Mkuu Chasha hiyo ni breaking news kwenye industry ya kuku! Hao kuku uliosema huo utagaji ni super!
Kusema ukweli kwa upande wangu hadi sasa kuku wa Malawi a.k.a kuku wa kienyeji ndiyo wamekuwa wakishikilia rekodi ya mayai 80 kwa mwaka! Mimi binafsi sijawahi kufuatilia kiukweli idadi ya utagaji kwa mwaka bali matokeo ya utafiti wa kuku wa kienyeji yanaonyesha kuwa kuku anaenyang'anywa vifaranga baada ya kutotoa huwa na mizunguko 6 ya utagaji kwa mwaka hapo ni mayai 60 hadi 70. Kwa utaratibu wa kutotolesha kwa mashine tukichukulia kuwa kuku akimaliza kutaga mzunguko mmoja unayachukua mayai yake yote asipate kuatamia atakaa siku 10 kabla hajaanza kutaga upya mzunguko mwingine. Kwa hiyo siku 10 za kupumzika kutaga ukijumlisha na siku 15 za kutaga mayai 13 (maana hatagi kila siku) ni jumla ya siku 25 yaani ni karibia mwezi mmoja! Kwa wastani tunaweza kuchukulia kuku wa kienyeji mtagaji mzuri kila mwezi utaokota mayai 13 (wastani) zidisha kwa miezi 12 ni sawa na mayai 156! Ingawa inahitajika kutafiti ili kupata idadi halisi ya mayai ya kuku wa kienyeji kwa mwaka ninaimani idadi haiwezi kucheza mbali sana na hapo maana kuku wa kienyeji tuliowazoea huwa wanapumzika siku kadhaa baada ya kumaliza mzunguko mmoja kabla hawajaanza tena kutaga.

Kwa maneno mafupi ni kwamba hao kuku wa Kenya wanaotaga mayai 280 kwa mwaka utagaji huo kwa kuku wa kienyeji kiwango ni cha juu sana. Kiwango cha utagaji wa kuku wa mayai kwa mwaka kinachokubalika ili kupata faida nadhani ni zaidi ya mayai 300 (watatusaidia wataalam wa mifugo). Kuku asiyefikia idadi hiyo hakubaliki kama kuku wa mayai.

Mkuu nafuatilia na Baada ya Uchaguzi naweza Tia Timu Huko kwa ajili ya Kununua Vifaranga wake na nitaarifu, Ila tatzio linakuja kwenye kuwavusha make nasiki ni lazima upewe kibali na wizara ya Mifugo na wizara zetu zilivyo na urasimu si dhani, Ila naweza fanya kila njia kuwavusha Namanga Boda
 
Mkuu nafuatilia na Baada ya Uchaguzi naweza Tia Timu Huko kwa ajili ya Kununua Vifaranga wake na nitaarifu, Ila tatzio linakuja kwenye kuwavusha make nasiki ni lazima upewe kibali na wizara ya Mifugo na wizara zetu zilivyo na urasimu si dhani, Ila naweza fanya kila njia kuwavusha Namanga Boda

Fanya hivyo mkuu kikubwa uwapo njiani kwenda Kenya, ukifika mpakani ulizia wenyewe wanaweza kukupa ujanja, unajua hizi njaa zetu saa zingine ukijua jinsi ya kuzifanyia kazi mbona utaipenda TZ. Halafu yale mayai yaliyotishiaga soko la Dar kwani yalikuwa yanapitaje? Lianzishe mkuu wangu, nakutakia mafanikio mema.
 
Kha ha ha ha ha ha ha ha haaaaa! Humu ndiyo Jamiiforums bana!

guta umesikia onyo toka kwa ticha?

Tushindane sasa! Kubota hiyo chick marsh sijui kama nitapata ya kupima kweli! Ngoja majaliwa niwaulize walengwa wenyewe!


