Big joke from TFF

Kabengwe

JF-Expert Member
Oct 20, 2009
240
47
Timu ya taifa ya Tanzania inatazamia kupambana na Ivory Coast siku ya Jumatatu wakati Ivory Coast wakijiandaa kwa safari yao ya kwenda Angola kwenye mashindano ya kombe la mataifa huru ya Africa. Ivory Coast watakaa nchi kwa siku sita ambapo Jumatano watapambana na Rwanda

Kwangu huu ni utani, ni bora tuwakaribishe Uganda waje kucheza na hawa jamaa hiyo Jumatatu, na hiyo Jumatano wacheze na Rwanda!

Naamini timu yetu ya taifa haiwezi kuwafunga Ivory Coast ambayo itakuja na mastaa wao wanaocheza Ulaya akiwamo Drogba, Kalou, Toure, Eboue Dindane na Bamba.

Kwa kiwango tulichokionesha Kenya kwenye mashindano ya Chalenji sidhani kama TFF wanatazamia mechi hii kuwa na ushindani zaidi ya kujipatia mapato kwa kwenda kuwaona kina Drogba! Naamin hata kama wangesema Uganda na Ivory Coast watachezea uwanja wa taifa, tungeenda tu kuangalia, kuliko kwenda kupokea hicho kipigo kilicho mbele yetu!

Bringing Ivory Coast at this point is a big joke as we are not going to learn anything from this game rather than hating Maximo and our team more.
 
Back
Top Bottom