Msaada: Duka la nguo za watoto

Memory

Senior Member
Jun 29, 2011
106
37
WanaJF,
Baada ya kufanikiwa katika maandalizi ya kilimo sasa nimefikia kubuni biashara sambamba na kilimo. Katika harakati za kutafuta biashara ya kufanya nimefikia uamuzi wa kuanzisha biashara ifuatayo:

(i) Nguo za watoto kati ya 0-12yrs na mahitaji yao mengine lakini pia nikijumuisha pamoja baadhi ya mahitaji ya akina mama.
(i) Simu za mikononi na makasha yake.
Hii yote itakuwa katika mkoa wa Mwanza.

Ombi langu kwa wale wenye uzoefu na hii biashara ni kwamba naomba kupata connection na wafanyabiashara wa jumla wa nguo za watoto hapa Tanzania especially Kariakoo lakini pia ninaomba kufahamishwa ni nchi zipi wafanyabiashara wa nguo wa Tanzania wanachukulia nguo zao kwa jumla. Hapa namaanisha nguo ambazo ni affordable kwa watanzania wenye kipato cha kati na cha chini.

Naomba pia nifahamishwe ni nchi gani wafanyabiashara wa simu za mikononi wanapata hii bidhaa. Nilisikia kuwa kuna nchi simu zinauzwa katika mzani na akina mama wa Uganda wanaenda sana huko, je kuna mtu mwenye data za hii biashara? maana zamani ilikuwa dubai lakini siku hizi nasikia dubai hailipi tena. Naomba msaada kwa wazoefu wa hii kazi.

Ushauri katika hii biashara pia utakuwa mhimu sana.
 
Unataka uwe unaenda kuchukua mzigo mwenyewe nje au unataka mzigo ukishatua ndio ununue za kuuza kwa jumla?
 
@Husninyo
Thanks kwa kuonesha nia ya kunipatia data. Kwa kuanzia nitaanza kununua mzigo ambao tayari upo hapa nchini kwa wateja wanaouza jumla then nikipata uzoefu na biashara naweza nikaextend na kufikiria kuchukua mzigo nje moja kwa moja. Hili ndilo wazo langu hasa katika suala la nguo ila nitafurahi kwa ushauri tofauti kwa wazoefu.

Ninapanga kuanza na nguo lakini baadaye baada ya kuona biashara ya nguo imesimama vizuri ndipo nitaongeza biashara ya simu. Kwa upande wa simu ningependa kuzifuata moja kwa moja nje.
Ahsante
 
Habari za asubuhi wana JF

Nakuja tena nikiomba ushauri juu ya biashara kama hii nimekuwa nina interest nayo sana yaa kuuza vifaa vya watoto wachanga mpaka wakubwa kidogo
kwanza nllitaka nijue gharama za kuanziasha hilo duka l. mtaji ni kama shi ngapi hivi

Nahitaji wataalamu waliowahi kufanya hii kitu wanijuze
 
WanaJF,
Baada ya kufanikiwa katika maandalizi ya kilimo sasa nimefikia kubuni biashara sambamba na kilimo. Katika harakati za kutafuta biashara ya kufanya nimefikia uamuzi wa kuanzisha biashara ifuatayo:

(i) Nguo za watoto kati ya 0-12yrs na mahitaji yao mengine lakini pia nikijumuisha pamoja baadhi ya mahitaji ya akina mama.
(i) Simu za mikononi na makasha yake.
Hii yote itakuwa katika mkoa wa Mwanza.

Ombi langu kwa wale wenye uzoefu na hii biashara ni kwamba naomba kupata connection na wafanyabiashara wa jumla wa nguo za watoto hapa Tanzania especially Kariakoo lakini pia ninaomba kufahamishwa ni nchi zipi wafanyabiashara wa nguo wa Tanzania wanachukulia nguo zao kwa jumla. Hapa namaanisha nguo ambazo ni affordable kwa watanzania wenye kipato cha kati na cha chini.