Mama Joe nashukuru sana kwa kuokoa jahazi kwa majibu yako kwa mdau. Yaani unajua ninavyobimbilika na magogo yangu huko porini nachelewa kujibu hoja. Kwa kweli udumu sana maana bila hivyo LiverpoolFC karibu atakuja kunitoa kwenye matanulu yangu. LiverpoolFC ukitaka kuja huku uwe makini usije ukanaswa na mitego, huku kuna miradi mingi.
 
Last edited by a moderator:
Kha ha ha ha ha ha ha ha haaaaa! Humu ndiyo Jamiiforums bana!

guta umesikia onyo toka kwa ticha?

Tushindane sasa! Kubota hiyo chick marsh sijui kama nitapata ya kupima kweli! Ngoja majaliwa niwaulize walengwa wenyewe!
LiverpoolFC , hapa kuna maticha we acha tu. nawafuatilia kwa karibu sana, chick mash ya kupima inapatikana mimi nimeinunu hiyo. na hata vifaranga wa mwanzo nilitumia ya kupima mpaka wakakua, changamoto niliyo nayo ni magonjwa. vifaranga wale wakubwa kama watatu hivi wanaumwa nimewatenga walikuwa wanavaa mikoti nikawapa miarobaini wakachangamka kwa muda wa siku mbili tatu sijui dozi haikukolea, jana naona kamoja kamezidiwa tena. nitaweka picha yake.
 
Last edited by a moderator:
Hongera kwa kupata vifaranga nakushauri uwatenge na kuku wengine kama hutaweza waache na mama yao wawape joto. anza kama alivyoshauriwa LiverpoolFC jana ila nenda na dalili hizo za jogoo famasi wakupe dawa. Mtenge pekee na osha vyombo kwa dawa. Ungeanza na mdondo kama unawasiwasi na dawa nyingine za vifaranga utapewa famasi. Keep it up

Thanks, nilikwenda famasi wamenipatia dawa leo nimeanza kumpata. ila nina vifaranga wakubwa wawiki sita naona nao wanasinzia niliwapa muarobaini kama ulivyoelekeza walipokuwa wanashusha mabawa, walichangamka lakini tena wameanza kusinzia.
 
Mkuu Guta hapo umecheza vizuri sana kuongea kwa picha, hongera kutotolesha, sasa wewe na LiverpoolFC ndiyo muanzishe kutekeleza kwa vitendo mliyoona yanawafaa kwenye hii thread, endeleeni kutoa mshindo nyuma. Guta huyo jogoo kama ulishamrambisha dawa ya mdonde wewe usihofu huyo ni kuku wa kienyeji tena ni jogoo, kama anapata fursa ya kuchunga majani hiyo itapita tu, huo uharo mbona ni kawaida tu, hofu kwa kuku wa kienyeji mkuu iko kwenye vifaranga na VINYOYA! Picha zinaongea maneno alfu moja kuliko kuandika, asante sana kuturushia picha!

nashukuru mkuu Kubota kwa kunitoa hofu. chanjo ya mdondo niliwapa, hofu yangu nyingine ni vinyoya vinasinasinzia sana.
 

Attachments

  • IMG-20130301-00190.jpg
    IMG-20130301-00190.jpg
    110.3 KB · Views: 488
guta Mi kitendo hiki cha picha inanishinda kubandika hapa kabisa na ningependa sana nibandike picha kadha wa kadha ila ndiyo hivyo na natumia N73.


nashukuru mkuu Kubota kwa kunitoa hofu. chanjo ya mdondo niliwapa, hofu yangu nyingine ni vinyoya vinasinasinzia sana.
 
Last edited by a moderator:
kwanza niwashukuru wadau wote mliochangia ktk uzi huu ulianzishwa na kubota kiukweli nimepata elimu kubwa sana kuhusu industry hii ya ufugaji wa kuku wa asili.

kumekuwa na imani fulani inayo aminika kuwa kuna baadhi ya mambo ili yafanikiwe yanategemea ngekewa alimaharufu kama MKONO MZURI pia katika swala la ufugaji wa kuku inaaminika ili uwe na kuku wengi inategemeana na mkono wako yaani inamaana kwamba kuna watu wana ngekewa/bahati na kuna watu kamwe hawawezi kuwa na idadi kubwa ya kuku,hii inaaminika kuwa Mungu anahusika na upendeleo wa kalama hii.Kwa mfano kuna ndugu yangu mmoja akipanda pilipilihoho hazikui lakini akimwita mtu mwingine ampandie ktk hiyo hiyo bustani yake kinachotokea hoho ustawi na kutoa matunda.JE,HII PIA INAWEZA IKAWA CHANGAMOTO NYINGINE KTK UFUGAJI WA KUKU?Asante.
 
