitisha kuwa kilanja. Manfredy alikuwa mkorofi sana kiasi kwamba alimpiga mwalimu akapotea mtaani.

Awali niliposikia kuteuliwa kwa Oscar, akili ilikwenda mbio kumkumbuka Manfredy na kuwaza hizo stereotypes zetu enzi hizo. Kwa bahati mbaya nilikuwa polini ambako hardly niliweza kusoma post za JF. Hivyo nikashindwa kuwapa haka ka-dot..

My question:
Kama tunaweza ku-connect the dots na kupata facts au mwangaza kwa mtoto wa B'mulo kwa nini hatupati dots kwa mtoto wa Igunga?
 
Mzee Mwanakijiji,

Kutumia jina la Rwegasira badala ya Mukassa huenda ikawa kwasababu za ukabila. Kuna maeneo ambayo bila kutumia majina ya huko basi wewe sio mmoja wao. Kama kule kwetu wengine watu wengi shuleni walitumia majina ya baba zao yaani bila kuweka majina ya ukoo lakini wakiingia kwenye siasa lazima watumie majina ya ukoo yaani yale yanayoanzia na Mwa...

Wacha tusubiri tuone hilo pingamizi litaishia wapi. Ila kama ni kweli sio raia basi jamaa naye atakuwa kilaza kama yule jamaa wa CHADEMA. kabla hata ya kufikiria kugombea ubunge angehakikisha anayaweka sawa mambo yake ya uraia. Watu kama hao ambao wamezaliwa TZ na kukulia TZ ni raia ila tu ili kulinda sheria zetu inabidi wahalalishe uraia wao.
 

My question:
Kama tunaweza ku-connect the dots na kupata facts au mwangaza kwa mtoto wa B'mulo kwa nini hatupati dots kwa mtoto wa Igunga?


kengeleeeee nggggrrrrrrrrr!!!

Alipofariki mzee Mazula muda mfupi tu JF ikaanza kujazwa na facts za watu waliosoma naye enzi hizo na waliowafahamu watoto wake na ndugu zake wengi. Leo huyu Oscar katajwa tu watu wametoka "porini" na kuja na taarifa ambazo mtu mwingine ambaye anajua si za kweli anaweza kuzipinga lakini ni data ambazo zinasimama zenyewe. Alisoma wapi, alihamia kutoka wapi, na walimu wake na wanafunzi wengine walikuwa kina nani.

Nina uhakika hata majina ya mitaani yanajulikana.

LInapokuja suala la RA, habari zake ni sifuri.
 
ALIKOTOKA


Mukasa aliyezaliwa Julai 1970, ni mtoto wa tano kati ya 10 katika familia ya Mzee William Mukasa na Mama Apolonia Mukasa. Alizaliwa katika kijiji cha Rukaragata kilichopo takriban kilometa tatu kutoka mji Biharamulo, barabara ya kwenda wilayani Ngara.
Baba yake ni mtumishi wa umma mstaafu ambaye amewahi kuwa Ofisa Afya wa wilaya ya Biharamulo kati ya mwaka 1977 na mwaka 1987 kabla ya kuwa Ofisa Afya wa mkoa wa Kagera kati ya mwaka 1987 na 1992 alipostaafu kwa mujibu wa sheria. Kabla ya hapo, aliwahi kuwa mtumishi wa umma sehemu mbalimbali nchini.


Alipata elimu ya msingi katika shule ya msingi Biharamulo kuanzia mwaka 1978 mpaka 1984 na baada ya hapo alichaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari katika shule ya Nyakato iliyopo nje kidogo ya mji wa Bukoba.

Mwaka 1989 alichaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano na cha sita katika shule ya sekondari ya Pugu, Dar es Salaam katika masomo ya Fizikia, Kemia na Hisabati.


Mwaka 1991/1992, alitumikia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria katika kambi za Ruvu mkoani Pwani na Maramba, Tanga.


