Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
Ndugu zanguni
Jana Usiku kuna maeneo nilipata nafasi ya kutembelea baada ya kusikia habari za kutatanisha kuhusu maeneo haya kwanza nilifika kimboka by night pale Buguruni Sheli , Nilipotia mguuu tu upande wangu wa kushoti mbele niliona wasichana umri kuanzia miaka 16 mpaka 20 wakija mbele yangu wamevaa nusu uchi wananiuliza kama nahitaji huduma ya msichana pale , niliposema ndio nikaulizwa nataka aina gani ya msichana baada ya hapo nikaulizwa nataka kwenda nae wapi manake wote wako pale , swali la mwisho ni kama nataka wale wa kinga au si kinga yote haya ni maamuzi yangu mimi mwenyewe kama nataka kinga au la .
Kilichoendelea hapo siwezi kuendelea kuandika hapa kwa sasa lakini wahusika watilie macho eneo lile baada ya hapo nikaenda zangu kinondoni karibu na makaburini hapo nilikutana hata na wakina mama wako wanajiuza wanauliza kijana unataka huduma gani una bei gani gesti ziko jirani tu ukiwa na pesa zako twende kama hutaki jimama basi wana vitoto vyao navyo viko mjini kwa biashara hiyo .
Nikaamua kwenda kabisa makaburudi kule napo ni balaa tupu utazikuta kuna watu wenye heshima zao tu wanapaki magari wanashuka kwenda kuokota msichana pale wanamwingiza ndani ya gari lake ana maliza haja zake basi msichana Yule anashuka wengine huwachukuwa kwenda nao starehe sehemu mbali mbali kasha wanawarudisha mahali pale usiku ule ule au kesho yake inategemea na makubaliano yao .
Safari yangu ya mwisho ilikuwa ni mitaa ya sinza katika bar moja inaitwa kona kuna wasichana pale warembo nao wako katika biashara hiyo wengi wao ni wanafunzi toka chuo cha ustawi wa jamii kijitonyama , hawa ni wasichana ambao baadaye wanaweza kuajiriwa kushika nafasi nyeti katika serikali , makampuni binafsi na mashirika ya ummah hawa hawa ndio customer care wetu katika makampuni ya simu wako kule wanajiuza .
Nyumba nyingi sana za wageni mitaa ya sinza zimegeuzwa madanguro kwa siri haiwezekani ukute wasichana wamekaa tu mbele ya nyumba hizi bila kazi maalumu na muda mwingi wako hapo hapo , utaweza kujiuliza wanafanya kazi hapo ? kama ndio hawana muda wa kupumzika ? au kama ni wageni tu wanapesa za kuweza kuishi kuishi miezi katika nyumba hizo nani ana wafadhili chanzo cha pesa hizo ni wapi kama sio biashara hii ya kujiuza ?
Najiuliza mfano unapokutana na customer care wa kampuni kubwa pale anajiuza unawaza huyu analipwa bei gani katika kampuni yake au katika kampuni hizo hakuna vitengo vya kusimamia maadili ya watu hawa kuwafunza na kuwaonya kuhusu mambo mengine ya kidunia hawa ni vijana size yetu lazima kampuni hizi , wizara hizi na mashirika haya yawe na njia za kuhakikisha wanalelewa vizuri haswa katika maisha yao banafsi tunapokutana na wadada hawa sehemu hizi tunatilia hata mashaka utendaji wao wa kazi katika sehemu husika .
Kuna wakati wanaofanya biashara hizi kukamatwa na jeshi la polisi lakini inapofikia wakati wa kupelekwa mahakamani basi ndio mwisho wa kesi baadhi ya askari hao wanaundugu na wasichana hawa wanapesa pesa basi wanafuta kesi zao au kufanya hujuma zingine kuhakikisha hawapelekwi mbali zaidi ya vituo hivyo vya polisi
Kama kweli huwa wanapelekwa na kufungwa kungekuwa na mifano hai ya wasichana hawa au wanaume hawa wanaojihusisha na biashara haya , kama jeshi la polisi limeshindwa kupambana na biashara hii , kama wazazi na walezi wameshindwa kudhibiti watoto hawa kufanyike kitu mbadala basi kuhakikisha jamii yetu inakuwa salama dhidi ya biashara hii .
Katika nchi zilizoendelea biashara hii imehalalishwa , wanatambulika na wanalipa kodi kuongeza mapato ya serikali , hata huku kwetu tunaweza kuhalilisha lakini kwa sharti la umri na kuhakikisha afya zao ziko salama pamoja na mambo mengine ya kisheria
Nasema ihalalishwe kwa sababu mitaani watu wameshahalalisha watunga sheria wetu ndio wateja wakuu katika biashara hizi , wafanyakazi wetu ndio wateja pia , walimu , na watu mbali mbali kwanini wasitambulike basi wakishatambulika wapimwe kuw ana umri Fulani wa kufanya biashara hii na wawe na maeneo maalumu ya kufanya biashara hiii
Sio kama sasa mtoto miaka 15 nae yuko na dada yake miaka 18 wote wanajiuza , mama zao nao wanajuza lazima kuwe na utofauti Fulani
Jana Usiku kuna maeneo nilipata nafasi ya kutembelea baada ya kusikia habari za kutatanisha kuhusu maeneo haya kwanza nilifika kimboka by night pale Buguruni Sheli , Nilipotia mguuu tu upande wangu wa kushoti mbele niliona wasichana umri kuanzia miaka 16 mpaka 20 wakija mbele yangu wamevaa nusu uchi wananiuliza kama nahitaji huduma ya msichana pale , niliposema ndio nikaulizwa nataka aina gani ya msichana baada ya hapo nikaulizwa nataka kwenda nae wapi manake wote wako pale , swali la mwisho ni kama nataka wale wa kinga au si kinga yote haya ni maamuzi yangu mimi mwenyewe kama nataka kinga au la .
