DA HUSTLA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2012
- 3,663
- 3,882
Jamani wadau naomba mnishauri kuhusu yafuatayo.Nahitaji kufanya biashara ya kusafirisha alizeti lakini sifahamu ABC yake,vile vile kuna watu wananishauri nifanye kusindika kabisa ili nipate faida zaidi lakini sifahamu pia ABC yake.Kwa hiyo naomba mnijuze kama ntafanya kusafirisha wapi ntapata bidhaa na soko lake ntapata wapi ikiwemo bei pamoja na viwango vinavyohitajika.Pia nkifanya usindikaji itanigharimu kiasi gani kumudu kufanya hivyo ikiwemo gharama za vifaa,wafanya kazi pamoja na soko pia kufikia viwango vinavyohitajika,ni hayo tu wakuu naombeni msaada wenu.