Kubota Duh! Uko cha wapi Kamanda wetu?

Kuna usalama huko ulipo?
Ama tanuru limeiva tayari!
Tuzungukie hata huku Kamanda wangu!
 
Last edited by a moderator:
Kubota
Mama Joe
guta
Mama timmy

Hebu litazameni hili lililonipata jana baada ya Mi nikiwa Safari niliporudi nikakuta kuku mmoja mtetea amekufa ndani ya banda na hata hakuonyesha dalili yoyote na leo nikajaribu kutafuta watalaam nikakuta leo ni siku ya mapumziko na nipo nikachukua maamuzi ya kuzika.

Je? Kwenu haya yanatokeaga? Na hata nimejaribu kumpigia guta RETI na bila ya mafanikio baada ya simu zao kutopokelewa.

NAOMBENI USHAURI WENU WANDUGU!

Asanteni sana!
 
Last edited by a moderator:
kwanza niwashukuru wadau wote mliochangia ktk uzi huu ulianzishwa na kubota kiukweli nimepata elimu kubwa sana kuhusu industry hii ya ufugaji wa kuku wa asili.

kumekuwa na imani fulani inayo aminika kuwa kuna baadhi ya mambo ili yafanikiwe yanategemea ngekewa alimaharufu kama MKONO MZURI pia katika swala la ufugaji wa kuku inaaminika ili uwe na kuku wengi inategemeana na mkono wako yaani inamaana kwamba kuna watu wana ngekewa/bahati na kuna watu kamwe hawawezi kuwa na idadi kubwa ya kuku,hii inaaminika kuwa Mungu anahusika na upendeleo wa kalama hii.Kwa mfano kuna ndugu yangu mmoja akipanda pilipilihoho hazikui lakini akimwita mtu mwingine ampandie ktk hiyo hiyo bustani yake kinachotokea hoho ustawi na kutoa matunda.JE,HII PIA INAWEZA IKAWA CHANGAMOTO NYINGINE KTK UFUGAJI WA KUKU?Asante.

Mkuu chama2chawa: Umeleta hoja ngumu na pana sana kuweza kuielezea kwa utoshelevu ikaweza kukidhi haja. Ni hoja inayoweza kuzua malumbano yasiyoisha kiasi cha kuharibu uelekeo wa hii THREAD. Maana hoja hii imejikita kwenye imani zilizojichimbia sana kwenye jamii nyingi za kiafrika na imani hizi zinatutafuna sana tusiweke juhudi ya kung'ang'ania zaidi kuyatafuta yale tunayoamini yanaweza kutuinua kimaendeleo. Imani hizi ndiyo kwa mapana yake watu wanajikuta kwenye kutafuta ndumba zinazodhuru hadi maisha ya watu ili wapate kinachoitwa ngekewa au waondoe nuksi!

Suala hilo linawatatiza zaidi watu ambao hawajaelimika. Kadri jamii au watu wanavyoelimika zaidi ndiyo jinsi ambavyo imani kama hizo zinapungua! Mtu aliyeelimika hutamjua kwa kumiliki vyeti na madigrii bali utamjua kwa anayojiamini na kwa matendo yake, mtu aliyeelimika anatarajiwa ahusishe kufikiri juu ya ukweli wa lile analoliamini na siyo kukariri mambo kama tunavyokaririshwa bila kuhoji vitabu vya dini!