Kilichoendelea hapo siwezi kuendelea kuandika hapa kwa sasa lakini wahusika watilie macho eneo lile baada ya hapo nikaenda zangu kinondoni karibu na makaburini hapo nilikutana hata na wakina mama wako wanajiuza wanauliza kijana unataka huduma gani una bei gani gesti ziko jirani tu ukiwa na pesa zako twende kama hutaki jimama basi wana vitoto vyao navyo viko mjini kwa biashara hiyo .
Nikaamua kwenda kabisa makaburudi kule napo ni balaa tupu utazikuta kuna watu wenye heshima zao tu wanapaki magari wanashuka kwenda kuokota msichana pale wanamwingiza ndani ya gari lake ana maliza haja zake basi msichana Yule anashuka wengine huwachukuwa kwenda nao starehe sehemu mbali mbali kasha wanawarudisha mahali pale usiku ule ule au kesho yake inategemea na makubaliano yao .
Safari yangu ya mwisho ilikuwa ni mitaa ya sinza katika bar moja inaitwa kona kuna wasichana pale warembo nao wako katika biashara hiyo wengi wao ni wanafunzi toka chuo cha ustawi wa jamii kijitonyama , hawa ni wasichana ambao baadaye wanaweza kuajiriwa kushika nafasi nyeti katika serikali , makampuni binafsi na mashirika ya ummah hawa hawa ndio customer care wetu katika makampuni ya simu wako kule wanajiuza .
Nyumba nyingi sana za wageni mitaa ya sinza zimegeuzwa madanguro kwa siri haiwezekani ukute wasichana wamekaa tu mbele ya nyumba hizi bila kazi maalumu na muda mwingi wako hapo hapo , utaweza kujiuliza wanafanya kazi hapo ? kama ndio hawana muda wa kupumzika ? au kama ni wageni tu wanapesa za kuweza kuishi kuishi miezi katika nyumba hizo nani ana wafadhili chanzo cha pesa hizo ni wapi kama sio biashara hii ya kujiuza ?
Najiuliza mfano unapokutana na customer care wa kampuni kubwa pale anajiuza unawaza huyu analipwa bei gani katika kampuni yake au katika kampuni hizo hakuna vitengo vya kusimamia maadili ya watu hawa kuwafunza na kuwaonya kuhusu mambo mengine ya kidunia hawa ni vijana size yetu lazima kampuni hizi , wizara hizi na mashirika haya yawe na njia za kuhakikisha wanalelewa vizuri haswa katika maisha yao banafsi tunapokutana na wadada hawa sehemu hizi tunatilia hata mashaka utendaji wao wa kazi katika sehemu husika .
Kuna wakati wanaofanya biashara hizi kukamatwa na jeshi la polisi lakini inapofikia wakati wa kupelekwa mahakamani basi ndio mwisho wa kesi baadhi ya askari hao wanaundugu na wasichana hawa wanapesa pesa basi wanafuta kesi zao au kufanya hujuma zingine kuhakikisha hawapelekwi mbali zaidi ya vituo hivyo vya polisi
Kama kweli huwa wanapelekwa na kufungwa kungekuwa na mifano hai ya wasichana hawa au wanaume hawa wanaojihusisha na biashara haya , kama jeshi la polisi limeshindwa kupambana na biashara hii , kama wazazi na walezi wameshindwa kudhibiti watoto hawa kufanyike kitu mbadala basi kuhakikisha jamii yetu inakuwa salama dhidi ya biashara hii .
Katika nchi zilizoendelea biashara hii imehalalishwa , wanatambulika na wanalipa kodi kuongeza mapato ya serikali , hata huku kwetu tunaweza kuhalilisha lakini kwa sharti la umri na kuhakikisha afya zao ziko salama pamoja na mambo mengine ya kisheria
Nasema ihalalishwe kwa sababu mitaani watu wameshahalalisha watunga sheria wetu ndio wateja wakuu katika biashara hizi , wafanyakazi wetu ndio wateja pia , walimu , na watu mbali mbali kwanini wasitambulike basi wakishatambulika wapimwe kuw ana umri Fulani wa kufanya biashara hii na wawe na maeneo maalumu ya kufanya biashara hiii
Sio kama sasa mtoto miaka 15 nae yuko na dada yake miaka 18 wote wanajiuza , mama zao nao wanajuza lazima kuwe na utofauti Fulani