Baada ya hapo, mwaka 1993 alijiunga na Chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa masomo ya shahada ya kwanza ya sayansi katika hisabati na takwimu.


Hakuishia hapo kwani baada ya kufanya kazi kwa muda katika Kituo cha Utafiti na Maendeleo ya Afya cha Ifakara, alikwenda Uholanzi kwa masomo ya shahada ya uzamili ya sayansi katika Teknolojia ya Mawasiliano na Habari katika tiba (MSc in Medical Informatics) kwenye Taasisi ya Sayansi za Afya. Alihitimu shahada hiyo mwaka 2001.
Hivi sasa ni mwanafunzi wa masomo ya shahada ya uzamivu katika teknolojia ya habari na mawasiliani kwenye fani ya afya katika chuo kikuu cha Basel, Uswisi.


Mfumo wa masomo anayosomea ni ya mazoezi ya vitendo na ukusanyaji wa takwimu kwa ajili ya masomo. Alisema mfumo huo unamwezesha mwanafunzi kuendelea na kazi pia na unatoa nafasi ya kuoanisha masomo ya nadharia na vitendo.


Licha ya kuwa mtaalamu aliyebobea katika fani ya TEKNOHAMA, Mukasa ni kijana mwenye uelewa mpana kutokana na bahati aliyoipata katika kutembelea sehemu mbalimbali duniani.


Baadhi ya nchi alizotembelea kutokana na masomo, warsha na ziara za kikazi ni ndani na nje ya bara la Afrika, Kenya, Uganda, Ghana, Afrika ya Kusini, Uholanzi, Scotland, Uingereza, Ethiopia, Canada, Italia, Uswisi na Vietnam.


Vile vile amekwishafanya machapisho ya kisayansi 10 na kuongoza, kusimamaia, au kuandika miradi takriban 13 ya kitaalamu iliyostahili na kupata ufadhili mkubwa wa fedha.
Mukasa hayuko mbali sana kijamii kwani ni mjumbe wa kamati ya usimamizi na tathmini ya masuala ya kitaalamu ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Vile vile ni mwakilishi wa umoja wa kimataifa wa wanataaluma wa sayansi na teknolojia ya habari na mawasilino katika afya kanda ya Tanzania.

Hatua aliyoichukua Mukasa ni ya kuigwa na vijana wengine wa Tanzania waliobahatika kupata elimu. Changamoto kwa vijana na wasomi wengine nchini ni kushiriki kikamilifu katika kutatua matatizo yanayozikabili jamii kwa kuwa na wao ni sehemu ya matatizo hayo.
 
Watu kama hao ambao wamezaliwa TZ na kukulia TZ ni raia ila tu ili kulinda sheria zetu inabidi wahalalishe uraia wao.

hapana, hata kama wamezaliwa Tanzania na na kukulia Tanzania hakuwafanyi kuwa raia, kwani raia ni legal concept. Siyo suala la kuzaliwa, kuzungumza lugha au kuishi tu mahali fulani. Hivyo, mtu hawezi "kuhalalisha" uraia wake; anaweza kuhalalisha ukazi wake kwa kuwa raia. Hivyo, kama siyo raia basi Oscar siyo raia na hivyo atatakiwa kufuata sheria zilizofuatwa na kina Jenerali na wengine kupata uraia wa TAnzanai.

Lakini zaidi kama ni raia, ni muhimu kuweza kujibu ili swali ili isije kutokea tena uko mbeleni kwamba baada ya uchaguzi watu wakakata rufaa juu ya uraia wake kama alivyofanyiwa Premji.

Na ni vizuri kama ulivyosema kuhakikisha hawa wagombea kutengeneza mambo yao kabla ya kujitokeza kugombea nafasi ya uongozi.
 