NGEKEWA au NUKSI ni maneno ambayo huyatumia watu wanaojifariji kwa kutafuta majibu rahisi kwa masuala magumu! Mtu aliefanikiwa watu humwelezea kuwa ana NGEKEWA na mtu aliyeshindwa kufanikiwa humchukulia ana NUKSI. Dunia ya leo (ya sayansi na technolojia) mtu ambaye bado anaamini hivyo atachelewa sana au ataishia kubaki nyuma! Mtu anaedhani ana mkono mbaya na akaamini hivyo huyo maendeleo hawezi kuyapata kamwe!

Hakuna binadamu anaeng'ang'ania kujifunza jambo akashindwa kulijua, tunaweza kutofautiana spidi ya kuelewa jambo tunapojifunza lakini mwisho wa siku mtu utaelewa tu, ndiyo maana tunavaa suluali, mashati na viatu kwa usahihi, kwenye vyoo vyetu vya shimo tunalenga vizuri tu, yote haya tulijifunza hatukuzaliwa tukijua yote haya na kama huamini kumbuka jinsi mtoto anavyopishanisha matundu anapoanza kufunga vifungo vya shati siku za mwanzo, au kubadili viatu mguu kulia kuvaa kushoto.

Ikitokea mtu umefanya jambo mara moja, mbili, tatu hata mara nne usifanikiwe siyo sahihi kujichukulia kwamba una nuksi au unadamu mbaya! Kama una imani juu ya jambo unalolifanya kwamba ukilimudu kulifanya linaweza kukuinua basi wewe endelea kulifanya tu maana kadri unavyoendelea kupiga mieleka ndiyo unavyozidi kulielewa vizuri zaidi mwishoni kitaeleweka tu.

Kuhusu mfano wa mpandaji wa hoho ulioutoa anaweza akawa na mkono mbaya kwa maana ya kwamba hajui kupanda hoho! Je alikuwa anapanda kwa usahihi? Ni rahisi sana kufanya utafiti ili kujua kama ni mwili wake ndiyo wenye nuksi na siyo kwamba hajui kupanda. Aende akapande sehemu tatu tofauti na watu wengine ili ionekane kama kote huko matokeo ni yale yale! Ikitokea hivyo tueleze hapa JF tumtangaze huyo Bwana maana wenzetu wa nchi zilizoendelea huyo jamaa kwao atakuwa kivutio kikubwa sana cha utalii na itabidi wampime hata damu yake waichunguze! Kwamba yeye kila akipanda hoho haziponi au hazizai au hazisitawi lol!

Kupanda miche au mbegu siyo ni kule kufukia mche kwenye udongo tu, kuna mbinu zake! Kwenye kilimo cha vitunguu na mpunga mimi mwenyewe nimewahi kukutana na baadhi ya wapandaji wangu vibarua kadhaa ambao wamewahi kunisababishia hasara kwa miche waliyopanda kufa au kutokusitawi vizuri! Hii ilitokana na wao wanapopanda wanashika miche vibaya, wanaishikia katikati ya mche na kuizamisha hivyo hivyo kwenye udongo na inajikunja kama herufi ya U, yaani majani na mizizi inatokeza juu, shina ndiyo linazamishwa chini! Yaani mche unapandikizwa lakini ukiutazama unakuta mizizi yote imetokeza juu ya udongo! Mpandaji huyo unakuta ile strip aliyopanda yeye ama miche inakufa au inakuwa dhaifu tofauti kabisa na walikopanda wengine! Mpandaji huyu akisakamwa kuwa akipanda miche inakufa au haizai vizuri atajiona ana mkono mbaya! Kuna mifano mingi tu ya aina hii ambapo watu kwa kuwa makini wengine wanafanikiwa na kuitwa wana ngekewa au damu nzuri na wengine kwa kutokuwa makini hawafanikiwi na wanaonekana wana damu mbaya au nuksi!

Kwa hiyo Mkuu chama2chawa kujibu hoja yako kuwepo ngekewa au kutokuwepo ngekewa kwenye eneo lolote la maisha inategemea wewe ni mtu wa mlengo gani! Watu walioelimika hilo wala siyo suala la kujadili kabisa!