Naomba pia nifahamishwe ni nchi gani wafanyabiashara wa simu za mikononi wanapata hii bidhaa. Nilisikia kuwa kuna nchi simu zinauzwa katika mzani na akina mama wa Uganda wanaenda sana huko, je kuna mtu mwenye data za hii biashara? maana zamani ilikuwa dubai lakini siku hizi nasikia dubai hailipi tena. Naomba msaada kwa wazoefu wa hii kazi.

Ushauri katika hii biashara pia utakuwa mhimu sana.


FYI,uSISAHAU KUNAMATAPELI HUMU PIA. USIFANYA BIASHARA YA KUTUMA HELA UTUMIWE MZIGO BORA USAFIRI KWA GHARAMA KUBWA COZ UNAHITAJI KWA SASA NI UJUZI NA SEHEMUZ AKUNUA MZIGO THEN FAIDA UTAPATA UKIWA SUGU. ALL THE BEST
 
Habari ndugu zangu wajasiriamali humu,Kwa wataalam wa hii biashara nguo za watoto wadogo age 0-5 nataka kuanzisha biashara hii hapa mtaani kwangu,nimepata fremu nzuri ipo barabarani inafaa kwa hiyo biashara naomba msaada wa dondoo juu hii biashara kama mtaji,mahali pa kununua nguo jumla na taratibu nyingine kama zipo Ahsanteni....
 
habari wana JF
naomba msaada wa mawazo na uzoefu kwa wale wanaofanya biashara ya kuuza nguo za watoto wadogo kuanzia umri 0- 10 hv je kwa biashara ya jumlajumla mzigo mmoja wa nguo za watoto bei gani? na vp kuhusu vifaa vya watoto km car seat, vitanda, na vyoo vya watoto navyo vinauzwaje kwa bei ya jumla??
 
Habari wakuu,

Nakusudia kuanzisha biashara ya nguo za watoto wachanga chini ya umri wa miaka miwili.Nahitaji msaada wa mawazo kwa mwenye uzoefu wa hii biashara. Nipo Dar es salaam. Mtaji wangu ni shilingi milion tatu (3000,000/=).
Nawasilisha.
 
Habari wakuu,

Nakusudia kuanzisha biashara ya nguo za watoto wachanga chini ya umri wa miaka miwili.Nahitaji msaada wa mawazo kwa mwenye uzoefu wa hii biashara. Nipo Dar es salaam. Mtaji wangu ni shilingi milion tatu (3000,000/=).
Nawasilisha.
Ushauri wangu, fungua duka la bidhaa za watoto kwa ujumla wake, yaani kuwe na nguo, diapers, mafuta, poda, sabuni, na vifaa vya kuchezea watoto, lenga sehem yenye mkusanyiko wa watu, ukibahatika kwenye makutano ya barabara nyingi, kwa msingi huo mdogo maisha yatasonga vizur tu.
 
Ushauri wangu, fungua duka la bidhaa za watoto kwa ujumla wake, yaani kuwe na nguo, diapers, mafuta, poda, sabuni, na vifaa vya kuchezea watoto, lenga sehem yenye mkusanyiko wa watu, ukibahatika kwenye makutano ya barabara nyingi, kwa msingi huo mdogo maisha yatasonga vizur tu.
Ahsante mkuu kwa ushauri wako,naufanyia kazi
 
Kijana anamtaji wa shilingi laki 4, anataka kufungungua duka la kuuza chupi za kike, sidiria, chupi za watoto, boksa za kiume pamoja [ special] na urembo mdogo mdogo wa kina dada kama rangi za kucha n.k
Eneo amepata amepata Mwanza maeneo buhongwa sokoni,
Kwa yoyote mwenyewe mawazo chanya juu ya biashara hii tafadhari maoni yako ni muhimu, mf; wapi anaweza kupata mzigo nzuri wa kuanzia? Sifa za eneo anapotakiwa kufungua biashara hy? Mzunguko wake ukoje?
Karibuni kwa ushauri
Ahsante!
 
Back
Top Bottom