ALIKOTOKA

1. Mukasa aliyezaliwa Julai 1970, ni mtoto wa tano kati ya 10 katika familia ya Mzee William Mukasa na Mama Apolonia Mukasa.
Alizaliwa katika kijiji cha Rukaragata kilichopo takriban kilometa tatu kutoka mji Biharamulo, barabara ya kwenda wilayani Ngara.

2. Baba yake ni mtumishi wa umma mstaafu ambaye amewahi kuwa Ofisa Afya wa wilaya ya Biharamulo kati ya mwaka 1977 na mwaka 1987 kabla ya kuwa Ofisa Afya wa mkoa wa Kagera kati ya mwaka 1987 na 1992 alipostaafu kwa mujibu wa sheria. Kabla ya hapo, aliwahi kuwa mtumishi wa umma sehemu mbalimbali nchini.

3. Alipata elimu ya msingi katika shule ya msingi Biharamulo kuanzia mwaka 1978 mpaka 1984 na baada ya hapo alichaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari katika shule ya Nyakato iliyopo nje kidogo ya mji wa Bukoba.

4. Mwaka 1989 alichaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano na cha sita katika shule ya sekondari ya Pugu, Dar es Salaam katika masomo ya Fizikia, Kemia na Hisabati.


5. Mwaka 1991/1992, alitumikia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria katika kambi za Ruvu mkoani Pwani na Maramba, Tanga.
Baada ya hapo, mwaka 1993 alijiunga na Chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa masomo ya shahada ya kwanza ya sayansi katika hisabati na takwimu.

6. Hakuishia hapo kwani baada ya kufanya kazi kwa muda katika Kituo cha Utafiti na Maendeleo ya Afya cha Ifakara, alikwenda Uholanzi kwa masomo ya shahada ya uzamili ya sayansi katika Teknolojia ya Mawasiliano na Habari katika tiba (MSc in Medical Informatics) kwenye Taasisi ya Sayansi za Afya. Alihitimu shahada hiyo mwaka 2001.

7. Hivi sasa ni mwanafunzi wa masomo ya shahada ya uzamivu katika teknolojia ya habari na mawasiliani kwenye fani ya afya katika chuo kikuu cha Basel, Uswisi.

.

- Eti wakuu hii ni CV ya mtu asiyekua raia wa Tanzania? Yaani mzazi wake alifikia mpaka kuwa ofisa wa serikali yetu huku akiwa sio raia wetu? Na huyu kijana yote haya ameyafanya huku akiwa sio raia wetu?

I am missing something or what?

Respect.

FMEs!
 
FMES,

Tatizo hapo linaweza kuwa uraia wa baba au mama yake. Huenda alipofikisha miaka 18 alitakiwa kujaza form ya kuukana uraia wa baba au mama yake.

Hii sheria ndio inaliza watu wengi na Watanzania mnaoishi nje, huko mbele angalieni maana wanenu watakuja kulizwa na hii sheria.
 
FMES,

Tatizo hapo linaweza kuwa uraia wa baba au mama yake. Huenda alipofikisha miaka 18 alitakiwa kujaza form ya kuukana uraia wa baba au mama yake.

Hii sheria ndio inaliza watu wengi na Watanzania mnaoishi nje, huko mbele angalieni maana wanenu watakuja kulizwa na hii sheria.

- Sasa baba yake alifikiaje kufanya kazi kwenye serikali yetu mpaka kuwa ofisa wa juu huko wilayani na mkoani bila kua raia wetu? It does not add up!

Respect.

FMEs!
 
- Sasa baba yake alifikiaje kufanya kazi kwenye serikali yetu mpaka kuwa ofisa wa juu huko wilayani na mkoani bila kua raia wetu? It does not add up!

Respect.

FMEs!


Mkuu FME, wamshangaa huyo kwani RA mbona amefika hapo alipo uraia wake je? Tanzania haijaanza kuliwa leo hasa na wageni toka nchi jirani hao ndo kabisaa!
 
Back
Top Bottom