Kuna jambo moja tu kwa uhakika kabisa ambalo lipo nalo linaitwa CHANCING hilo kwa hakika lipo! Kwa mfano ugonjwa wa kuku unaweza kukumba eneo fulani tu eneo lingine kuku wakasalimika; mvua inaweza kunyesha eneo fulani watu wakaokoa mazao na eneo lingine isinyeshe yakakauka; mtu anaweza kuuza hoho sokoni leo, kesho yake jirani yake akaingiza mzigo sokoni akakuta bei imeshuka au imepanda, unaweza kununua chanjo imekufa bila kujua kuku wako wakaugua na kufa jirani yako akaenda nunua kwingine chanjo nzima akatibu kuku wake wakabaki salama n.k. Lakini wataalamu wanasema kuwa kunachochangia sana kwenye mafanikio ya shughuri mbalimbali asilimia 5% ni CHANCING, na 95% inatokana na Management! Kwa hiyo iwapo kama chancing ni NGEKEWA (au NUKSI) mchango wake kwenye kufanikiwa ni asilimia 5% tu si kitu cha kutegemea wala si kitu cha kuhofia.
 
Kubota
Mama Joe
guta
Mama timmy

Hebu litazameni hili lililonipata jana baada ya Mi nikiwa Safari niliporudi nikakuta kuku mmoja mtetea amekufa ndani ya banda na hata hakuonyesha dalili yoyote na leo nikajaribu kutafuta watalaam nikakuta leo ni siku ya mapumziko na nipo nikachukua maamuzi ya kuzika.

Je? Kwenu haya yanatokeaga? Na hata nimejaribu kumpigia guta RETI na bila ya mafanikio baada ya simu zao kutopokelewa.

NAOMBENI USHAURI WENU WANDUGU!

Asanteni sana![/QUOTE

Mkuu LiverpoolFC nipo ndugu yangu namalizia weekend unajua
nasisi washinda porini mgodi ukitema weekend tunaenda kujipumzisha kwenye viti virefu kidogo.

Pole sana ndugu yangu kwa kifo cha mtetea wako wa mbegu bila shaka! Kusema kweli nimewahi kukutana na mikasa ya hivyo mara kadhaa! Kuna wakati ni nyoka alikuwa akiingia bandani na kuwadunga kuku! Na kuna wakati kuku anaweza kuwa amekula kitu cha kumdhulu! Nakumbuka siku moja nimekaa zangu home kuku alikuja kutoka alikotokea kama vile anakuja kushitaki jambo kwangu, alikuja akikimbia aliponikaribia nilipokuwa nimekaa akawa kama anapepesuka na kutandaza mabawa akawa anatoa ulimi nje kama vile kuna kitu amekula kimemkwama kooni, mara alitoa kama maji mdomoni, akawa anaruka ruka, baada kama ya dakika hivi kuku akawa amekufa! Just like that! Sasa yanapotokea hayo kama hapo karibu kuna mtaalamu wa mifugo mzuri mpelekee ingawa atakuchaji, hao jamaa huwa wanaweza kumkagua na kujua iwapo amekufa kwa sumu au kagongwa na nyoka na kadharika.

Pia kagua mazingira yako ujiridhishe kama hakuna uwezekano wa kuwepo nge au nyoka!
 
Kubota hakika hilo la kuwepo juu ya viti virefu weekend hii nimeweza fikiri baada ya kukukosa on line kitambo nikajua lazima tunuru la mkaa imekuweka hewani vema!

Je? Hapo kweli hakuna uwezekano wa mafua kuwepo?


Kubota
Mama Joe
guta
Mama timmy

Hebu litazameni hili lililonipata jana baada ya Mi nikiwa Safari niliporudi nikakuta kuku mmoja mtetea amekufa ndani ya banda na hata hakuonyesha dalili yoyote na leo nikajaribu kutafuta watalaam nikakuta leo ni siku ya mapumziko na nipo nikachukua maamuzi ya kuzika.

Je? Kwenu haya yanatokeaga? Na hata nimejaribu kumpigia guta RETI na bila ya mafanikio baada ya simu zao kutopokelewa.

