BIAFRA -Hiki ni kiwanja cha Siasa, Michezo au Promosheni na Mahubiri?

Iga

Senior Member
Dec 17, 2007
112
6
NINAANDIKA kwa niaba ya vijana wa Kinondoni Biafra na maeneo karibu ambako tunafadhaishwa na kitendo cha kampuni kubwa kama Zena Mobile phones kuvamia uwanja wetu na kutunyima nafasi ya kufanya mazoezi na kushindana na wenzetu hususan katika futiboli.

Hivi hii ndio corporate responsibility ya watu kama Zain? Na katika eneo hili ambako kuna shule za msingi, sekondari, Chuo kikuu na mahospitali je viongozi wetu wa Kinondoni wanaona ni sawa tu kuruhusu shughuli zenye vurugu, makelele na zisizo na ustaraabu hadi saa nne usiku au zaidi?

Nchi imeshindwa kutupa ajira je, mnataka kutunyima hata kujiendelza wenyedwe ili tujiajiri wenyewe jamani?

Mzee Kikwete wewe mwenzetu Kinondoni hebu tuma watu wako uone unyama tunaofanyiwa sisi vijana wa Kinondoni kiasi wenzetu wasiogopa kifo sasa wanadandia mabasi katika mchezo wa kuteleza na roller-skaters ambao ni wa hatari sana. Wengine tena ndio wameishia kwenye ngono kwa kukosa michezo ya kufanya mzee.


Hivi awamu ya 4 inataka ishindwe pia hata katika jambo hili rahisi la kuhakikisha watoto na vijana wa Kitanazania popte walipo wana viwanja na bustani za kuchezea na kupumzikia? Itakuwa aibu kubwa kiasi gani? Tunashindwa michezo kwa sababu michezo yetu inaanzia matawini ya miti na haianzii kwenye mizizi halisi nako ni viwanja vizuri mitaani na vijijini eti?

Tunashindwa hata na Iraq ambao juzi walikuwa wakibomolewa viwanja na bustani zao na Marekani? Hata Gaza na Afghanistan kusiko na utulivu jamani?

Nilitarajia viongozi wa DINI watajenga retreat na makambi ya kisasa nje ya Jiji na watu kama Zain wataweka hata mazoo karibu na jiji badala ya wao nao kuwa ndio sababu ya kuua mchezo Tanzania na kudumaza maendeleo ya vijana!
 
Nchi nzima haina utaratibu - kwa kuongezea hilo, napenda kufahamu hawa vijana wanauza ICECREAM ZA AZAM wamezagaa barabara zote - wanaendesha vibajaji vyao kama vile wanalipa road licence - yaani wanajihesabia haki na magari mengine - saa ingine inabidi uwapishe au unaweza ukawagonga - mbona machinga wanakatazwa kufanya biashara wanakamatwa - hawa wana HAKI GANI YA ZIADA - kuna uonevu mwingi wanafanyiwa vijana - wengine RUKSA wengine WANAZUIWA - haieleweki - Hii wizara ya inayoshughulikia maswala ya vijana iko SERIOUS kweli?? au ni UFISADI tu unaendelea?? Hizi kampuni za simu zinafanya promotion bila utaratibu - zifanye promotion za kuleta maendeleo sio MUSCI tu - ITS TOO MUCH
 
Kaka nakuunga mkono kwa hili. Biafra ilikuwa maarufu kwa mpira enzi za timu kama Five Star nakadhalika. Lakini sasa haieleweki nini kinafanyika pale, maana mara mahubiri, soko la mnada n.k. Biafra irudishwe kama zamani kuwa viwanja vya mpira wa miguu.
 
Tatizo viongozi wa mji hawakupangilia mipango miji toka mwanzo na hivyo imesababisha ukosefu wa maeneo wazi (open space) katikati ya mji au sehemu nyingi tuu jijini, kwa hiyo vichache vilivyopo vinakuwa na multi purpose. Kutokana na kuwa imeshakuwa hivi ilivyo, then kinachotakiwa ni kuwa na uangalizi tuu, mpangilio wa uwanja kutumika na wote kwa utaarabu zaidi na manufaa ya jamii nzima. Wote wanahaki ya kutumia uwanja/viwanja vilivyopo sawa sawa. Maeneo ya shule yenye viwanja vya mpira inaweza kutumika kwa ajili vijana wanaopenda kucheza mpira...kwenye nia pana njia isiwe sababu ya kuacha kucheza mpira na kuingia kwenye makundi mapotovu. Tuangalie how best to use what is here and how to accomodate each and everyone's need. We learn from mistakes and move on, sio kukaa kulalamika na kukosa matumaini.
 
Zaini wana sehemu nyingingi za kwenda kufanya mambo yao. After all ile sarakasi ingekwua free bado tunalipa kwa hela nyingi sana. Watuachie uwanja wetu ambapo kila mtu ana uhuru wa kwenda na mpira wake akacheza akichoka unarudi nyumbani.

Nimegundua kwa nini mafisadi ya mwanzo yaliuza mpaka open space, walijua ni zao hawakufikiria kuwa ni mali ya mtanzania. Awamu ya nne ni sioni kama kuna kitu kinafanyika, wameendekeza ankara mno.
 
Ni vyema kwanza ukangaza maslahi kama ni shabiki wa Voda ama Tigo. Zain sio walioweka pale, Zain ni wadhamini tu. Mama Afrika Ciircus ni kampuni ambayo inajitegemea. Na inabidi uwapongeze kwa kuweka michezo pale badala ya mambo ambayo wengine wanaweka. Hii ni kampuni ya michezo iliyowezesha vijana wa kitanzania toka Magomeni, Temeke nk kupata ajira kwa namna maalumu na kuonyesha vipaji vyao. Ukienda kushuhudia sarakasi zao, walahi utatamani kurudi tena na tena. Na kupitia hapo wamepata soko la kimataifa. Maonyesho hayo yalianzia masaki mwisho, na wametangaza baada ya biafra wataendelea nchi zingine.

Halafu, wewe ni nani kuamua matumizi ya uwanja ule? Ule si uwanja wa timu za vijana, wala wa serikali. Ni uwanja wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), hivyo ni uamuzi wa chama kusema nani autumie kwa malipo. Unaweza hata kutumika kwa ku-park magari.


........ndiyohiyo
 
Back
Top Bottom