ariflardhi
Member
- Mar 4, 2013
- 10
- 6
Kwa utotoaji wa kuku wa kienyeji kwa uhakika tumia incubator za kutoka brinsea uk ambazo zinapatikana golden ball tanzania ltd mkabala na wizara ya mifugo .
Pole sana kwa kweli kuwaweka na mama zao inasaidia joto ila kuna risk kupata magonjwa kubwa sana, kifupi hawa wakubwa wakifika umri fulani wanakuwa wamepata immunity ya magonjwa mengi ingawa wanakuwa na vijidudu kwenye damu, au choo ila hayawadhuru tatizo ikitokea hawa vifaranga wamekutana na vinyesi vya wakubwa tu uambukizo kwao unakuwa ni ugonjwa. Hii inatokea kwa hata kuchanganya vyombo vya maji, ku share banda au kwa miguu ya watunzaji toka nje au banda hili kwenda hili. Ndo maana kuhofia hilo kuna wengine wanashauri kuanzia wiki ya pili hata kama hawaumwi wapewe Amprolium dose ndogo huwakinga na ugonjwa wa coccidiosis, ingawa sina uzoefu na hawa wa kienyeji ila hii ni kwa wa kisasa tumekuwa tukifanya hivyo ukichelewa na hasa kama uambukizo ukitokea inabidi watibiwe. Kutokana na dalili zako naweka hapa dalili kutoka kitabuni lakini nakushauri jieleze vizuri pharmacy wataelewa ni ugonjwa gani
Ugonjwa Dalili za Ugonjwa Kinga/Tiba
Kuharisha damu (Coccidiosis)
Kuzubaa
Kushusha mabawa kama
mtu aliyevaa koti.
Kupoteza hamu ya kula.
Kuharisha kinyesi chenyerangi ya kahawia au kilichochanganyika na damu.
Kuharisha damu
Manyoya kutimka
Kupauka kwa upanga na ndevu
Kudhoofika na hatimaye huwezakufa.
Tiba:
Ugonjwa huo unawezakutibika kwa amprolium, salfa na ESb3 kama hatua
za kuudhibitizitachukuliwa mapema
Kinga kuepuka unyevunyevukatika matandiko.
Kuwatenga kuku wanaoonyeshadalili za ugonjwa.
Kinga kwa kutumia coccidiostat.
Kutibu kwa kufuataushauri wa wataalam wa mifugo.
My take, wakati tunasubiri ushauri wa wengine nakushauri ondoa maranda au uchafu wowote bandani, ukitibu watibie kuku wote, kila yakilowa maranda ondoa weka mengine jitahidi kuwasogeza hata wagonjwa kwenye dawa, mwaka jana mie iliwapata broiler walichanganya vyombo vyao na hawa chotara wakubwa, ukijitahidi wanapona hasa vile hawa ni kienyeji wako strong. All the best
Kwa utotoaji wa kuku wa kienyeji kwa uhakika tumia incubator za kutoka brinsea uk ambazo zinapatikana golden ball tanzania ltd mkabala na wizara ya mifugo .
Mama timmy, pole na kupata tabu ya kutengeneza funza.mimi nilikuwa natumia mbolea ile ile ya kuku na pumba za mahindi.kuna dumu la lita 20 nimelikata juu kote uwa naanza kuweka bolea kama nusu na juu na weka pumba nusu ya kiwango cha mbolea nilichoweka.Baada ya hapo namwangia maji hadi kunalowana kabisa, nafanya zoezi la kumwagia maji kwa siku 2 halafu siku ya 3 simwagii then siku ya 4 unakuta funza wameshapatikana wa kutosha naewapa kuku.Njia nyingine ambayo ina gharama kidogo ni ya kutumia pumba na utumbo au nyama zile ambazo hazifai kuliwa.unachanganya hizo nyama au utumbo na pumba halafu unamwagia maji kiasi hadi vilowane kwa siku 3 hadi 5.Karibu.
mama timmy mimi si mgeni sana hapa jf.Huwa si comment chochote nachukuwa tu maujuzi.Ila nimeona nitoe mchango wangu kwa hili.Tafuta kinyesi cha ng'ombe cha tumboni (inabidi upate aliyechinjwa) jaza kinyesi kwenye mfuko wa rambo,funga mfuko vizuri,chimba shimo,fukia na uache kwa muda wa week 1 then fukua utakuta funza wakubwa sana. n.b. Nimeelekezwa sijajaribu.Ndugu zangu mimi ninapata tabu sana ninapotaka kuwatengenezea kuku wangu funza au mchwa kwani bado sijaelewa vizuri namna ya kuwatengeneza hawa wadudu.naomba mwenye ujuzi huo anipige msasa kidogo.
Pole sana mkuu LiverpoolFC , hii kazi ni ngumu sana lakini tutafika tu, matatizo yangu kama yako.
Nami nasikitika sana kuku wangu wametotoa vifaranga wachache sana mmoja katotoa vifaranga 2 kati ya mayai 12, wapili katotoa vifaranga 4 kati ya 12 watatu katotoa naye 4 kati ya 12, sijajua tatizo ni nini, maana niliwasubirisha ili waatamie mayai kwa wakati mmoja, lakini ilichukua muda wa siku 4 wote wakawa wanaatamia siku ya tano nikawawekea mayai 12 kila mmoja. Maotokeo ndo hayo, ila mmoja bado anaatamia nategeme week ijayo naye atotoe yeye sikumsubirisha na wala sikuyatoa mayai yake kama wale wengine , ngoja nisubiri matokeo.
Jambo jingine naona kuna ugonjwa bado unasumbua kuku, vinyoya vimepata ugonjwa kama vitatu vimeshakufa, na kimoja bado kinaendelea kuugua. nimevipa madawa mpaka navionea huruma. pia kuna mmoja kati ya hao wakubwa naye kinyesi chake ni cha kuharisha damu, huyu nimemuoana leo asubuhi, mpaka sasa niko njia panda yaani nafikiria niwamalize kuku wote nianze upya kabisa. Inaweza kuwa ni sababu yakutotoa mayai machache.
Ngoja nijaribu kwanza dawa aliyopendekeza Mama Joe, au kama anaushauri mwingine atumwagie tafadhari.
Poleni sana wadau ila tusonge mbele, Kubota asante kwa pongezi. Niliona umetaja tiba mbadala nyingi je mafua ya kuku yanayo kinga au tiba unayoifahamu?
Mheshimiwa Guta pole kwa kuuguza na kupotelewa kinyoya. Naona tatizo lako linafanana na LiverpoolFC nadhani fanyia kazi kwanza ushauri wa Mama Joe, kuhusu tatizo la kutotoa inategemea lishe, jogoo, urefu wa muda unaohifadhi mayai, mazingira unayohifadhi mayai kabla hujawawekea kuku na pilika pilika za kwenye viota wakati wa kuatamia labda kuku hawatulii shauri ya kufukuzana kwenye viota au shauri ya chawa n.k. Je hali halisi ikoje, hebu dadavua.
ata mm nina mpango huo lakin nimeweka budget ya min incubator ya mayai60 ni dola kama mia2 ivi ila uhakika wa umeme ndio shida.