NAOMBENI USHAURI WENU WANDUGU!

Asanteni sana![/QUOTE

Mkuu LiverpoolFC nipo ndugu yangu namalizia weekend unajua
nasisi washinda porini mgodi ukitema weekend tunaenda kujipumzisha kwenye viti virefu kidogo.

Pole sana ndugu yangu kwa kifo cha mtetea wako wa mbegu bila shaka! Kusema kweli nimewahi kukutana na mikasa ya hivyo mara kadhaa! Kuna wakati ni nyoka alikuwa akiingia bandani na kuwadunga kuku! Na kuna wakati kuku anaweza kuwa amekula kitu cha kumdhulu! Nakumbuka siku moja nimekaa zangu home kuku alikuja kutoka alikotokea kama vile anakuja kushitaki jambo kwangu, alikuja akikimbia aliponikaribia nilipokuwa nimekaa akawa kama anapepesuka na kutandaza mabawa akawa anatoa ulimi nje kama vile kuna kitu amekula kimemkwama kooni, mara alitoa kama maji mdomoni, akawa anaruka ruka, baada kama ya dakika hivi kuku akawa amekufa! Just like that! Sasa yanapotokea hayo kama hapo karibu kuna mtaalamu wa mifugo mzuri mpelekee ingawa atakuchaji, hao jamaa huwa wanaweza kumkagua na kujua iwapo amekufa kwa sumu au kagongwa na nyoka na kadharika.

Pia kagua mazingira yako ujiridhishe kama hakuna uwezekano wa kuwepo nge au nyoka!
 
Last edited by a moderator:
amani
iwe nanyi wadau wa jukwaa hili pia poleni na majukumu ya ujenzi wa
future nzuri kwa kizazi hiki na kijacho.

Inasemekana kuna mbinu mbadala ya kuvipa joto vifaranga,mbinu hiyo ni
kutumia maji ya moto kwenye madumu ya plastiki.Mbinu
hii ufanyika kwa kuvitenga vifaranga na mama zao halafu unavilea kwa
kutumia maji ya moto yaliyo ndani ya madumu katika banda la vifaranga
i.e nursury.

Mimi sifahamu kiundani utumiaji wa mbinu hii kama mjuavyo kila kitu kina hatua zake na kanuni zake kwahiyo, kama kuna mdau yeyote anae fahamu vizuri utaalamu huu wa kutumia maji ya moto
il kuvipa joto vifaranga naomba kufahamishwa namna nzuri ya kutumia hii
mbinu tafadhali.
 
amani
iwe nanyi wadau wa jukwaa hili pia poleni na majukumu ya ujenzi wa
future nzuri kwa kizazi hiki na kijacho.

Inasemekana kuna mbinu mbadala ya kuvipa joto vifaranga,mbinu hiyo ni
kutumia maji ya moto kwenye madumu ya plastiki.Mbinu
hii ufanyika kwa kuvitenga vifaranga na mama zao halafu unavilea kwa
kutumia maji ya moto yaliyo ndani ya madumu katika banda la vifaranga
i.e nursury.

Mimi sifahamu kiundani utumiaji wa mbinu hii kama mjuavyo kila kitu kina hatua zake na kanuni zake kwahiyo, kama kuna mdau yeyote anae fahamu vizuri utaalamu huu wa kutumia maji ya moto
il kuvipa joto vifaranga naomba kufahamishwa namna nzuri ya kutumia hii
mbinu tafadhali.

Kunathread moja nilisoma humu JF imeelezea vizuri kuhusu kitu hii ulioulizia. Jaribu kuitafuta wakati ukisubiria michango ya wanajamii! Nami nikiiona tena nitaku-PM nikuelekeze ilipo uisome.
 
Kubota hakika hilo la kuwepo juu ya viti virefu weekend hii nimeweza fikiri baada ya kukukosa on line kitambo nikajua lazima tunuru la mkaa imekuweka hewani vema!

Je? Hapo kweli hakuna uwezekano wa mafua kuwepo?]

Sidhani kama mafua yanaweza kuua kwa ghafla kiasi hicho, nahisi itakuwa ni sumu au kaumwa na mdudu!
 
Wadau mara ya mwisho niliishia kuelezea kuhusu magonjwa na visumbufu nilivyokutana navyo, mdonde, viroboto, utitiri na chawa. Leo ninaendelea kuelezea kuwa nami pia niliwahi kukabiliana na matatizo ya vifaranga kupata utando mweupe kama siagi machoni, vifaranga kuharisha na uharo kugandamana kwenye njia ya haja kubwa kiasi cha kuiziba kabisa, vinyoya walisumbuliwa na vichwa kuvimba pamoja na ndui!

Huko nyuma niligusia kueleza jinsi ambavyo lishe duni inachangia kwenye baadhi ya magonjwa mengi yanayoshambulia vifaranga! Moja ya magonjwa hayo ni hilo la vifaranga kutoa utando machoni utando ambao ni mfano wa kitu kama siagi nyeupe au mgando wa maziwa mzito mweupe kwenye macho! Tatizo hili linaweza kuwa linachangiwa na ukosefu wa vitamin A. Nilikuwa nikilitatua kwa kuwasafisha macho vifaranga walioathirika kwa kutumia maji na pamba kuondoa huo utando na niliwadondoshea dawa ya macho ya binadamu. Walipona! Sambamba na hilo nilikuwa natafuta majani ya mchicha na kuwaning'inizia bandani na pia nilikuwa ninatafuta mapapai yaliyoiva na niliwawekea pia.

Tatizo la vifaranga kuharisha na uharo kugandamana kwenye njia yao ya haja kubwa hilo nimehangaika nalo kwa kipindi kirefu sana na lilichangia kuua sana vifaranga vyangu kwa kipindi kirefu! Dalili zake zilikuwa vifaranga wakimaliza wiki moja au zaidi wanaanza kuharisha na wanakuwa wanakaa kwa kubanana banana kila wakati! Vifaranga walikuwa wanabanana kama vile joto halitoshi! Wataalamu walisema ni ugonjwa wa pullorum (Pullorum salmonela), wanasema ugonjwa huo hutokea kwa mama zao kupitia mayai kwa hiyo wanapototolewa huwa na viiini vya ugonjwa huo! Walinishauri niwachinje kuku wote nianze upya! Kwa kuona kwamba kuku hao wangeendelea kunizalishia vifaranga wenye magonjwa tayari. Wazo hilo nililiona ni chungu kama kunywa mwarobaini!

Vifo vya vifaranga viliendelea kwa spidi kubwa lakini ilikuwa ni kipindi kile ambacho nilikuwa nikijitengenezea chakula cha vifaranga mimi mwenyewe na nilikuwa nikiwatenga vifaranga na mama zao yaani walikuwa hawachungi! Baadae nilitekeleza wazo la wataalamu niliwauza kuku wote nikanunua kuku wengine wapya kabisa wale 30 niliowasimulia awali! Lakini hata hivyo baada ya kuku hao wapya kuanza kutotoa kuna wakati niliona tatizo hilo likianza kujitokeza tena! Hapo ndipo nilichanganyikiwa na kuanza kuona kizunguzungu lakini sikukata tamaa!

Tatizo hilo la Pullorum nilikuja kulikomesha kwa:
(1) kununua chick marsh baada ya kuambiwa na mtaalamu kuwa kwa kujitengenezea chakula hasa cha vifaranga si rahisi kuchanganya chakula kwa ufanisi ukapata quality diet hivyo vifaranga hupata malnutrition na kuwa dhaifu kwa magonjwa kadhaa.

(2) kuwapatia vifaranga dawa za antibiotics siku chache baada ya kuzaliwa ili kuua vimelea vya magonjwa wanavyokuwa wamezaliwa nayo. Baada ya kuchukua hatua hizo tatizo hilo lilitoweka!

Tatizo la kuku kuvimba vichwa lilikuwa linanipata kwa namna tofauti tofauti, tatizo hili lilikuwa linatokea zaidi kwa VINYOYA (yaani wale vifaranga wakubwa umri wa wiki zaidi ya 5). Kichwa chote cha kinyoya kilikuwa kinavimba, au jicho au shavu liliumuka, unakuta upande mmoja kuku amevimba na kutoa nundu kubwa sana mithili ya katuni! Yaani kuna wakati kuku anavimba minundu kichwani hadi anatisha au kuchekesha kabisa! Kwa namna inayoshangaza na ambayo sijapata maelezo ya kikemikali ni kwamba tatizo hili nilikuwa ninalitatua kwa kuwapaka kuku mafuta ya alizeti! Labda pengine mafuta ya aina nyingine yanaweza kutibu lakini mimi nilitumia mafuta ya alizeti! Mara baada ya kuwapaka, baada ya siku moja uvimbe wote uliokuwepo ulinywea na baadae kuku kupona kabisa! Hadi leo hii kwenye kaya yangu hadi mtoto anajua tiba hiyo kwa tatizo hilo ni kupaka mafuta ya alizeti!

Kadharika tumewahi kuokoa kuku wenye ugonjwa wa ndui kwa kuwapaka mafuta ya alizeti kwenye makovu kwenye vichwa vyao! Ugonjwa wa ndui (fowl pox) dalili rahisi kuziona ni vidonda kwenye ngozi ya kichwani kwa kuku vinyoya na kuku wakubwa. Ugonjwa huu huwapata kuku wa kienyeji VINYOYA ambao wanakaribia kuwa mitetea au majogoo! Vidonda vya ndui huanza kama vidonda vidogo vidogo na baadae huwa manundu manundu. Utaalamu wa kisayansi unasema kuwa ndui huwa haitibiki bali kwa chanjo tu lakini utaalamu pia unaonyesha kuwa unaweza kupunguza makali ya ugonjwa wa ndui kwa kutibu magonjwa nyemelezi yanayoendana na ugonjwa wa ndui! Mimi nilipambana na kutibu magonjwa nyemelezi. Nilitumia kuwapaka kuku mafuta ya alizeti ili kutibu madonda yao pia niliwapatia kuku dawa za kuongezea madini na vitamin na madawa ya antibiotics. Mimi nilifanikiwa kutibu ugonjwa huu na ugonjwa huu kwangu siyo tishio!!

Ukikabiliwa na changamoto ya magonjwa na kama unafursa ya kupata mmea wa mlonge na mwarobaini usikae ukitazama kuku wakigaragazwa na magonjwa, chukua hatua tumia mimea hiyo ni tiba mbadala! Mimi unga wa mashudu ya mwarobaini ilikuwa ni sehemu ya chakula cha kuku kwa hiyo vimelea vya magonjwa vilidhibitiwa mapema sana! Huko mbeleni nitakuja kuwasilisha Miujiza ya Mlonge kama tiba mbadala!

Simulizi itakayofuata ni jinsi nilivyomudu kulinda kuku bila kutumia fensi.......(nawasilisha wakuu) ITAENDELEA
 
Hapo kwenye utando Mfano wa maziwa ya mgando nami kuku wangu huwasumbua sana.hii hupelekea kuku kuwa kipofu au chongo Kama haitatafutiwa ufumbuzi mapema.mimi huwa nawatoa huo utando,nawasafisha halafu nawapaka mafuta ya mgando sehemu husika na inanisaidia sana.nashukuru kwa darasa na mbinu mpya ya mafuta ya alzeti
 
Mungu akubariki mkuu kubota elimu unayo toa itanisaidia sana katika ufugaji wa kuku maana ninampango wa kuanzisha aina hii ya ujasiriamali.Kila raheli nakuombea uzima ili urudi tena kutuelimisha.
 
Mungu akubariki mkuu kubota elimu unayo toa itanisaidia sana katika ufugaji wa kuku maana ninampango wa kuanzisha aina hii ya ujasiriamali.Kila raheli nakuombea uzima ili urudi tena kutuelimisha.
Nashukuru mkuu kama inasaidia, tuendelee kuwa wote na usichoke kutembelea uzi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom